Mhariri Tanzania Daima ashikiliwa na Polisi!

Mhariri Tanzania Daima ashikiliwa na Polisi!

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Mhariri wa gazeti la Tanzania Daima Edson Kamukara anashikiliwa na Jeshi la Polisi tangu asubuhi mpaka muda huu.

Taarifa kutoka ndani ya jeshi la polisi hazijaweka bayana kosa la Mhariri huyo ingawa amehojiwa kutokana na habari anazozihariri.

Baada ya serikali kulifungia gazeti la Mwanahalisi gazeti linaloandamwa kwa sasa ni Tanzania Daima.Inadaiwa serikali haifurahishwi na habari mbalimbali zinazotolewa na gazeti hilo hasa taarifa zinazoonekana kukitangaza na kukijenga Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA
 
Wanapoteza muda ,wafanye kazi tuliyowaajiri wafanye.Kwanza waanza na kutafuta wauaji wa viongozi wa dini wakiwapata ndio waanze na waandishi wote hata wa Uhuru na Mzalendo.
 
Hii ni aibu kwa serikali kushindwa kutekeleza ahadi zake na kuishia kuitishia gazeti.
 
Hata wakitaka libaki gazeti la Uhuru liwe peke yake 2015 ndo mwisho wao hao mafisadi

Hii serikali ya vilaza kweli kweli toka lini KIMBUNGA kikazuiwa?? Ingekuwa hivyo marekani na utajiri wao wote walishindwa kuzuia kimbunga cha SANDY; hivyo ccm na serikali yake wajue hawawezi kuzuia mabadiliko kwa kufungia magazeti , the best they will ever achieve ni kuchelewesha mabadiliko at their own peril!!
 
Serikali haifarahishwi na yanayoandikwa kwenye Tanzania Daima, lakiki wanafurahishwa na yanayotangwa na radio Imaan? Au serikali inafurahishwa na mahubiri ya sheikh Ilunga?

Ni vigezo gani vilivyotumika kupima Tanzania Daima lakini vikaacha radio imaan au sheikh Ilunga na DVD zake?

Waziri wa habari anaweza kuwaambia watanzania serikali inaridhishwa na radio Imaan?
 
Mtanzania Daima halifikii hata10% ya watanzania

naona jamaa wanazidi kwenda marikiti
 
Mhariri wa gazeti la Tanzania Daima Edson Kamukara anashikiliwa na Jeshi la Polisi tangu asubuhi mpaka muda huu.

Taarifa kutoka ndani ya jeshi la polisi hazijaweka bayana kosa la Mhariri huyo ingawa amehojiwa kutokana na habari anazozihariri.

Baada ya serikali kulifungia gazeti la Mwanahalisi gazeti linaloandamwa kwa sasa ni Tanzania Daima.Inadaiwa serikali haifurahishwi na habari mbalimbali zinazotolewa na gazeti hilo hasa taarifa zinazoonekana kukitangaza na kukijenga Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA

Tumechoka kusikia uonevu wa kijinga namna hiyo. Mbona uhuru linatukana halikamatwi?
 
Back
Top Bottom