Mawingi
JF-Expert Member
- Oct 23, 2013
- 213
- 44
namskiliza hapa anaongea vzr unafaa kua waziri kivuri wa mambo ya nje.
Namsikiliza waziri kivuli wa wizara Mambo ya nje. Anaongea kwa hoja kama mtangulizi wake Mch. Msigwa. Cha msingi nilichoshika hapa ni kwamba Tanzania inashindwa kufanya maamuzi ya ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kuwa tuko SADC pia. Kwamba hatuwezi kuweka sheria na taratibu zitakazoridhisha mashirikisho yote mawili.Hatima yake ni nchi yetu kusasua na mwishowe kutoa majibu mepesi kwa hoja nzito. Kwamba tunangoja talaka. Kwamba sisi ndio tumeoa. Hoja ni kwamba mbona hatuendi sambamba na wenzetu katika kufikia malengo tuliyojiwekea? Mfano vitambulisho, VISA, n.k. Nchi yetu inaonekana ikipinganani na jirani zetu kwenye kila hoja kisha inakuja kulalamika kuwa tunatengwa.
Viongozi wetu hawa wasituaminishe kwamba tunatengwa bali tunajitenga kwa kuwa tunashindwa kuamua tumtumikie bwana yupi; SADC au EAC.
Huyu WENJE ni MKENYA au MTANZANIA? namsikiliza hapa ITV, jamani ni aibu kwa taifa, hakika hawa ni watu tulionao wanaoweza kuikana nchi yao hivi hivi.
Anaita Kauli za MAWAZIRI, SITTA na MEMBE kuhusu ushiriki wa Tanzania katika EAC kuwa ni matamko ya hovyo hovyo. Hivi WENJE alitaka Tanzania ijikombe kwa WAKENYA, WAGANDA, na WANYARWANDA ili iweje? huyu ni mtu wa aina gani? Hivi ni kweli WENJE hajui chanzo cha Mawaziri hao kutoa matamko hayo? mbona hakupendekeza tangu zamani nini kifanyike pale KAKAGAME alipouona ushauri wa JK kuwa ni upuuzi? WENJE hana habari kuwa hizo nchi anazoziona kama hazina matatizo zimekuwa zikfanya vikao bila kuishirikisha Tanzania? JAMANI naipenda sana TANZANIA na kamwe siwezi kuwa na akili mbovu kama ya WENJE ya kuivua nguo nchi yangu kiasi hiki.
WENJE asifikiri anawashambulia MEMBE na SITTA bali anajidhalilisha yeye kama Mtanzania, anatudhalilisha watanzania ambao tuko tayari kuifia nchi yetu na analidhalilisha taifa la Tanzania kwa ujumla.