mwa 4
JF-Expert Member
- Oct 8, 2013
- 3,390
- 751
Wanabodi niwasalimu nyote habari za jioni,
kwanza kabisa nianze kuwapa pole na shughuri za siku nzima imani yangu tunaafya njema kadri ya mapenzi ya mmwenyezi mungu alivyopendezwa ziwe.
siku chache zilizopita nchi yetu ilikuwa kwenye mjadala mkali kuhusu miamara ya utoaji wa fedha katika A/c ya Tegeta Escrow mjadala ambao uliisha kwa bunge kupendekeza kuchukuliwa kwa hatua mbali mbali kwa wale wote waliohusika kwa namna moja ama nyingine,hii ni pamoja na taasisi mbalimbali ambazo zitaonekana kuhusika katika utoaji wa fedha hizo bila kufuata utaratibu.
Miongoni mwa hatua zilizopendekezwa kuchukuliwa ni pamoja na kuwajibishwa kwa baadhi ya viongozi akiwemo mwanasheria mkuu,waziri wa nishati na madini,waziri nyumba na maendeleo ya makazi pamoja na katibu mkuu wizara ya nishati na madini.
Pamoja na kuwepo kwa viongozi takribani wanne waliopendekezwa kuwajibishwa mimi nitazungumzia waziri wa nishati na madini prf sospeter muhongo kutokana na umhimu wake kwenye wizara ya nishati na madini pamoja na kazi kubwa alizofanya kwenye wizara husika kwa mda mchache ambao ni takribani miaka miwili tu lakini ameweza kufanya mambo makubwa ambayo yako bayana kwa kila mpenda maendeleo.
kwasasa wizara ya nishati na madini chini ya uongozi wa muhongo inafanya uwekezaji mkubwa kila sehemu wenye lengo la kuifanya wizara iweze kujitegemea pasipo kutegemea ruzuku ya serikali,wizara chini ya uongozi wa muhongo sasa inasomeaha watanzania wengi nje ya nchi kwenye taluma za mafuta na gesi kitu amabacho hakijawahi kufanywa na uongozi wowote wa wizara ila muhongo kathubutu,aidha muhongo na jopo lake la uongozi ameipa uhai Tanesco mpaka sasa umeme unakwenda kila kijiji na kupunguza kwa kiasi kikubwa kukatika kwa umeme.
wizara ya nishati na madini chini ya uongozi wa muhongo ipo kwenye uwekezaji mkubwa na plani za mda mrefu ambazo zinapaswa kuungwa mkono na watanzania wote hasa kwenye mradi wa uwekezaji kwenye mafuta na gesi huko mtwara ambao kwa sasa umefika hatua nzuri sana hivyo ni vema waziri muhongo akaendelea kuwepo ili kutimiza ndoto na mipango yake aliyonayo kwenye wizara.
uhusika wa muhongo kwenye kashifa ya EScrow A/C.
Nimefanikiwa kupata tarifa ya CAG sijaona mahala popote muhongo ametajwa kuhusika kwenye hiyo kashifa iwe kwa maneno au kwa vitendo hakuna mahala popote anapotiwa hatiani na ripoti hiyo,kwamantiki hiyo napata shida kuamini mawazo na maoni ya kamati ya PAC ambayo wanadai waliyatoa kwenye ripoti ya CAG mimi nasema hapana ila nahisi siasa imechukua nafasi kubwa zaidi kuliko ukweli na uhalisia wa jambo.
Baada ya kuzungumza na watu wa aina tofautitofauti nimebaini yafuatayo,
waziri wa nishati na madini mh muhongo anachukiwa na baadhi ya watu ambao amewabana wakashindwa kupenyeza mirija yao pale wizarani hasa tanesco na kwenye vitaru vya gesi hapa unamkuta mbunge wa msoma vijijini mh Nimrod mkono na mfanya biashara marufu na mmiliki wa vyombo vya habari kadhaa hapa nchini hawa waliapa kuwa muhongo lazima aondoke kwa namna yoyote ile hapa ndipo nguvu ya pesa nilipoiona kumbe mtu yupo tayari kuacha kulipa watumishi wake kwa miezi miwili ili pesa hiyo iende kumuangusha muhongo nimeshangaa sana.
Lakini pia nimekuta chuki binafsi ndani ya chama cha mapinuzi kwa baadhi ya wabunge kudhani kuwa baraza la mawaziri likibadilishwa wanaweza kuukwaa uwaziri wapo waliofanya jitihada kubwa kuhakikisha kuwa muhongo aondoke kwakuwa nao ni wasomi tena wenye ngazi ya profesa kama muhongo waliamini kabisa akiondoka watapewa wao ikizingatiwa kuwa waliwahi kuwa mawaziri wa hiyo wizara enzi hizi ikiitwa wizara ya maji nishati na madini hapa mtamkuta mzee wetu waziri asiyeshika popote na mbunge wa jimbo mojawapo kule mbeya.
Lakini pia nimekuta msukumo mkubwa wa mashirika kadhaa ya mafuta na gesi yakiwemo simbioni na mengine nao wameshindwa kuchota tena pesa kutoka tanesco kiujanja kama zamani nao walimwaga pesa ya kutosha ili muhongo aondoke kwa namna yoyote ile pesa hizi zilimwagwa kwa wabunge wengi wakiwemo wa chama tawala na upinzani.
kwa upande mwingine nimekuta ugomvi binafsi baina ya mbunge wa simanjiro mh Ole sendeka na Muhongo,kama mtakumbuka muhongo na sendeka wanaugomvi wao binafsi ambao kila mtu anafahamu kuwa sendeke aliwahi kuomba rushwa akiwa kwenye kamati ya kudumu ya bunge ya nishati na madini muhongo akamlipua bungeni ndipo sendeka akaapa kumfanyia kazi muhongo na maswi mpaka waondoke,Lakini walienda mbali zaidi kwa muhongo kutoa cheti cha matokeo ya sendeka aliyokuwa amepata sifuri ndipo ugomvi ulikolea zaidi lakini ugomvi huo mwanzo ulikuwa ni kama utani baina ya watu hao hatukutegemea kuwa sendeka atauingiza mpaka kwenye kuathiri utekelezaji wa mipango ya maendeleo.
chuki kwa muhongo,
Muhongo amechukiwa na baadhi ya watu hasa wafanyabiashara na wanasiasa walioshindwa kupenyeza mambo yao wizarani hasa tanesco na kwenye vitaru vya gesi Lakini pia muhongo anachukiwa na wachache hao kwa kuwa muwazi kitu ambacho watanzania wachache hasa mafisadi hawajazoea kuusikia lakini muhongo alikuwa anausema.
Wito wangu kwa mh Rais na mamlaka ya uteuzi kwa ujumla sisi wazalendo na wapenda maendeleo tunaomba muhongo asiondolewe ili atuondoe kwenye dunia ya tatu kwa kutimiza ndoto zake kwenye miradi kadhaa ya uwekezaji ambayo ameianzisha,
Muhongo ni binadamu hawezi kukosa mapungufu na mazuri pia lakini ukipima mapungufu na mazuri ya muhongo mazuri yake ni mengi kuliko mapungufu kwani mapungufu yake yanavumilika wala hayana madhara katika ujenzi wa jamii mpya kwani hata uongo anaotuhumiwa kuusema bungeni unamadhara gani kwenye maendeleo ya ujenzi wa jamii mpya? Tunamhitaji sana muhongo kwa wakati huu kuliko wakati wowote,mh Rais usimuondoe waziri wa Nishati na Madini tunamhitaji sisi watanzania wapenda maendeleo tusiotoka kwenye familia za kifisadi.
kwanza kabisa nianze kuwapa pole na shughuri za siku nzima imani yangu tunaafya njema kadri ya mapenzi ya mmwenyezi mungu alivyopendezwa ziwe.
siku chache zilizopita nchi yetu ilikuwa kwenye mjadala mkali kuhusu miamara ya utoaji wa fedha katika A/c ya Tegeta Escrow mjadala ambao uliisha kwa bunge kupendekeza kuchukuliwa kwa hatua mbali mbali kwa wale wote waliohusika kwa namna moja ama nyingine,hii ni pamoja na taasisi mbalimbali ambazo zitaonekana kuhusika katika utoaji wa fedha hizo bila kufuata utaratibu.
Miongoni mwa hatua zilizopendekezwa kuchukuliwa ni pamoja na kuwajibishwa kwa baadhi ya viongozi akiwemo mwanasheria mkuu,waziri wa nishati na madini,waziri nyumba na maendeleo ya makazi pamoja na katibu mkuu wizara ya nishati na madini.
Pamoja na kuwepo kwa viongozi takribani wanne waliopendekezwa kuwajibishwa mimi nitazungumzia waziri wa nishati na madini prf sospeter muhongo kutokana na umhimu wake kwenye wizara ya nishati na madini pamoja na kazi kubwa alizofanya kwenye wizara husika kwa mda mchache ambao ni takribani miaka miwili tu lakini ameweza kufanya mambo makubwa ambayo yako bayana kwa kila mpenda maendeleo.
kwasasa wizara ya nishati na madini chini ya uongozi wa muhongo inafanya uwekezaji mkubwa kila sehemu wenye lengo la kuifanya wizara iweze kujitegemea pasipo kutegemea ruzuku ya serikali,wizara chini ya uongozi wa muhongo sasa inasomeaha watanzania wengi nje ya nchi kwenye taluma za mafuta na gesi kitu amabacho hakijawahi kufanywa na uongozi wowote wa wizara ila muhongo kathubutu,aidha muhongo na jopo lake la uongozi ameipa uhai Tanesco mpaka sasa umeme unakwenda kila kijiji na kupunguza kwa kiasi kikubwa kukatika kwa umeme.
wizara ya nishati na madini chini ya uongozi wa muhongo ipo kwenye uwekezaji mkubwa na plani za mda mrefu ambazo zinapaswa kuungwa mkono na watanzania wote hasa kwenye mradi wa uwekezaji kwenye mafuta na gesi huko mtwara ambao kwa sasa umefika hatua nzuri sana hivyo ni vema waziri muhongo akaendelea kuwepo ili kutimiza ndoto na mipango yake aliyonayo kwenye wizara.
uhusika wa muhongo kwenye kashifa ya EScrow A/C.
Nimefanikiwa kupata tarifa ya CAG sijaona mahala popote muhongo ametajwa kuhusika kwenye hiyo kashifa iwe kwa maneno au kwa vitendo hakuna mahala popote anapotiwa hatiani na ripoti hiyo,kwamantiki hiyo napata shida kuamini mawazo na maoni ya kamati ya PAC ambayo wanadai waliyatoa kwenye ripoti ya CAG mimi nasema hapana ila nahisi siasa imechukua nafasi kubwa zaidi kuliko ukweli na uhalisia wa jambo.
Baada ya kuzungumza na watu wa aina tofautitofauti nimebaini yafuatayo,
waziri wa nishati na madini mh muhongo anachukiwa na baadhi ya watu ambao amewabana wakashindwa kupenyeza mirija yao pale wizarani hasa tanesco na kwenye vitaru vya gesi hapa unamkuta mbunge wa msoma vijijini mh Nimrod mkono na mfanya biashara marufu na mmiliki wa vyombo vya habari kadhaa hapa nchini hawa waliapa kuwa muhongo lazima aondoke kwa namna yoyote ile hapa ndipo nguvu ya pesa nilipoiona kumbe mtu yupo tayari kuacha kulipa watumishi wake kwa miezi miwili ili pesa hiyo iende kumuangusha muhongo nimeshangaa sana.
Lakini pia nimekuta chuki binafsi ndani ya chama cha mapinuzi kwa baadhi ya wabunge kudhani kuwa baraza la mawaziri likibadilishwa wanaweza kuukwaa uwaziri wapo waliofanya jitihada kubwa kuhakikisha kuwa muhongo aondoke kwakuwa nao ni wasomi tena wenye ngazi ya profesa kama muhongo waliamini kabisa akiondoka watapewa wao ikizingatiwa kuwa waliwahi kuwa mawaziri wa hiyo wizara enzi hizi ikiitwa wizara ya maji nishati na madini hapa mtamkuta mzee wetu waziri asiyeshika popote na mbunge wa jimbo mojawapo kule mbeya.
Lakini pia nimekuta msukumo mkubwa wa mashirika kadhaa ya mafuta na gesi yakiwemo simbioni na mengine nao wameshindwa kuchota tena pesa kutoka tanesco kiujanja kama zamani nao walimwaga pesa ya kutosha ili muhongo aondoke kwa namna yoyote ile pesa hizi zilimwagwa kwa wabunge wengi wakiwemo wa chama tawala na upinzani.
kwa upande mwingine nimekuta ugomvi binafsi baina ya mbunge wa simanjiro mh Ole sendeka na Muhongo,kama mtakumbuka muhongo na sendeka wanaugomvi wao binafsi ambao kila mtu anafahamu kuwa sendeke aliwahi kuomba rushwa akiwa kwenye kamati ya kudumu ya bunge ya nishati na madini muhongo akamlipua bungeni ndipo sendeka akaapa kumfanyia kazi muhongo na maswi mpaka waondoke,Lakini walienda mbali zaidi kwa muhongo kutoa cheti cha matokeo ya sendeka aliyokuwa amepata sifuri ndipo ugomvi ulikolea zaidi lakini ugomvi huo mwanzo ulikuwa ni kama utani baina ya watu hao hatukutegemea kuwa sendeka atauingiza mpaka kwenye kuathiri utekelezaji wa mipango ya maendeleo.
chuki kwa muhongo,
Muhongo amechukiwa na baadhi ya watu hasa wafanyabiashara na wanasiasa walioshindwa kupenyeza mambo yao wizarani hasa tanesco na kwenye vitaru vya gesi Lakini pia muhongo anachukiwa na wachache hao kwa kuwa muwazi kitu ambacho watanzania wachache hasa mafisadi hawajazoea kuusikia lakini muhongo alikuwa anausema.
Wito wangu kwa mh Rais na mamlaka ya uteuzi kwa ujumla sisi wazalendo na wapenda maendeleo tunaomba muhongo asiondolewe ili atuondoe kwenye dunia ya tatu kwa kutimiza ndoto zake kwenye miradi kadhaa ya uwekezaji ambayo ameianzisha,
Muhongo ni binadamu hawezi kukosa mapungufu na mazuri pia lakini ukipima mapungufu na mazuri ya muhongo mazuri yake ni mengi kuliko mapungufu kwani mapungufu yake yanavumilika wala hayana madhara katika ujenzi wa jamii mpya kwani hata uongo anaotuhumiwa kuusema bungeni unamadhara gani kwenye maendeleo ya ujenzi wa jamii mpya? Tunamhitaji sana muhongo kwa wakati huu kuliko wakati wowote,mh Rais usimuondoe waziri wa Nishati na Madini tunamhitaji sisi watanzania wapenda maendeleo tusiotoka kwenye familia za kifisadi.