Elius W Ndabila
JF-Expert Member
- Jul 17, 2019
- 339
- 677
Mh Rais pole na kazi za kututumikia Watanzania. Ninakupongeza kwa kazi kubwa unazofanya katika kuleta mapinduzi makubwa katika Taifa hili la Tanzania.
Kazi zako zinaonekana na zinaungwa mkono na Watanzania wengi. Wachache wanaokukosoa wanatimiza wajibu wao wa kukuimarisha katika majukumu yako.
Mh Rais ninajua una kazi nyingi na unakosa hata muda wa kupitia kwenye mitandao muda mwingine.
Pamoja na hayo ninaomba niandike haya machache ninaamini kupitia wasaidizi wako ndani ya Chama na Serikali watakufikishia.
Mh Rais afya yako ni muhimu kuliko mambo yote. Watanzania wengi tunafurahishwa na kazi unazofanya lakini pia wanakuhurumia kwa kuwa unaji overload.
Leo nimeshuhudia ukitoka Dodoma ukienda Chato. Ukiwa njiani umetumia muda mwingi kusikiliza kero za Watanzania waliokusimamisha njiani.
Umetumia muda mrefu kuzungumza na kutatua kero za wananchi kiasi ambacho umefanya zaidi ya mikutano 20 kwa siku ya leo.
Mh Rais ninatambua unakerwa na mambo mengi na ndiyo maana unalazimika kufanya kazi muda wote. Binafsi ninaamini Watanzania wanatamani kuendelea kukuona ukiwa Rais wao lakini ukifanya kazi kwa kiasi na kuuruhusu mwili kupumzika.
Umekuwa na mfululizo wa mikutano mingi tena ya kusimama muda mrefu. Shida za Tanzania hazitaisha kwa muda mfupi kwa kuwa zilitengenezwa kwa miaka mingi.
Ninatambua unafanya hivyo ili kujaribu kumaliza kero zote, lakini afya ni mhimu kuliko haya yote.
Mwisho nimalizie kwa kwa kukupongeza kwa kuendelea kuiongoza Tanzania ikiwa na umoja na utulivu mkubwa.
Mungu aendelee kukupigania ili unayotamani kuyaona katika kipindi chako yaendelee kudhihirishwa.
Kazi zako zinaonekana na zinaungwa mkono na Watanzania wengi. Wachache wanaokukosoa wanatimiza wajibu wao wa kukuimarisha katika majukumu yako.
Mh Rais ninajua una kazi nyingi na unakosa hata muda wa kupitia kwenye mitandao muda mwingine.
Pamoja na hayo ninaomba niandike haya machache ninaamini kupitia wasaidizi wako ndani ya Chama na Serikali watakufikishia.
Mh Rais afya yako ni muhimu kuliko mambo yote. Watanzania wengi tunafurahishwa na kazi unazofanya lakini pia wanakuhurumia kwa kuwa unaji overload.
Leo nimeshuhudia ukitoka Dodoma ukienda Chato. Ukiwa njiani umetumia muda mwingi kusikiliza kero za Watanzania waliokusimamisha njiani.
Umetumia muda mrefu kuzungumza na kutatua kero za wananchi kiasi ambacho umefanya zaidi ya mikutano 20 kwa siku ya leo.
Mh Rais ninatambua unakerwa na mambo mengi na ndiyo maana unalazimika kufanya kazi muda wote. Binafsi ninaamini Watanzania wanatamani kuendelea kukuona ukiwa Rais wao lakini ukifanya kazi kwa kiasi na kuuruhusu mwili kupumzika.
Umekuwa na mfululizo wa mikutano mingi tena ya kusimama muda mrefu. Shida za Tanzania hazitaisha kwa muda mfupi kwa kuwa zilitengenezwa kwa miaka mingi.
Ninatambua unafanya hivyo ili kujaribu kumaliza kero zote, lakini afya ni mhimu kuliko haya yote.
Mwisho nimalizie kwa kwa kukupongeza kwa kuendelea kuiongoza Tanzania ikiwa na umoja na utulivu mkubwa.
Mungu aendelee kukupigania ili unayotamani kuyaona katika kipindi chako yaendelee kudhihirishwa.