Mujuni2
Senior Member
- Jun 11, 2008
- 142
- 3
Mh. Waziri mkuu, Miizengo Kayanza Peter Pinda, umekuwa mwepesi wa kutoa majibu ya papo kwa papo kwa maswali yanayohitaji uchunguzi wa kina. Sasa hili la Gongo la Mboto natarajia utatumia umahiri wako Mungu aliokujalia kutoa majibu ya papo kwa papo. Ila Mh. kama ulivyonyoosha kidole kwa wale uliowatuhumu ni waanzilishi wa vurugu za Arusha , basi nategemea kidole hicho hicho kitaelekezwa kwa WAHUSIKA wa Mabomu ya Gongo la Mboto na nina hamu kusikia nani atawajibika? Mungu aendelee kukupa ujasiri kama aliokupa alhamisi ile ukiwa bungeni Dodoma.