Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Tangu Noni ateuliwe kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa TIB benki hiyo imekuwa inategewa fedha za kutosha kwenye bajeti. Katika bajeti ya mwaka huu ilitengewa fedha eti za kukopesha kwaajili ya kilimo. Kwa mtu mwenye akili lazima ujiulize, inakuwaje kwa benki kama TIB ambayo haina mtandao wowote hapa nchini, ikapewa jukumu la kutoa mikopo kwaajili ya kilimo, kwa wakulima walio sambaa nchi nzima ? Mbali na hayo, kuna hili suala la madeni sugu. Hivi sasa wadaiwa wote, waliokopeshwa na serikali katika mazingira yenye utata, yalihamishiwa yote TIB. Hii ni pamoja na fedha zilizolipwa na Benki kuu kwaajili ya mikopo ya makampuni iliyokuwa imeyatolea mdhamana k.m ililipa takribani bilioni 10 kwaajili ya kampuni ya mbunge wa zamani wa Sumbawanga Mh. Mzindakaya. Vivyo hivyo ililipa karibu shs bilioni 100 kwaajili ya Kagera Sugar. Hii ni mbali na mikopo ya pembejeo na import support ambayo yote kwa pomoja inakimbilia kwenye trilioni ya Tshs. Sasa swali langu, hivi hiyo mikopo ilihamishiwa TIB ili iweje?