Mh. Mgimwa eleza ukweli acha mzaha

KALEBE

JF-Expert Member
Aug 11, 2011
773
338
Jamani wa Tz mmemsikia waziri wa fedha Mgimwa kuwa noti za aina mbili mpya na za zamani zitaendelea kutumika hadi hapo wananchi watakapotoa maoni yao kuwa wanataka zitumike noti za aina gani.

Je, ni kweli walishawahi kupita kwa wananchi hata siku moja na kuuliza ni noti za namna gani wanataka zitumike?

Kwani hata leo wakipita jibu liko wazi kuwa tunataka za zamani na siyo hizi mpya kwani mimi binafsi sioni kama kweli ni mpya kwani ndo zinaonekana za zamani kuliko zilizokuwepo hapo awali.

Hivyo basi Mgimwa sema ukweli wako tu kuwa pengine mkakati wenu haukufanikiwa katika hili na kwa njia hiyo taifa limepoteza mabilioni ya shilingi kuchapisha fedha ambayo hatujafaidika nayo hata kidogo.

Maoni yangu je, kabla ya kuzichapisha hizo fedha hawakujua ya kuwa zina ubora wa chini? na kama walijua je, waliotufikisha hapa tulipo watachukuliwa hatua gani za kisheria
?
 
mbona hawakutaka maoni ya wananchi kabla ya kuziprint?aseme tu zilikuwa hela za uchaguzi wa 2010,yani ukiwa ccm bichwa lako unaruhusu lichezewe na watu kama lukuvi kwa kumezeshwa maneno...
 
jamani watz mmemsikia waziri wa fedha mgimwa kuwa noti za aina mbili mpya na za zamani zitaendelea kutumika hadi hapo wanacnhi watakapotoa maoni yao kuwa wanataka zitumike noti za aina gani je ni kweli walishawahi kupita kwa wananchi hata siku moja na kuuliza ni noti za namna gani wanataka zitumike kwani hata leo wakipita jibu liko wazi kuwa tunataka za zamani na siyo hizi mpya kwani mimi binafsi sioni kama kweli ni mpya kwani ndo zinaonekana za zamani kuliko zilizokuwepo hapoi awali hivyo basi mgimwa sema ukweli wako tu kuwa pengine mkakati wenu haukufanikiwa katika hili na kwa njia hiyo taifa limepoteza mabilioni ya shilingi kuchapisha fedha ambayo hatujafaidika nayo hata kidogo maoniyangu je kabla ya kuzichapisha hizo fedha hawakujua ya kuwa zina ubora wa chini na kama walijua je waliotufikisha hapa tulipo watachukuliwa hatua gani za kisheria

Kumbe yapo ya kujivunia kutoka kwa Balali, moja ni kutupatia noti bora
 
Wananchi ndio walitoa maoni ya kuwa na noti mbili? Huu ushirikishwaji umeanza lini? Hapa lazima kuna scandala.
 
Back
Top Bottom