Mh. Jaji Warioba kuunguruma leo ITV

Mh. Jaji Warioba kuunguruma leo ITV

Aisee kwa dakika 5 tu alizoongea ni wazi kwamba serikali 3 haziepukiki...nimeshaona points kadhaa kama ifuatavyo:
1-kasema yale mambo 22 ya Muungano yaliyokuwa kikatiba yamenyofolewa kiholela
2-Wazo la serikali 1 lilijadiliwa kimapana ikaonekana haifai
3-Wabunge wa Zenji wanakuja Tz bara na wann mamlaka kamili ikiwa pamoja na kukagua miradi ya maendeleo na kuwashurutisha halmashauri, wakati watz hawana uwezo huo wakienda zenji..
Na mengine mengi ila ndo UMEME wamekata..hapa Nangurukuru
 
Asante asante mzee Warioba,"usiwatishe wananchi et kwakuwa unataka serikali 2"
Mungu kaa na Warioba
 
tuliofilisika kwa hoja tusijaribu kutumia makanisa na jeshi kuwaburuza wananchi kwenye Serikali 2.
 
...ni uoga tu kukataa shirikisho...
 
Dah, sijui kwanini nimetiririkwa na machozi, huyu mzee ana hekima sana.
 
...dah kabomoa ngome ya wanaojificha nyuma ya neno jeshi litachukua nchi kwa kukosa mshahara,mbona hawakupindua wakati wa idi amini,tulipojifunga mikanda kupambana na nduli..?
 
dakika 45 leo zimekuwa kama dakika 5 tu maana mzee warioba kila anayotiririka na vina ndio hamu ya kumsikiliza inaongezeka
 
"muda wa dk45 umekuwa mdogo, hivyo msiache kutufuatilia katika kipindi hiki jumatatu ijayo tutakuwa tena Mh. Jaji Warioba katika sehemu ya pili ya kipindi hiki. Aksanteni"
 
"Tulichukua maoni pia kwenye kambi za jeshi na kero walizotuambia ni pamoja na kuwapigia mizinga21 maraisi wawili, hili limewakera sana wanajeshi na wameomba lirekebishwe kwani hakuna amiri jeshi wawili ndani ya jeshi au nchi." Warioba
 
"Tulichukua maoni pia kwenye kambi za jeshi na kero walizotuambia ni pamoja na kuwapigia mizinga21 maraisi wawili, hili limewakera sana wanajeshi na wameomba lirekebishwe kwani hakuna amiri jeshi wawili ndani ya jeshi au nchi." Warioba
Wangeongeza hili likiendelea sisi kama wanajeshi tutachukua nchi.
 
...ngoja waimba mipasho waje na mipasho yao,msg imewagonga na bado tunamleta tena warioba...
 
hawa bin fujo bin ghasia alikuwa wapi wakati kipind ikina endeshwa? na paulo mchafu, na baharia wa mtera? au ana subiri Riz 1 amteua kuwa dc au cheo chochote?
 
Back
Top Bottom