Mh. Jaji Warioba kuunguruma leo ITV

Mh. Jaji Warioba kuunguruma leo ITV

Mtauliza maswali yasiyokuwa na maana ili tu kuharibu kipindi na muda uishe.
Ref: timu buku7, Lumumba.
...ingefaa aje kwenye kipima joto, ila huwa anawatuma wakina polepole tu...
 
Kila nikiangalia tume ya warioba nakosa hata mtu wa kumtoa kasoro ilivyokuwa imesheheni watu wenye weledi na wakereketwa wa ccm, hebu tujiulize ni nani leo anaweza akasimama ndani ya ccm kujilingalisha na Warioba, Jaji Augustino ramadhana, Salim, Marehem Mvungi, Mwesiga baregu! tuseme wote hao ni vichaa ila ma ccm tu? Kingine hii rasimu Rais alikabidhiwa baada ya warioba kumaliza kazi kabla haijapelekwa bungeni kama aliona ina mapungufu si asingeruhusu ikasomwe wala kujadiliwa bungeni na mamlaka alikuwa nayo coz yeye ndio katoa hadidu za rejea! Mpaka leo siwaelewi ccm kabisa! wamekomaa s2 ukiwauliza kwa nn hata data hawana za kulidhisha kweli nchi hii mungu saidia tu!
...mkuu kuna wataalamu (proffessionals) toka idara ya takwimu kama sikosei, pia wapo watu toka ofisi ya raisi na waziri mkuu. yaani kuna high ranking personel wengi sana toka serikalini. tatizo jaji warioba aliwaambukiza uzalendo wajumbe wa tume yake woote,ndo maana hawakujali cha ccm wala jk, hapoo ndo chanzo cha vurugu/mgogoro na ccm....
 
Buhohela tunaomba baada ya jaji Warioba aje Hamphrey Polepole ndo pindi lako litakuwa na mashiko.
 
Mhe Jaji Warioba leo usiku kwenye kipindi.cha dakika 45 Itv atakuwa anahojiwa juu ya katiba mpya napia kutoa maoni yake kwa kinachoendelea katika bunge la katiba mpya usikose kutazama Itv ifikapo saa tatu usiku live....
 
Tunachoweza kusema kwa Warioba ni kuonyesha uongozi bora. Kiongozi bora ni yule anayeweza kuwaunganisha watu wa mitazamo tofauti kufanya kazi pamoja na kutoa kitu kimoja bora kwa maridhiano bila tofauti. Mzee Warioba alionyesha hili kwa hali ya juu. Tume ilikubaliana kila ibara bila kupiga kura baada ya mjadala!
 
Ntarudi hapa baada ya kuisha kipindi,,,kwa sasa naifadhi maneno yangu,,,huwa siwaamini wana-ccm,,,anaweza akaja kugeuza kabisa mchezo,,,,kwa kusema hata wananchi hawakutaka seriklali tatu ila wajumbe wenzie wamemshinikiza tu


Tena baada ya kutunukiwa hiyo tuzo
 
mbona ccm wameshaizima mitambo ya itv? itv haiko hewani ilipoanza taarifa ya habari tu wakaipiga pini, hizi ni hujuma za wazi ili warioba asisikike lakini wanasahau kile kipindi kimesharekodiwa na siyo live.
 
Matangazo ya itv yamekatika huku kwetu maeneo ya kibamba,tv zingine ziko on air
 
Matola kuna jinsi ya kuomba kirudiwe!au ni jinsi gani huyu Mzee na timu yake watapewa audience tuwasikie!
 
ni kweli ITV haikuwa hewani.mim niko znz. lakini sasa imerudi sbri tuone hii filamu
 
...anadai mwanzo wa bunge la katiba haukuwa mzuri. Wameanza kuzingatia maslahi ya makundi...
 
...bara 13% walitaka serikali 1,24% walitaka serikali 2 na 64% serikali tatu...
...katiba ya zanzibar imevunja muungano,rais wa zanzibar amepewa madaraka ya rais,inabendera,wimbo...
 
Kumbe mambo mengine ya muungano yaliondolewa kinyemelaaa!!!!! huh!
 
kaeni mkao wa kula, mambo ya takwimu yanawekwa wazi.

"takwimu kwa upande wa bara zilikuwa wazi na kweli kabisa"- Warioba.
 
...maoni ya mabaraza yalikuwa influenced na viongozi kwa maslahi binafsi...
...ni technolojia ndo imetoa takwimu na hakuna uchakachuzi wowote...
...je umemsaliti nyerere ? No wanaosema hivyo ndo wamemsaliti,marais wawili,uhuru wa mahakama,mambo ya muungano yameondolewa kinyemela...watawala wa sasa hawatendi wanayosema wamerithi kwa mwalimu..
 
Back
Top Bottom