Huyu ni DC na kada wa CCM ambaye pia katabia ka ufisadi amekuwa nacho tangu akiwa chuoni pale mzumbe nakumbuka alivyokula pesa za serikali ya wanafunzi (MUSO) akiwa kama Vice President. Jamaa huyu ni hatari sana kwenye issue ya pesa. Kuwa kada wa CCM naona yupo uwanja wa nyumbani kabisa.
Elibariki Kingu said:Mimi Elibariki Kingu Mkuu wa Wilaya ya Igunga,nimesikitishwa na tuhuma zilizotolewa dhidi Yangu kuwa nilipokuwa Makamu wa Rais katika serikali ya wanafunzi(Muso).Mzumbe kwamba niliwahi kula fedha zilizochangwa na wanafunzi
Napenda ifahamike kuwa nimeitumikia ofisi ya wanafunzi (Muso) kwa vipindi viwili mfululizo na nimefanya kazi pale kwa ufanisi na uzalendo wa hali ya juu.
Haijawhi kutokea kabla ya hapo kiongozi wa Muso kuongoza nafasi Moja kwa vipindi viwili, hili kwangu liliwezekana tena nikiwa na umri mdogo.
Ufanisi na uadilifu niliouonyesha katika nafasi hiyo kwa muda wote ulifanya nitunukiwe tuzo ya ufanisi katika uongozi,nimepewa barua za pongezi "letter of appreciation" na menejiment ya Chuo na kupata vyeti vya uongozi uliotukuka.
Tuhuma kuwa kuna pesa za wanachuo nilizokula ndio nazisikia na kusoma kupitia Jamii Forums,ni vema tukaacha mzaha wa kuwapa watu tuhuma bila uthibitisho usio na ukweli wowote.
Kuhusu kuchukua trekta kama ilivyochangiwa humu kwamba nilichukua kwa mgongo wa vijana hili si kweli sijafanya hivyo kwa kuwa mgongo wa yeyote ni vema wakaanza utamaduni wa kumuogopa Mungu kwa kuacha tabia ya kutunga hadithi za kitoto.
Binafsi ninayo trekta niliyokopa kupitia taratibu zote za ukopaji na zile za kiserikali na so vinginevyo.
Pia nimewezesha kuleta trekta nne katika wilaya ya Igunga ambayo leo yanakabidhiwa kwa wakulima waliojiunga katika vikundi, zoezi hili litafanywa na katibu mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana.
Kuhusu mgogoro wa wafugaji na wakulima Igunga ieleweke kuwa ni wakulima wa Igunga ndio waliovamiwa na wafugaji kutoka Kishapu na wakauliwa zaidi ya watano.
Katika migogoro hiyo ya ardhi Mimi ni kiongozi niliyeweza kuweka rekodi kwa kutatua migogoro mikubwa ya ardhi ikiwemo ya Mwanzugi, Mgogoro uliodumu kwa miaka 12.
Niliweza kuumaliza kwa katika kipindi kifupi cha uongozi wangu na ilipelekea ripoti ya mgogoro huo kutatuliwa kutangazwa katika vyombo vya vya habari vikubwa duniani ikiwemo CNN na BBC nami kupata pongezi kutoka lands zote za dunia.
Hiyo sihusiki wala kuendesha mashamba ya umwagiliaji Igunga kwa kuwa sina tabia ya kujilimbikizia Mali
Kuhusu malalamiko ya mapunjo ya fidia ya umeme kwa wananchi wa Igunga Mimi ndiye niliyeshughulikia kero hiyo kwa kuagiza Takukuru kuchunguza na kuwachukulia hatua waliohusika na malipo.
Sihusiki kwa namna yoyote na ubadhirifu wala sijawahi kutuhumiwa kwa kukosa maadili.
Nimeiongoza wilaya ya Igunga kwa ufanisi na kuwa mfano kwa kufungua ajira ya vijana katika sekta ya kilimo na uzalishaji katika maeneo yote.
Nimeweka maridhiano ya kisiasa katika wilaya kwa kutoa uwanja huru kwa vyama vyote name sasa wana Igunga no wamoja.
Hivyo basis mwenye tuhuma dhidi yangu anapaswa azithibitishe badala ya kuandika kwa dhana na dhamira ya kunichafua.
Nimechagua kuwa mzalendo kwa taifa langu nitaishi hivo kwa kufanya kwa bidii na katika taratibu zinazokubalika, nitajitoa na kujituma kwa ajili ya watanzania popote nitakapokuwa huku nikiongozwa na dhamira njema kwa nchi yangu
Ni mategemeo yangu kuwa haitajitokeza tena
Wenu Elibariki Kingu
Mkuu wa wilaya Igunga.