Habari za kuaminika zinasadikisha kuwa leo Jumatatu kutakuwa na mgomo wa Madereva wa hiace (daladala). Chanzo cha mmgomo ni kuwa wamechoshwa na faini zinazotozwa na jeshi la polisi, pamoja na maadili mabovu ya polisi. Polisi wanalaumiwa kuwa huwa wanajificha katika vichochoro vya Nyumba, au vichaka vya miti vilivyoko karibu na barabara kutegezea madereva, na gari inapokaribia hujitokeza haraka na kuanza kufokea madereva kuwa hawakuwa waangalifu kutiii amri ya kusimama iliyotolewa na polisi, madereva niliobahatika kuongea nao wanasewma kosa liko wapi kama askari wa usalama barabarani watasimama mahali pa wazi kuliko kuishi maisha ya kufumaniana na kulazimishana faini zisizo za lazima, mfano dereva kuonekana kuwa amekataa kusimama kuepusha ajali endapo trafiki amejitokeza ghafla na gari ilikuwa katika mwendo......... MNAOHUSIKA HASA RPC UTATUE TATIZO HILO MAPEMA KAMA LITATOKEA KUTOKUATHIRI MAENDELEO YETU YA KIJAMII, KISIASA, KIUCHUMI NA KIUTAMADUNI...............