Mgomo wa Daladala Dar baadhi ya vituo.... hakuna gari kituo cha simu mawasiliano!!

Mgomo wa Daladala Dar baadhi ya vituo.... hakuna gari kituo cha simu mawasiliano!!

MGOMO DAR Madereva wa daladala wanaotumia kituo cha Simu 2000 Ubungo wamegoma kuingia katika kituo hicho wakilalamikia ubovu wa barabara.
f9a6684523aaa3d37d821739f5b66504.jpg
 
Sababu ni ongezeko la ghafla from 500 to 1000.wamekuja hapa viongozi na matrafiki wamewaambia watoe gari kwa 500 then watakua na kikao SA tano asubuhi but madereva bado wamegoma wamesema wanasubiri mpaka hiyo saa tano kwasababu wana malalamiko mengi na hii Leo imekua kama starting point.



Kwahiyo hayo magari yapo ndani ya kituo hayatoki nje, ama yapo nje ya kituo yamegoma kuingia ndani.
 
Hakuna kusafiri kituo cha daladala cha mawasiliano asubuhi hii kwa wanainchi kutokana na mgomo wa daladala wa ghafla ktk kituo hicho.

Sababu za mgomo hazijulikani!!!
Wana sababu nyingi mojawapo ubovu wa Barabara ya kuingia
 
Hakuna kusafiri kituo cha daladala cha mawasiliano asubuhi hii kwa wanainchi kutokana na mgomo wa daladala wa ghafla ktk kituo hicho.
f9a6684523aaa3d37d821739f5b66504.jpg

Sababu za mgomo hazijulikani!!!


=====

Waendesha daladala wa kituo cha mawasiliano wagoma baada ya kupandishiwa ushuru wa kuingia kituoni kutoka sh 500/= kwenda sh 1000/=

Madereva na makondakta wanalalamikia ushuru huo mkubwa kutolewa na wakati huohuo miunfombinu ya kuingia kituoni kama vile barabara ni mbovu na pia matrafiki wanawakamata ovyo ovyo!

Hali ni mbaya kwani hakuna usafiri na hivyo wafanyakazi wamebaki kuhangaika hapa wasijue cha kufanya!

Mkuu leo nitakuwa tofauti kidogo na Wewe. Mimi nawaona hao Madereva sijui Wamiliki wa Mabasi kuwa ni ' Mapopoma / Wapumbavu ' sana kwani huko nyuma niliwahi kuja na uzi humu humu JF kuwataka wagome kuingiza Magari yao humo Stendi hadi Mamlaka husika ijenge hiyo barabara mbovu na kero ya kuelekea humo ndani na ambayo Abiria wengi walikuwa wakilalamika lakini hawakufanya hivyo na bado wakawa wanapita humo humo.

Leo kuambiwa walipe Kodi hiyo ndiyo wanagoma? Hivi kama wangegoma tokea Kipindi kile hadi barabara hiyo ijengwe leo wasingekuwa na hoja ya msingi ambayo ingeweza kutushawishi hata sisi Kuwatetea? Kwahiyo wanataka hiyo Kodi iondolewe halafu waendelee kutupitisha na kututesa katika hayo ' mahandaki ' yao?

Hivi hao Wamiliki au Madereva wa hayo Mabasi wanajua kwamba endapo hiyo barabara itajengwa katika Kiwango cha Lami inaweza hata kuwavutia Abiria wengi kwenda hapo kinyume na ilivyo sasa ambapo Abiria wengi wanayakwepa mno Magari yanoyopita hiyo njia hali ambayo huenda ikawa ni moja wa sababu ya kuwapunguzia wao mapato ambayo pengine hiyo barabara ingekuwa nzuri wangepata Faida kubwa / nyingi hivyo hata kuweza kulipa hiyo Kodi waliyopangiwa bila wasiwasi wowote?

Wamechelewa sana na nawaona ni ' Wapuuzi ' watupu.
 
Waendelee kugoma watqshangaa feeder za udart zinachukua ruti zao sasa! Hii si awamu ya kulingalinga, walikuwa wapi siku zote kugomea miundombinu mibovu??
 
Back
Top Bottom