Mgomo wa chuo kikuu RUCO Iringa

Ikifika wakati wa kukata pesa waliyokukopesha wako very punctual!!!

Hii nchii hii,,,sijui tuiteje,majina yameisha

Na ukichelewa tu hata kidogo kuanza kulipa unapigwa na faini ya asilimia 10! Natumaini wangekuwa wanawapa watu hizi pesa kwa wakati migomo kama hii isiyokuwa ya lazima ingeweza kuepukwa.
 
Aaaaahhh!;!; kitu cha bure siku zote kinausumbufuuu

kama hujui kitu kunahaja gani ya kuchangia si bora ukasoma hata coments za wenzako tu alokwambia hzo pesa za bure nani ni haki yao si mikopo ilishakuwa alocated kwao na watatakiwa kulipa watakapo ajiriwa hata kama ni mkopo kweli siyo kigezo cha kutokufika kwa wakati ata mim nawaunga mkono maana hamna namna nyingne ndo maana akina lisu wanawaambia serikali chovu watu wanaona porojo! mtafanya mpaka wezi nao watagoma kudai kuongezewa siku maana inaonekana kila kitu bila mgomo hakiwezekani.shame on you and yuor felow mlio na mawazo mgando na fikra finyu kama hzo au wew huna ndugu au yeyote wakarib anayesoma ndo maana vitu hivi havikuumi?
 
Kiukweli wanafunzi vyuoni wana wakati mgumu sana,jana niliongea na mdogo wangu aliyepo ktk moja ya vyuo jijini Dsm,anasema kwa sasa idadi kubwa ya wanafunzi wanashindwa hata kuhudhuria vipindi darasani na kwenda kujisomea ktk maeneo yao ya kujisomea(maarufu kama vimbwetani kwa wale wa Udsm)wanabaki wamelala ktk vyumba vyao kwa sababu ya njaa.Alafu entarahamwee mmoja anakuja hapa anasema eti hao ni ukawa wanawachochea!!inatia hasira!
 
Nyie hata mkisema kuwa ni shinikizo LA wanasiasa sisi hatutaki kujua si tunachojali ni kupewa mpunga wetu na anayesema kuwa ni shinikizo LA kisiasa wewe tuletee hela uone kama utatona barabaran
 
kunapopoma moja lina dai upinzani ndiyo chanzo yawezekana linaongea ukweli ambao likiambiwa liutete litakimbia ila naweza unga hoja mkono maana hawa wapinzani kias chake wamewafanya watu wadai haki zao bila kuogopa keep it up
 
kunapopoma moja lina dai upinzani ndiyo chanzo yawezekana linaongea ukweli ambao likiambiwa liutete litakimbia ila naweza unga hoja mkono maana hawa wapinzani kias chake wamewafanya watu wadai haki zao bila kuogopa keep it up
Wanapaswa kuwa wamelipwa, hao wanafunzi. Tatizo ni cash-flow na banking procedures. Ila najua fedha zimeshaanza kupelekwa. Wenzao wa SUA-SO leo walitinga HESLB na kuambiwa mambo yameanza kuwa mazuri!
 
Sina hakika kama unawajua wanafunzi masikini kwani hao ndio wanaumizwa sana na kuchelewa kwa "Boom". Suluhisho ni serikali kutimiza wajibu wake vinginevyo mwenye njaa atafanya lolote atakalohisi linafaa kwa wakati huo. Huna huruma wewe, hujawahi kuwa masikini - unaniudhi sana kwa mtazamo wako huu.
 
Wanapaswa kuwa wamelipwa, hao wanafunzi. Tatizo ni cash-flow na banking procedures. Ila najua fedha zimeshaanza kupelekwa. Wenzao wa SUA-SO leo walitinga HESLB na kuambiwa mambo yameanza kuwa mazuri!

Laiti majibu kama haya wangekuwa wanapewa wahusika nadhani kusingekuwa na haya yote yaliyotokea tatzo wenye kuhusika na kumaliza matatizo haya ndo hao wanakula viyoyozi 24 hrs wanakuja kuwabandikia tangazo wiki mbili baada ya wiki iliyotakiwa hela kutoka sasa hapo we unategemea nin kama siyo migomo afu masiki watoto wa familia za kipato cha chini ndo wanaumia dada zetu ndo hatar zaidi mungu awanusuru
 
ni shidaaaaaaaaaaaaaaaaaa saaaana maana pesa ni haki yetu tumeandikishana hadi saini so what ucheleweshe:tonguez:
 
hahah nimependa Huyo mkuu wa Polis alivyoongea .

Kajiamini ..
ambomu tumepiga ,alipata mshtuko hayo ni matatizo yake ...mabomu yamepigwa hakuna aliyerudhika .

Iringa kipabele ni amani mengine yanafuata baadae .. kama una matatizo fuata utaratibu wa kikanuni ,na sheria .

kuna wanasiasa waanaacha bunge wanakuja iringa .. hatutaki mambo ya siasa huku .
 
Ukawa wameshindwa kwa Madereva sasa wamehamia kwa Wanafunzi vyuo Vikuu...

Mkuu usitafute pa kutokea, ni sawa na umeshindwa ku-provide service za muhimu kwa familia alafu watoto wako wanakwenda kuiba vyakula kwa jirani wanaleta nyumbani wanakula alafu unasingizia watoto wa jirani wamerubuni, embu hii issue ya wanafunzi itatueni kwanza alafu wakigoma ndio mseme ukawa
 

Siku zote mjinga ndio anawaita wengine wajinga, Kanuni za mkopo unampa MTU kama unazo kama huna ni ahadi ya kusubiri nikipata nitakupa!!!!
 
hao wanafunzi hawana madai ya msingi wanasukumwa na wanasiasa
njaa kila mtu anayo mbona hata kijijini wana njaa wanavumilia------------

Msemaji mkuu
Makao makuu
Sio lumumba

Wewe unajua kitu mkataba! Hao vijijini wanamkataba gani na serikali. Wakati tunaelekea kipindi cha mwisho wa Mkapa ilikuwa neema hiki kituko hakitasahaulika kirahisi!
 

Mkuu, nakubaliana na wewe kwa 100% kwamba migomo hii inachochewa na wanasiasa uchwara, wabinafsi, wavivu wa kufikiri, wavivu wa kutenda kwa wakati, waliochoka kufikiri na ambao hawawezi kutekeleza wajibu wao bila kusukumwa...

Hivi watendaji wa serikali wangetekeleza wajibu wao kwa wakati...
Nani angegoma !?
Nani angekubali kushawisha kugoma wakati ametekelezewa mahitaji yake...!!?

Acha kujitoa ufahamu...Adui wa Serikali ya CCM siyo wapinzani bali ni watendaji wake ndani ya serikali.

Acha kuwasingizia wapinzani kwa uzembe wa serikali...SERIKALI YA CCM IMECHOKA...

Tafakari...
 
Mbona chuo chetu cha kata tumeisha pewa adi imeisha, pole sana aise wadau.
 
Ukiwa na njaa hata kitabu hakipandi. Ila mzigo si umeshaanza kwenda! Wawe na subira!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…