Wadau.
Nimepata taarifa kuwa wanafunzi wa chuo kikuu cha Mandela kilicho Arusha wameandaa mgomo wa kutoingia madarasani kuanzia asubuhi ya leo 4/2/2013. Wakati taarifa hizi zikiendelea kuenea, Makamu mkuu wa chuo hicho prof Mwamila ameomba kuzungumza na wanafunzi wote saa 10 jioni.
Kwa kuwa niko arusha wiki hii, nitafika eneo la tukio asubuhi kujua kama mawasiliano hayo na mkuu wao yanaweza kuathiri mwenendo mzima wa mgomo huo. Pamoja na mambo mengine, wanafunzi hao wanagomea uongozi wa chuo kutoa pesa "kiduchu" kwa wanafunzi wa mwaka wa pili ambao wanaanza tafiti zao (research fund).
Kulingana na "fee structure" ya chuo hicho, wadhamini wanatoa milioni 12.5 kwa ajili ya utafiti kwa wanafunzi wa masters na milioni 37.5 kwa ajili ya wanafunzi wanaofanya PhD. Mtoa habari hizi kanidokeza kuwa kuna watu wanafanya PhD lakini wamepewa pesa chini ya milioni kwa ajili ya research zao. Aibu!
Hata hivyo mtoa taarifa alishindwa kubainisha kuwa ni mgomo wa muda gani (duration).
Nawasilisha!
Source: Nimezungumza na wanafunzi wa Mandela.
Nimepata taarifa kuwa wanafunzi wa chuo kikuu cha Mandela kilicho Arusha wameandaa mgomo wa kutoingia madarasani kuanzia asubuhi ya leo 4/2/2013. Wakati taarifa hizi zikiendelea kuenea, Makamu mkuu wa chuo hicho prof Mwamila ameomba kuzungumza na wanafunzi wote saa 10 jioni.
Kwa kuwa niko arusha wiki hii, nitafika eneo la tukio asubuhi kujua kama mawasiliano hayo na mkuu wao yanaweza kuathiri mwenendo mzima wa mgomo huo. Pamoja na mambo mengine, wanafunzi hao wanagomea uongozi wa chuo kutoa pesa "kiduchu" kwa wanafunzi wa mwaka wa pili ambao wanaanza tafiti zao (research fund).
Kulingana na "fee structure" ya chuo hicho, wadhamini wanatoa milioni 12.5 kwa ajili ya utafiti kwa wanafunzi wa masters na milioni 37.5 kwa ajili ya wanafunzi wanaofanya PhD. Mtoa habari hizi kanidokeza kuwa kuna watu wanafanya PhD lakini wamepewa pesa chini ya milioni kwa ajili ya research zao. Aibu!
Hata hivyo mtoa taarifa alishindwa kubainisha kuwa ni mgomo wa muda gani (duration).
Nawasilisha!
Source: Nimezungumza na wanafunzi wa Mandela.