Akilindogosana
JF-Expert Member
- Jan 12, 2020
- 2,876
- 8,694
Naanza kuona dalili mbaya.
... yuko kazini hivyo!
Wapinzani naona wanapiga mark time tuMgombea Urais kupitia Chama cha ACT Wazalendo pamoja na mgombea mwenza Profesa Omar Hamad leo Agosti 7, 2020, wamechukua fomu ya kuwania Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ofisi za NEC Jijini Dodoma.
View attachment 1529783TAARIFA KWA UMMA
View attachment 1529827
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Mh. Jaji wa Rufaa (Mst), Semistocles Kaijage akikabidhi fomu za kugombea kiti cha Rais kwa Mgombea wa Chama cha ACT-Wazalendo, Bernard Membe katika Ofisi za NEC Njedengwa Jijini Dodoma leo Agosti 7,2020, kushoto ni Mgombea Mwenza, Prof. Omar Faki Hamad . Chama hicho kinakuwa cha nane kuchukua fomu.
View attachment 1529828
====
MEMBE ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA URAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.
Mgombea Urais wa Chama cha ACT-Wazalendo, Ndugu Bernard Kamilius Membe leo tarehe 7, Agosti 2020 amechukua fomu ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Membe amekabidhiwa fomu hiyo ya uteuzi na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage Jijini Dodoma.
Katika uchukuaji huo wa fomu, Membe aliambatana na Mgombea mwenza wake, Profesa Omary Fakih Hamad.
Aidha msafara huo wa Membe uliongozwa na Mwenyekiti wa Chama, Maalim Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu, Ndugu Ado Shaibu, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Ndugu Mhonga Said Ruhwanya, Katibu wa Mambo ya Nje Ndugu Bonifasia Mapunda, Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma, Ndugu Janeth Rithe, Katibu wa Ngome ya Vijana Ndugu Mwanaisha Mndeme na viongozi wengine waandamizi wa Chama.
Akiongea na waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa fomu hizo, Ndugu Bernard Membe amesema kuwa amejiandaa kufanya kampeni kabambe kila Kona ya nchi ili kuipatia ACT Wazalendo ushindi mnono na kuhakikisha ifikapo tarehe 28 Oktoba 2020, utawala wa Rais Magufuli unafikia tamati.
Imetolewa na:
Janeth Joel Rithe
Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma.
Imetolewa leo tarehe 07 Agosti 2020.
Mtu yeyote anayeamini kuwa Membe ni mpinzani basi huyo ana ukichaa ambao hata Mirembe hawawezi kuutibu
Mtaacha lini siasa za kutafuta kura za huruma? Ni kosa la kiufundi kuingia kwenye uchaguzi ukitegemea msaada wa chama kingne. Hakuna chama kilichoanzishwa kwa ajili ya kukisaidia kingine kushinda.hili ni pandikizi kuu la ccm, kazi yake kuu ni kuhakikisha anapunguza kura za upinzani.........mtanielewa siku fulani..
Kila chama viongozi wao wanawaza RUZUKU baada ya uchaguziKwanini Lissu asimuunge mkono Membe?
Makosa ya mwaka 2015 yanajirudia tenaSasa mbona wanatuchanganya siamuachie TL au wote wautaka Urais? Mwaka huu kazi ipo.
ifikapo tarehe 28 Oktoba 2020, utawala wa Rais Magufuli unafikia tamati.
Nafikiri Chama chenye wabunge wengi yani Chadema kwa sasa ndo kinapashwa kutoa mgombea urais sio ACT.Hata sasa wapinzani wamegawanyika kwa kuwa kila mmoja anafikiri anatosha kuingia Ikulu.
endelea na usingizi wako mkuu.Mtaacha lini siasa za kutafuta kura za huruma? Ni kosa la kiufundi kuingia kwenye uchaguzi ukitegemea msaada wa chama kingne. Hakuna chama kilichoanzishwa kwa ajili ya kukisaidia kingine kushinda.
act & chadema huenda kuna kitu wamenusa ndio mana wagombea wao wote wameachwa wachukue form! akipigwa chini mmoja anaungana na mwingine na disco linaendelea.Ila Membe anahangaika nini?
Washauri wake naoni viazi.
Haiwezekani mkuu....... Tundu Lissu yuko kwenye mioyo ya watzAmeshaianza safari itabidi Tundu Lisu amuunge mkono!
Yaaani anatupotezea muda tu......... Usikute kila siku anafanya retirement kule ofisi za tiss kwa kueleza Mikakati ya act na wapinzani......... yuko kazini hivyo!
Huyu hana lengo lolote la kusaidia upinzani......Kivuruge
Unamaanisha ccm??Mbona hampendi demokrasia?
Hahaaa....... Nimekuelewa sn legendary..Huyu Membe ni mpinzani wa Magufuli sio CCM