Mgombea UKAWA Kujulikana Rasmi August 4

Mgombea UKAWA Kujulikana Rasmi August 4

Huu UKAWA ni shida! Ilipaswa mgombea ajulikane zaidi ya mwezi mmoha kuelekea kampeni ili kupunguza tofauti za kiitikadi, 'kumuuza' mgombea kwa wananchi, na kuratibu kampeni vyema, hasa masuala ya bajeti, timu, .... CCM wanapiga kam?peni kwa kusema wanamtambulisha mgombea. Urambuisho huo utafanyika nchi nzima. Nausikitikia upinzani wa Bongo usio na mwelekea sahihi na imara.
Kimbori Usilolijua ni sawa na usiku wa kiza UKAWA wanaenda kwa timing wanajaribu kurekebisha loose ends zote ili watakapoingia kwenye mtanangane wawe kama wale jamaa wa navy seals na snipers wao HAWAKOPESHI
 
Last edited by a moderator:
Kuna tetesi kwamba CHADEMA wakimpokea Lowasa, Slaa atahamia CCM.
 
Hii ni hatari kubwa mpaka inafikia bado siku 90 vyama vinavyojiita mbadala wa chama kilicho madarakani awana MTU sahihi alie andaliwa kuwa raisi wa nchi hii. Kwa taarifa yenu wana Ukawa rais ni Institution kamili yenye mamlaka juu ya nchi hivyo basi ili kuwa pale sharti uwe na vigezo, sio kukulupukia Ikulu ukidhani ni jimbo moja la uchaguzi be serious jamani kama mna dhamila ya kweli ya kuwatumikia watanzania.
 
CCM mbele kwa mbele

Kama vipi mtajeni October 24 kabisaa...manake naona mnapanga na kupangua km vikao vya harusi
 
Hawaaminiki hawa. Kwani si walituambia kuwa mgombea wao atajylikana leo?


Lizaboni wewe ni ccm damu damu. Huna sababu ya kutamka kwa mdomo woga wako wa kuanguka mwaka huu. Unaonyesha kabisa ni namna gani hulali kufight kwa namna yoyote ile ili angalau ccm ipone lakini naomba ndugu yangu ukubali ukweli japo ni mchungu kwamba ccm kwisha kazi.

Juhudi zako za kutaka kuonyesha UKAWA haipo haina nguvu na yote yale ni sawa na kupambana na upepo. Huwezi Lizaboni.

Ninakushauri uwaandae na wenzako kisaikolojia kwamba UKAWa ndio washindi. Ccm siyo inashindwa tu bali inakufa!.

Huna sababu ya kujifanya eti unajivika rangi ya ukawa as if ni kweli kuna kitu ulichokuwa unakisubiri kwa mema. Hapana Lizaboni. Umekua sasa ni vyema ukaonyesha ukomavu.
 
Hawaaminiki hawa. Kwani si walituambia kuwa mgombea wao atajylikana leo?

Kinachojulikana ni kuwa huyo mgombea lazima atatangazwa tu, hakuna haraka.
Anza kujiandaa kisaikolojia mkuu.
Mafuriko yake yatawasomba wote.
 
2010 walichelewa kwa kumsubiri Sitta mwaka huu vile vile bado wanambembeleza Lowasa inamaana ukawa nzima hakuna mwenue mvuto kwa wananchi wa kugombea urais.

Jifunze siasa mkuu, sio kufuata mkumbo usio na maana.
 
Hawaaminiki hawa. Kwani si walituambia kuwa mgombea wao atajylikana leo?
Mkuu kumbuka hakuna siku inayoitwa leo,
hata leo ni leo,kwa hiyo tarehe 4 au 5 mwezi wa 8,ikifika itaitwa leo.
Hivyo tulia.
 
Kumekuwa na sintofahamu nyingi sana juu ya hatima ya nani mgombea wa Ukawa katika uchaguzi mkuu Oktoba 25.

Na sintofahamu hii imekuwa ikitumika na CCM kama sehemu ya propaganda na kuwahadaa wananchi kuwa UKAWA inamigogoro.

Lakini ukweli wenyewe utajulikana Tarehe 4 au 5 ya mwezi wa nane,Akiongea na Sauti ya ujerumani (DW) jana mchana katibu mkuu wa CHADEMA alisema"Mgombea wa ukawa atatangwazwa tarehe hiyo tajwa hapo juu.

Na ili kuondoa uongo au upotoshwaji unaofanyika kwa makusudi na baadhi ya watu ni vema kusubiri na kuwa wavumilivu kama mwenyekiti wa
CHADEMA alivyosema mwanza na kila kitu kitakuwa wazi siku ikiwadia.

Habari zote zinazosambaa kuhusu uwepo wa Ukawa na Lowassa kujiunga
CHADEMA ni kelele za CCM baada ya mgombea wao Pombe kuanza kuchuja,Na wananchi kuanza kumwona kama ni mtu wa kukurupuka na asie na busara za uongozi.

Iwe ni Dr. Slaa,Prof Lipumba au Lowassa hilo ni jambo linawahusu Ukawa,CCM Ni vema waache kuweweseka na waendelee kutulia dawa iwaingie.

CCM Mlitangulia tu,Na kutangulia si kufika.Ukawa wapo na wanakuja kwa kasi ya kimbuka,Nchi itakaa kimya soon.
Mkuu mbona kauli zinakizanza kila kukicha? Siku ile ya kikao alitokeza Mbatia akasema https://www.jamiiforums.com/attachment.php?attachmentid=269933&d=1437477158
leo tena Katibu Mkuu wa CHADEMA anasema vingine. Kauli ya Mbatia imekanushwa au Mbatia alikuwa akijisemea tu hakuwa anasema kwa niaba ya UKAWA?
 
Kinachojulikana ni kuwa huyo mgombea lazima atatangazwa tu, hakuna haraka.
Anza kujiandaa kisaikolojia mkuu.
Mafuriko yake yatawasomba wote.
Majadiliano bado yanaendelea ndani ya UKAWA? Naona UKAWA tena haipo kinachoendelea ni majadiliano kati ya EL na CHADEMA
 
Ado wanabr magufuli akatwe na ccm ili wamchuku kuwa mgombea wa ukawa
 
Majadiliano bado yanaendelea ndani ya UKAWA? Naona UKAWA tena haipo kinachoendelea ni majadiliano kati ya EL na CHADEMA

Kama UKAWA haipo hao wakina CUF, NLD and NCCR kwanini wasitangaze marais wao?
 
Back
Top Bottom