Mgogoro wa ardhi dhidi ya koo za wakurya, Tarime

Kwisense

JF-Expert Member
Sep 7, 2017
475
1,138
Jamani naandika ujembe huu nikiwa Tarime mjini nikielekea kata ya Kibasuka kijiji cha Nyarwana kitongoji cha Mwara kwenye msiba wa ndg. Magige Mesenda alieuwawa kwenye vita inayopiganwa kati ya kitongoji cha Mwara na Matongo (Nyamongo) kwa sababu ya mgogoro wa ardhi ambao umedumu kwa miaka zaidi ya mitatu sasa, vita hiyo imekuwa ikipiganwa mara kwa mara, na polisi wamekuwa wakifanya juhudi kubwa kuhakikisha usalama wa eneo hilo unaimarika lakini pale polisi wanapokuwa wametuliza amani ya eneo hilo huondoka kurudi vituoni na mapigano kuanza upya tena, na uongozi wa eneo husika umekuwa ukikaa kimya baada ya kuona fujo zimetulizwa bila kulitafutia swala hilo na kulipatia suruhisho la kudumu, hivyo basi baada ya polisi kuondoka kwenye eneo husika wananchi wamekuwa wakiviziana na kupigana, na wanazuiana hata kuchota maji kwa kina Mama kwenye mto Tigite (ambao ndio chanzo cha mgogoro), kuzuia hata wasio wenyeji wa maeneo husika wasipite njiani, kumekuwa kama Israel na Palestine jambo ambalo sisi Watanzania hautajalizoea, jana tu tarehe 30/09/2017 ameuwawa mtu mmoja na watatu kujeruhiwa, hivyo basi naomba ujumbe huu uwafikie Mkuu wa wilaya ya Tarime Mr Luoga, Mh William Lukuvi -WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAKAZI, WAZIRI WA OR-TAMISEMI, Waziri Mkuu Ndg Majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara watutembelee kijijini waone wananchi wanavyopata shida bila kujua hatima ya kilio chao kinapata mwarubaini lini, namba yangu ya simu ni hii 0765196548, nawaomba viongozi wetu mtusikie kilio chetu sisi wananchi wa eneo husika tunapata mateso makubwa sana. Maana kwa imani kubwa tulionayo sisi wananchi wa chini na serikali hii ya AWAMU YA TANO CHINI YA RAIS DKT. MAGUFULI, HUU MGOGORO HAUKUPASWA KUSHUGHULIKIWA HIVYO. Nisaidieni kupaza sauti kwa hilo jambo jamani.
Naomba viongozi wetu tusaidie kumaliza huu mgogoro maana ni wa siku nyingi sana
 
Sioni sababu ya kulinganisha ugomvi wa wakurya,kama palestina na Israel!!!!!Kunya anye kuku akinya bata uharo,Tarime mmoja kauwawa lakn inaonekana kama kitu kikubwa,Mbona juzi wakulima watatu wameuwawa morogoro tena kwa idadi ni kubwa kulinganisha na Tarime lakn comments nyingi hazikutoa mapovu kama Tarime.
 
Ukweli mgogoro baina ya koo za wakurya niwamuda mrefu lakini usio na sababu za msingi.Kimsingi hakuna tatizo la ardhi Tarime bali nimapokeo ya kijinga kuona kuwa eti niujasiri na ushujaa kuua mtu tena ndugu yako kwa kigezo cha kuchukua ardhi.
Wakurya wanaabudu sana koo kuliko utu. Ni aibu sana kwa karne hii watu kuuana kwa misingi ya ukabila.
 
Kuna watu wanajitoa ufahamu (hasa viongozi) juu ya historia na jiografia ya eneo la Mwara na kujaribu, badala ya kutafuta suluhisho kwa hawa Watanzania kuishi pamoja, wanatengeneza historia na jiografia yao mpya ambayo inawajengea uhasama! Kwa nini? Tafuteni sababu!
 
JAMANI NI KWANINI WAKURYA WANA SIFA MBAYA ZA UGOMVI NA UKOROFI.......

HIVI NI LINI MTABADILIKA NDUGU ZANGU NA WATANI ZANGU WAKURYA.

HEBU BADILIKENI HAYA MAMBO YANATOKEA HUKO TARIME IMEFIKIA WAKATI HATA KABILA ZINGINE WANAOGOPA KUOLEWA HUKO .
 
Inanikumbusa mwanzon wa 2000s kulikuwa na vita ya koo mbili pia km sijakosea "wanchoki" na "wanchari" hawa waliweka carrier na roho za viongozi (wazazi wetu) rehani hawa jamaa..
 
Ukweli mgogoro baina ya koo za wakurya niwamuda mrefu lakini usio na sababu za msingi.Kimsingi hakuna tatizo la ardhi Tarime bali nimapokeo ya kijinga kuona kuwa eti niujasiri na ushujaa kuua mtu tena ndugu yako kwa kigezo cha kuchukua ardhi.
Wakurya wanaabudu sana koo kuliko utu. Ni aibu sana kwa karne hii watu kuuana kwa misingi ya ukabila.
Sio ugomvi wa kikabila ni koo ndio zinazopigana, kabila wote ni wakurya.
 
Back
Top Bottom