Kuna kila dalili kwamba kuna mgao mkali sana unakuja kwani dalili hizi zipo wazi kutokana na halia halisi ya kinachotokea sasa.Kila siku sasa kwa takribani mwezi umeme unakatika hovyo si mchana si usiku,kuna nini TANESCO?
kuna kila dalili kwamba kuna mgao mkali sana unakuja kwani dalili hizi zipo wazi kutokana na halia halisi ya kinachotokea sasa.kila siku sasa kwa takribani mwezi umeme unakatika hovyo si mchana si usiku,kuna nini tanesco?
...ni kweli ndugu inakera mno....miaka 53 baada ya uhuru mambo "shaghalabaghala".....halafu pesa nyingi inaelekezwa kwenye posho za wateule wachache na safari nyingi za hovyo hovyo...hata hivyo "mgao" mmbaya zaidi ni kuishabikia "serikali hii dhalimu"....Nakerwa na tabia hii ya katikakatika mkuu,yaani nakerwa mnoooo,ndo maana nimeiweka kwenye tetesi.
mawaziri mzigo wapo wengi, wa kwanza kabisa ni professor muhongo, maneno anayosema na hali halisi ya umeme ni vitu viwili tofauti na sijui kwa nini hatuandamani nchi nzima kwa matatizo kama hayo, bei juu, halafu unaishi gizani, halafu nyanya zetu kwenye mafriji zinaoza
Tuvute subira! Uchumi wa gesi utamaliza tatizo hili na litabaki kuwa historia.