Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,468
- 113,583
Wanabodi,
Habari za masiku.
Leo naendelea na zile makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa. Leo nawaelimisha kidogo tuu kuhusu wafungwa.
Tanzania tunafuata mfumo wa sheria wa Uingereza, ambapo mtuhumiwa aliyeko gerezani, anahesabika "not guilt, untill proven" hivyo wafungwa wote wanaotuhumiwa, bado hawana hatia hadi wathibitishwe na mahakama na kuhukumiwa, hivyo wakiwa watuhumiwa tuu ni binadamu wenzetu, kama binadamu nao pia wana haki zao, na miongoni mwa haki hizo ni haki ya kutembelewa na mwenza na kupata faragha, ambayo inaitwa " Conjugal Visit".
Hii conjugal visit, sio starehe, sio favours, ni haki, ni stahiki, na inafanyika kwa mujibu wa sheria.
Msingi wa sheria zetu zote ni katiba, hivyo conjugal visit iko kwa mujibu wa katiba!.
Haiwezekani akajitokeza mtu kuzuia kwa kauli tuu, jambo ambalo limeruhusiwa na katiba na lipo kisheria.
Kwa vile sheria zetu nyingi, tumezirithi kutoka kwa wakoloni Waingereza, inawezekana lengo la conjugal visit ni starehe tuu na sii miongoni mwa haki za msingi za binaadamu na haki za wanandoa!.
Tukiona sisi hatuzihitaji, the right thing to do, sio kutoa kauli kuzifuta, bali ni kupeleka bungeni muswada wa kukifuta kipengele kinachoruhusu conjugal visits kwa watuhumiwa walioko magerezani. Kwa hapa naomba tutofautishe mtuhumiwa na mfungwa, na kutofautisha jela na mahabusu. Kwa nchi za wenzetu wanaoheshimu haki za binaadamu, wafungwa wanatenganishwa na watuhumiwa, wafungwa ni inmates na ndio wanaokaa jela zao, na watuhumiwa ni remandees wanakuwa na magereza yao ambako hawachanganywi na wafungwa na wana haki zote za kutembelewa hadi haki ya conjugal visits. Haku kwetu, wafungwa wanachanganywa na mahabusu na wanakuwa treated almost the same!.
Ila kiukweli tunakokwenda...
Sijui!.
Kama tumefika mahali haki zinageuzwa kuwa favours kwa kauli tuu, na watu wakakubali, na wakanyamaza, then inawezekana kabisa hata haki ya kuishi pia ikaja kuwa treated as its just a favour!.
Nitafanya mpango wa kuendesha vipindi vya uelimishaji umma kuhusu haki za msingi za binaadamu kupitia vituo mbalimbali vya TV ikiwemo TBC yetu sio tuu ili Watanzania tuelimike na kuzijua haki zetu, bali pia vipindi hivi vitawasaidia sana viongozi wetu kuelewa, umuhimu wa haki za binaadamu na kujua kuwa hakuna aliye juu ya katiba, haiwezekani kiongozi akaibuka na kuzuiahaki zilizotolewa kikatiba na kisheria, na tukawa tunamwangalia tuu au akaachwa hivi hivi bila kuambiwa.
Kwa sasa naomba ninyamaze nisije... maana wale wanaoibuliwa kwenye viroba ndio wenye bahati viroba vyao viliibuka, wasio na bahati, vinazama jumla, na kwa vile huwezi jua bahati yako ikoje, ni busara zaidi kujinyamazia!.
Paskali
Habari za masiku.
Leo naendelea na zile makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa. Leo nawaelimisha kidogo tuu kuhusu wafungwa.
Tanzania tunafuata mfumo wa sheria wa Uingereza, ambapo mtuhumiwa aliyeko gerezani, anahesabika "not guilt, untill proven" hivyo wafungwa wote wanaotuhumiwa, bado hawana hatia hadi wathibitishwe na mahakama na kuhukumiwa, hivyo wakiwa watuhumiwa tuu ni binadamu wenzetu, kama binadamu nao pia wana haki zao, na miongoni mwa haki hizo ni haki ya kutembelewa na mwenza na kupata faragha, ambayo inaitwa " Conjugal Visit".
Hii conjugal visit, sio starehe, sio favours, ni haki, ni stahiki, na inafanyika kwa mujibu wa sheria.
Msingi wa sheria zetu zote ni katiba, hivyo conjugal visit iko kwa mujibu wa katiba!.
Haiwezekani akajitokeza mtu kuzuia kwa kauli tuu, jambo ambalo limeruhusiwa na katiba na lipo kisheria.
Kwa vile sheria zetu nyingi, tumezirithi kutoka kwa wakoloni Waingereza, inawezekana lengo la conjugal visit ni starehe tuu na sii miongoni mwa haki za msingi za binaadamu na haki za wanandoa!.
Tukiona sisi hatuzihitaji, the right thing to do, sio kutoa kauli kuzifuta, bali ni kupeleka bungeni muswada wa kukifuta kipengele kinachoruhusu conjugal visits kwa watuhumiwa walioko magerezani. Kwa hapa naomba tutofautishe mtuhumiwa na mfungwa, na kutofautisha jela na mahabusu. Kwa nchi za wenzetu wanaoheshimu haki za binaadamu, wafungwa wanatenganishwa na watuhumiwa, wafungwa ni inmates na ndio wanaokaa jela zao, na watuhumiwa ni remandees wanakuwa na magereza yao ambako hawachanganywi na wafungwa na wana haki zote za kutembelewa hadi haki ya conjugal visits. Haku kwetu, wafungwa wanachanganywa na mahabusu na wanakuwa treated almost the same!.
Ila kiukweli tunakokwenda...
Sijui!.
Kama tumefika mahali haki zinageuzwa kuwa favours kwa kauli tuu, na watu wakakubali, na wakanyamaza, then inawezekana kabisa hata haki ya kuishi pia ikaja kuwa treated as its just a favour!.
Nitafanya mpango wa kuendesha vipindi vya uelimishaji umma kuhusu haki za msingi za binaadamu kupitia vituo mbalimbali vya TV ikiwemo TBC yetu sio tuu ili Watanzania tuelimike na kuzijua haki zetu, bali pia vipindi hivi vitawasaidia sana viongozi wetu kuelewa, umuhimu wa haki za binaadamu na kujua kuwa hakuna aliye juu ya katiba, haiwezekani kiongozi akaibuka na kuzuiahaki zilizotolewa kikatiba na kisheria, na tukawa tunamwangalia tuu au akaachwa hivi hivi bila kuambiwa.
Kwa sasa naomba ninyamaze nisije... maana wale wanaoibuliwa kwenye viroba ndio wenye bahati viroba vyao viliibuka, wasio na bahati, vinazama jumla, na kwa vile huwezi jua bahati yako ikoje, ni busara zaidi kujinyamazia!.
Paskali