kuna documentary moja niliicheki inaitwa money as debt. ziko tatu ila nimecheki mbili. pesa mara nyingi inavyoingizwa kwenye mzunguko huwa ni deni ambalo linatakiwa kurudi na faida. yaani ikiingia 1000 itatakiwa kurudi 1100,1200 au 1300 kulingana riba. pia inazungumzia historia ya pesa toka enzi za magoldsmith hadi modern banking. inaeleza jinsi mfumo wa pesa wa dunia ulivyo mbaya, mabenki yanavyo tengeneza faida out of nothing na jinsi yanahakikisha watu hawafundishi somo la jinsi pesa zinatengenezwa. itafute ni nzuri sana.
jamaa wamejitahidi kuelezea kote. mfano kila pesa inayoingia kwenye system inatakiwa kuingia kama mkopo na inatakiwa kurudi na riba. yaani kwenye mzunguko inaingia principal ila kurudi inatakuwa kurudi principal+interest. kwa hiyo hela inayoingia kwenye mzunguko ni ndogo kuliko inayotakiwa kutoka. sasa benki kuu kwa kucontrol riba inakontrol kiasi cha pesa kinachotakiwa kutoka kwenye mzunguko.Nafikiri hii imejikita zaidi kwenye mikopo. Benki zina regulate mikopo kwa riba. Lakini gumzo hili limejikita zaidi katika kuangalia pesa zinawezaje kuwa sawia bila noti kupungua au kufurika katika uchumi. Hili ni swali tofauti kidogo (lakini muhimu) na habari ya benki kuu zinavyoweza kutumia monetary policy ku regulate inflation, unemployment and eventually economic growth.
jamaa wamejitahidi kuelezea kote. mfano kila pesa inayoingia kwenye system inatakiwa kuingia kama mkopona inatakiwa kuruudi na riba. yaani kwenye mzunguko inaingia principal ila kurudi inatakuwa kurudi principal+interest. kwa hiyo hela inayoingia kwenye mzunguko ni ndogo kuliko inayotakiwa kutoka. sasa benki kuu kwa kucontrol riba inakontrol kiasi cha pesa kinachotakiwa kutoka kwenye mzunguko.
pia inacontrol kinachoingia. ikipandisha riba watu wanaogopa kukopa na pesa zinapungua na kinyume chake. pia wakishusha riba na hela zikiwa nyingi ajira huongezeka. kwa kushusha na kupandisha riba jamaa huweza kucontrol money supply, thamani ya pesa, employment,mfumuko wa bei na hata economic growth.
Jibu swaliHuu mfumo wetu wa elimu kweli ni shidaaaa. Mpaka mtu anajiunga na jamii forum hajui maana ya pesa, ilianza vipi, inahusiana vipi na uzalishaji, ina maana gani mzunguko wa fedha, kwa nini kuna noti chakavu na mpya? Hii nchi sasa ipo hatarini. Wengi waliopo jamii forum ni watu ambao wameshamaliza sekondari. Lakini elimu ya kawaida ya dunia hwaijui. Maana yake wamenyimwa haki hiyo mpaka mwisho wao. Hii inatisha sana. Kuzaliwa mjinga, kuishi mjinga na kufa mjinga. Basi tujipange walau kizazi kijacho wasiishi ujinga huu.
Hawa wachumi ndio watu wabaya zaidi hata ya wana siasa...mchumi anao uwezo wa kumlisha mwenzie ugali kwa picha ya samaki.ngoja wachumi waje watusaidie mkuu