Mfanyakazi ukiishi nyumba za kota usipokuwa makini unaweza usijenge kwako hadi ustaafu

sepema

JF-Expert Member
Jun 13, 2019
591
1,000
Wakuu salaam....

Husikeni na kichwa Cha mada.

Mwaka 2010 niliajiriwa pamoja na rafiki zangu6 kwenye taasisi 1 ya Serikali. Katika kuturahisishia mazingira ya kazi tuliambiwa Kuna nyumba za wafanyakazi ambapo kwa wakati huo kulikuwa na nafasi ya kukaa wafanyakazi wa3 Kati ya wale6 tulioajiriwa.

Baada ya kujadiliana nani wakae na nani wakapange mtaani, nikabahatika kuwa miongoni mwa wale wa3 waliopata nafasi pale kwenye zile nyumba za taasisi.

Baada ya miaka mi5 wale wenzetu waliopanga nyumba kila mmoja akawa amejenga na kuhamia kwake. Sisi tuliobaki Kwenye nyumba za bure aliyejitahidi sana alikuwa na kiwanja tu.

Siku moja rafiki yangu Kati ya wale waliojenga akanambia "Sepema naomba utoke kwenye hiyo nyumba ya bure ukapange nyumba".

Alinieleza faida nyingi ambapo mwaka 2016 nilikubali kuanza maisha ya kupanga nyumba. Nikawaacha wenzangu wawili pale wasijue nini kimenipata .

Mwaka 2019 nikafanikiwa kujenga nyumba kwenye kiwanja changu nilichokua nimekinunua wakati nipo kota.

Kilichonifanya nijenge ni zile hasira za kuishi kwa masharti kwenye nyumba za watu. Hasira zenye faida.

Wenzangu bado wapo na hawana mpango wa kujenga kwa Sasa.

Nimechunguza wafanyakazi wenzetu wengi tuliowakuta kwenye zile nyumba hawajajenga bado... kwanini hawajajenga ilhali wangine wana zaidi ya miaka 20 pale? Jibu ni moja, zile nyumba za bure wanazoishi hazina usumbufu wowote. Umeme na maji vipo free, wameridhika!

Mwisho, tuishi kwenye hizo nyumba za bure Ila tukumbuke Kuna kesho.

Tafakari, chukua hatua!
 
Aiseee hongera sana, ila kwanini Afrika kujenga ni kila mmoja anawaza na tunaona ni mafanikio??
 
Wahindi wamekaa kwenye nyumba za NHC miaka kibao huku wakifanya biashara kisa zipo mjini na zinawatosha na salama zaidi Yaani maisha simple kumbe wanalalia hela kwa utajiri

Kupanga ni kuchagua
Wengine wamejiwekea malengo mengi hapo
Ila ukitegemea mshahara tu ngumu sana
 
Aiseee hongera sana, ila kwanini Afrika kujenga ni kila mmoja anawaza na tunaona ni mafanikio??
Ni kwasababu ya kero za wenye nyumba. Africa hatuna real estate company nyingi na watu binafsi wenye nyumba za biashara(za kupangisha) wana maisha ya kuunga unga na jicho lao muda wote lipo kwenye hiyo nyumba na kuhesabu siku apokee kodi. Na wengine wanaishi hapohapo na wasio ishi hapo, unakuta kuna wapangaji wasio wastaarabu(hawajaelimika) hivyo kusababisha kero kwa wengine
 
Ukweli Mchungu ni kuwa kwa maisha ya ki Tanzania kujenga ni kitu muhimu kuliko vyote
Ukiwa na sehem ya kutokea inapunguza kiasi fulani ukali wa maisha utaenda kulipigania tumbo lako tu mtaani tofaut na ukawa huna pakuishi maisha yanakupiga mara mbili
Baba/mama mwenye nyumba akikutupia virago nje ni fedhea
 
Wahindi wanaogopa kujenga waha hofu yasije yakawatokea ya Uganda ya idd Amin
Aliwafukuza,ndo maana wahindi wako radhi wabanane kariakoo wachache ndo wamejenga
Wahindi wamekaa kwenye nyumba za NHC miaka kibao huku wakifanya biashara kisa zipo mjini na zinawatosha na salama zaidi Yaani maisha simple kumbe wanalalia hela kwa utajiri

Kupanga ni kuchagua
Wengine wamejiwekea malengo mengi hapo
Ila ukitegemea mshahara tu ngumu sana
 
Kujenga sio kazi,kazi kununua kiwanja
Ukweli Mchungu ni kuwa kwa maisha ya ki Tanzania kujenga ni kitu muhimu kuliko vyote
Ukiwa na sehem ya kutokea inapunguza kiasi fulani ukali wa maisha utaenda kulipigania tumbo lako tu mtaani tofaut na ukawa huna pakuishi maisha yanakupiga mara mbili
Baba/mama mwenye nyumba akikutupia virago nje ni fedhea
 
Back
Top Bottom