sawariya
JF-Expert Member
- Apr 9, 2015
- 388
- 359
Mfanyabiashara Patrick Moshi maarufu kwa jina la Patco aliekuwa anamiliki maduka lukuki pamoja na vituo vya mafuta katika jiji la Dar es Salaam amemwomba Rais Magufuli kuingilia kati mgogoro wake na taasisi moja ya fedha hapa nchini.
Akiongea na EFM jijini Dar es Salaam amesema mgogoro huo uliodumu kwa zaidi ya miaka mitatu umemsababishia hasara ya zaidi ya Bilioni 4 na pia amepata madhara ya kiafya ikiwemo kupata ugonjwa wa kiharusi. Amemuomba Rais kuingilia mgogoro huo ili aweze kupata haki yake.
Akiongea na EFM jijini Dar es Salaam amesema mgogoro huo uliodumu kwa zaidi ya miaka mitatu umemsababishia hasara ya zaidi ya Bilioni 4 na pia amepata madhara ya kiafya ikiwemo kupata ugonjwa wa kiharusi. Amemuomba Rais kuingilia mgogoro huo ili aweze kupata haki yake.