Mfanyabiashara ampiga risasi polisi, ajiua

Mfanyabiashara ampiga risasi polisi, ajiua

ndiyomkuusana

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
668
Reaction score
426
MFANYABIASHARA, Yemuga Fugungu (48), mkazi wa wilayani Bukombe, mkoani Geita, amejiua kwa kujipiga risasi baada ya kudhani amemuua askari wa kituo cha Runzewe, Fortunatus Beatus.

Kamanda wa polisi mkoani Geita, ACP Leonard Paul, ameiambia Tanzania Daima kwa njia ya simu kuwa tukio la mfanyabiashara huyo kujiua lilitokea juzi majira ya saa 2.30 usiku.

Alisema awali gari la mfanyabiashara huyo lilikamatwa na askari wa doria waliokuwa katika eneo la Nyantare kwenye barabara kuu ya Runzewe na Nakanyaki likiwa limebeba kokoto zinazodaiwa kuwa ni za wizi.

Kamanda Paul alisema baada ya gari hilo kukamatwa mfanyabiashara huyo aliyeonekana amelewa alianza kuwafokea askari kwa kuwataka waliachie gari lake hali iliyozua mabishano baina yao.

Alisema katika mabishano hayo Fugungu alitoa bastola na kuwarushia risasi askari na kusababisha majeraha kwa mmoja wa askari waliokuwa karibu na tukio hilo na kujeruhiwa tumboni na pajani kisha mfanyabiashara huyo akakimbia kutoka eneo la tukio.

Aliongeza kuwa baada ya kufanikiwa kukimbia mfanyabiashara huyo aliingia katika nyumba ya jirani ya mwanajeshi wa eneo hilo na kuwalazimisha watu waliokuwa ndani wampatie mavazi ya askari wa jeshi la wananchi na kisha kutokomea nayo nyumbani kwake.

"Yule bwana alikuwa amelewa na alipoona ameshamjeruhi askari akajua amemuua sasa akaenda kwenye nyumba ya jirani ambapo kulikuwa na mwanajeshi aliyekuwa likizo na kulazimisha apewe mavazi ya kijeshi na kutokomea nayo," alisema Paul.

Alibainisha kuwa baada ya mfanyabiashara huyo kuchukua mavazi hayo ya kijeshi alielekea nyumbani kwake ambapo polisi walimfuata kwa lengo la kumkamata.

Alisema wakati askari wakiwa katika harakati za kumdhibiti Fugungu aliendelea kuonyesha ukaidi hali iliyowalazimu askari warushe bomu la machozi katika nyumba aliyojifungia.

"Liliporushwa bomu la machozi yule bwana aliamua kujilipua kwa risasi nadhani alijua kuwa ameshamuua askari wetu kutokana na kumpiga risasi tumboni na mapajani," alisema Kamanda Paul.

Alisema mwili wa mfanyabiashara huyo umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti kwenye Hospitali ya Bukombe.
source: Tanzania Daima
 
Nashawishika kutokubaliana nastoria walioitoa askari kwa mwandishi wa habari. Askari wa doria wanashindwa kumdhibiti mlevi hadi anapata nafasi ya kucheza na silaha yake. Askari wengine (mwingine) alikuwa anfanya nini na silaha yake hadi atoroke. Mudawote mlevi kuomba mavazi ya jeshi kwa jirani na kukimbia askari walikuwa wapi. Je bomu la machozi lililolipuliwa laweza kuwa lilichangia? Wao walijuaje kuwa ilidhani alikuwa amemuua askari ndio maana akajiua?.
 
ndo msemaji kasema hivo!!!!! mie nashindwa kuelewa mwanajeshi aliyelikizo kugawa sare zake, inawezekana vipi?
 
alipigwa na kitu kizito chenze ncha kali.kilirushwa toka upande usiojulikana na warushaji hawakuonekana.. Siiamin stori hi
 
Jana nikiwa Runzewe nikitokea Mwanza, nilipaki gari na kwenda kula kwa jamaa zangu kando ya barabara. Jamaa yangu mmoja maarufu sana Runzewe akaniambia
'Mheshimiwa, unajua kilichotokea jana? Pale ambapo huwa unafikia (Zambabwe Guest) yule jamaa mmiliki wake kulitokea ugomvi na askari police na jamaa kauwawa'.
Nikashtuka sana, maana jamaa alikuwa ni mfanyabiashara hususan akinunua madini ya vijana wanayokwapua toka mgodi wa African Barrick Gold (Tulawaka), na kiukweli alikuwa na chenji nzuri tu.
Kwamba ugomvi ulitokea kituo cha polioce Runzewe na kweli huyo mfanyabiashara alikuwa kalewa na alimfyatulia risasi police.
Baada ya kumfyatulia risasi police, jamaa akaondoka kurudi kwake na kweli alifaulu kufika kwake. Police walifaulu kumfata kwake na wakamchukua kwenda naye mpaka Ushirombo ambapo ndipo makao makuu ya wilaya yapo na hospitali ya wilaya ilipo. Lengo likiwa aambatane na majeruhi askari ili watoe maelezo kwa intelijensia kwa kilichojiri.
Habari za kuaminika kabisa jamaa hakufia nyumbani kwake kama inavyodaiwa, aliwashwa naye risasi Ushirombo na hao hao wana-intelijensia. Vijiwe vyote pale Runzewe wanalijua hilo, na marehemu ikimbukwe alikuwa kawabeba vijana wengi wa Runzewe kuwapa ajira za kutafuta dhahabu.
Usiku uleule police walipomchukua nyumbani kwake marehemu akiwa hai, waliondoka na furushi 2 za begi zilizojaa fedha (noti) ambazo marehemu hukaa nazo kwa ajili ya ununuzi wa dhahabu. Marehemu alikuwa akipendelea zaidi kununulia dhahabu maeneo ya 'mwembeni' na 'mavota', hivi ni vijiji jirani kabisa ya mgodi wa Tulawaka.
Kweli alilewa, ila kauwawa akiwa Ushirombo. Ila kwa haraka sana usiku uleule police walitangaza jamaa kajiua akiwa nyumbani kwake, wananchi wakajiuliza 'mbona wamekuwepo nyumbani kwake na hawajaona maiti kubebwa kupelekwa Hospital kuhifadhiwa?'. Ndipo ufatiliaji ulianza na wananchi kuwasha pikipiki kwenda Ushirombo kushuhudia, waliyoyakuta huko...mh!!!
Source: Wananchi wa Runzewe center, hususan kundi kubwa la vijana linalomsikitia marehemu kuuwawa.
 
Askari wetu ni wauaji hata mwenye akili ndogo hakubaliani na hiyo taarifa ya huyo Rpc . Wameua harafu wanaleta story ya kijinga kwa Watanzania. Kukomesha huo unyama ni kuiondoa ccmpolisi madarakani 2015. Rip mfanyabiashara.
 
police wetu siku hizi hawaaminiki tena. Hata zile silaha wanazoonyesha wamekamata kwa malundo toka kwa majambazi huwa ni fix tu wanaweza yakawa wameyatoa warehouse yao tabora yakaja dar wakaonesha kana kwamba zimekamatwa leo kumbe Uongo mtupu
 
Mmmh! Askar hawa siyo wa kuwaamin hata kidogo,subir siri zitaanza kuvuja tutajua ukweli zaid ya huu,wazee wa vitu vyenye ncha kali!
 
hapana hii habari lazima itakuwa sio kweli, eti arushiwe bomu la machozi na yeye kujiua!!! Big no, hapa kuna kitu kinafichwa na hao Police.
 
dah kaniudhi marehemu kwa kumwacha hai huyo polisi angemuua kabisa.
 
eti "wakarusha bomu kwenye nyumba!!!!!! " . Nani kamuona akijiua? polisi ndio walio muua .
 
Back
Top Bottom