Mfahamu Ndugu MHAMAD SAIDI AL-BESH Mchinjaji Mkuu wa Serikali ya Saud Arabia

aleesha

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
775
1,117
Saudi Arabia ni moja kati ya nchi nne pekee, ambazo bado zinatekeleza adhabu ya kifo hadharani, nchi hizo ni korea kaskazini,Iran,Saudi Arabia,na Somalia.

Nchini Saudi Arabia Serikali ya kifalme inatekeleza adhabu hii kwa msimamo kuwa wanatekeleza shari, Kama ambavyo imeelezwa katika Qur'an tukufu..

Ivyo ikatokea raia amefanya kosa ambalo linapaswa ahukumiwe adhabu ya kifo adhabu hii inatekelezwa kwa mtu huyo kuchinjwa hadharani kwa upanga.

...{SIKU MOJA KABLA YA KUCHINJWA}

Siku moja kabla ya raia kuhukumiwa kifo Saudi Arabia kuchinja hadharani..

Mchinjaji Bwana Al-Besh hutembelea familia ya mtuhumiwa na kuiyomba msamaha,Msamaha huu anaye omba Al-Besh si kwaajili yake bali ni kwaajili ya yule anaye kwenda kuchinjwa kesho yake ili ndugu zake wamsamehe ili aondoke Duniani akiwa hana lawama kwa jamaa zake..

Katika mahojiano ya nadra sana aloyafanya na Arabu news Mwaka 2003.

Al-Besh alieleza ni njnsi gani aliingia katika ajira hii ya kipekee.Al-Besh alianza kazi yake ya kuchinja watu mwaka 1998.

Hapo mwanzo kazi yake ilikuwa Gerezani Maeneo ya taifa, na ilikuwa kuwafunga mikono,na vitambaa vyeusi usoni Wafungwa..!! ambao walipelekwa kuchinjwa hadharani baada ya kuhukumiwa.

Baada ya muda akajikuta anaanza kutamani na yeye kupanda cheo, awe mchinjaji ..

Ikitokea serikali ikatangaza nafasi ya kazi kwa ajili ya mchinjaji ,na bila kusita akaiwania hiyo nafasi haraka na kukubaliwa ombi lake bila pingamizi ..

Mara yake ya kwanza kuchinja mtu ilikuwa Mwaka 1998..

Al-Besh anasema alipo fika eneo la kuchinjia alimuinamisha mtuhumiwa na kumpiga ubapa wa panga shingoni kama ishara ya kumuweka utayari na baada ya hapo ndipo alimshushia upanga kwa kishindo na kutenganisha kichwa na kiwili wili..

Siku yake yakwanza ya kuchinja mtu, anaeleza hakupata usingizi kabisa.lakini baada ya hapo hakuwai kuwa na hofu tena, wala kuukosa usingizi kabisa,

Mpaka sasa amesha chinja mamia ya watu kwa ruhusa ya serikali ya Saudi Arabia na inaelezwa yeye atakuwa ndiye binadamu pekee aliye chinja binadamu wenzake kwa wingi zaidi Duniani na ndiye mchinjaji chaguo namba moja kwa serikali ya Saudi Arabia pale kunapohitajika watu kuchinjwa hadharani baada ya kuhukumiwa.

Besh anasema kuna kipindi anachinja hadi watu kumi na tano(15) kwa siku moja.

Al-Besh anajitetea kuwa yeye si mtu katili kwa sababu ya kazi yake anayofanya kwani anajisikia furaha kufanya kazi yake ya uchinjaji kwa kuwa anaamini kuwa anafanya kazi ya MUNGU,Kama ilivyo elezwa kwenye vitabu...

Pia anaendelea kujitetea kuwa kazi yake haimtengi na jamii kwa kuwa anamarafiki wengi misikitini na mitaani, pia ameongezea kwa kusema ni mtu anaye jisikia furaha pindi apitapo mtaani hunyenyekewa na watu..!! Pia ana ndugu zake ambao wanampenda na wamemuelewa kuhusu chaguzi ya kazi yake hiyo ya ajira..!!!

Sihivyo tu bali Al-Besh anaeleza kuwa huwa anawaruhusu watoto kumsaidia kuusafisha damu usime wake wa kuchinjia pindi atokapo kazini kwenye kuchinja watu deera Square...
 

Attachments

  • image.jpeg
    image.jpeg
    33.7 KB · Views: 69
Kwa hiyo anaamka asubuhi anaaga watoto wake anaenda kazini,better to be unemployed
 
Wauaji na Wanyongaji wapo kila nchi wapo USA Wapo Uk wapo china wapo japani kila nchi wapo!!! au unadhani hata hapa Tz anayeua watu waliohukumiwa kifo hayupo??..sema hao wenzetu hawana unafiki hiyo ndio tofauti
 
Wauaji na Wanyongaji wapo kila nchi wapo USA Wapo Uk wapo china wapo japani kila nchi wapo!!! au unadhani hata hapa Tz anayeua watu waliohukumiwa kifo hayupo??..sema hao wenzetu hawana unafiki hiyo ndio tofauti
Yeah kweli, wenzetu hawapendi unafiki hata kidogo
 
Karithi hiyo kazi kutoka kwa baba yake..tofauti ya jambia na risasi ni ndogo sana,ila electric chair ndio inatisha sana.
 
..... afadhali yeye. Ameajiriwa na anatoa uhai kihalali kabisa. Hajamuonea mtu na wala hajamhukumu kimakosa. Yeye ni kazi tu. Wauaji wametuzunguka labda yeye tumnyooshee kidole kwa vile staili yake ni ya kuchinja.

Kama wewe ni mwanamme na umempa mwanamke uja uzito bilaa nia ya kuitunza hiyo mimba na akaitoa basi na wewe ni muuaji pia.

Kama wewe ni Dr na umezembea kazini ikatokea mgonjwa ameaga dunia na wewe ni muuaji pia.

Dereva unaeendesha gari kiholela ukiwa umelewa ama bila umakini na ukasababisha ajali basi na wewe umo.

Kiongozi unaeshawishi vikundi mbali mbali vya watu kutofautiana na kusababisha vita na vifo ni muuaji pia.

Akina Mama na baba mnaopigia debe ukeketaji wa mabinti na kupelekea vifo vyao na vyie mna taji la kuwa wauaji.
 
Back
Top Bottom