Mfahamu Askofu Dr. Josephat Gwajima: Ni zaidi ya Mbunge, ni zaidi ya Waziri...! Ni Mtumishi wa Mungu aliye Hai! Si mtu wa mchezo mchezo!

Mfahamu Askofu Dr. Josephat Gwajima: Ni zaidi ya Mbunge, ni zaidi ya Waziri...! Ni Mtumishi wa Mungu aliye Hai! Si mtu wa mchezo mchezo!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
57,103
Reaction score
128,722
Wanabodi

JF ni ukumbi wa kuhabarishana, kuelimishana, kuburudishana na kusaidiana ikiwemo kuisaidia nchi yetu, taifa letu, viongozi wetu na watu wake.

Kuna watu wengi wanadhani wanamfahamu vizuri Askofu Dr. Josephat Gwajima, kama Askofu tuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, lakini kiukweli wengi hawamfahamu vizuri, Askofu Dr Gwajima, wala hawazijui nguvu zake!, huyu sio mtu wa mchezo mchezo!, sio mtu wa kawaida, huyu Askofu Dr Josephat Gwajima ni zaidi ya Mbunge, ni zaidi ya Waziri, ni zaidi hata ya Rais!.

Msikilize mwenyewe akijieleza
View: https://youtu.be/3uu59k7ExjY?si=aMrkmn76gQH3py4e

Huyu ni Mtumishi wa Bwana Mungu Aliye Hai!.

Nashauri hawa viongozi wa kiroho, wazingatiwe sana, wasipuuzwe!.

Kuna Askofu fulani, alimuamuru kiongozi fulani mkubwa tuu wa kisiasa atubu dhambi zake, na akaonya kuwa Mungu amemwambia, huyo kiongozi asipotubu, Mungu atamnanilii!, huyo kiongozi alipuuzia!, na mwisho wa siku, ni kweli alikuja kunaniliwa! na sasa ni naniliu!.

Kuna kiongozi mwingine alishauriwa na maaskofu kamsamehe kichaa fulani, huyo kiongozi akagoma!,
Hata mimi nikajitolea kumshauri humu Bernard Membe usibishane na Maaskofu, samehe tu. Yule ni kichaa anastahili msamaha, hakujua atendalo akapuuza ushauri huu!

Baada ya kupuuza ushauri huo, zilipita wiki mbili tuu!, yaani baada ya siku 14 jambo likatokea! nami nikaandika tazia Buriani Benard Membe, Umepigana Vita Vilivyo Vitakatifu, Mwendo Umeumaliza, Imani Umeitunza, Madeni Yako Yaliyobakia Karma Itakulipia!

Hivyo nashauri kwa kusisitiza, kama ni kweli Askofu Dr Josephat Gwajima , ni Mtumishi wa kweli wa Bwana Mungu Aliye Hai, kama nilivyo uliza hapa Askofu Gwajima ni Mtumishi wa Mungu wa kweli au? Asema Uongo. Adai yeye ni zaidi ya Rais

Then nashauri Askofu Dr Josephat Gwajima asipuuzwe!, tena azingatiwe kwa makini sana!.

Paskali
 
Naanza kupata wasiwasi hii NRNE haitoki kwa Lissu, yeye ni mbeba ujumbe tu. Ujumbe unatoka juu zaidi. SSH angekuwa na washauri wenye hekima / angewasikiliza wenye hekima basi ingeliponya taifa na kutuepusha na misiba / majanga yanayoepukika.

Mhubiri 7:17 " Lakini pia, usiwe mwovu sana wala usiwe mpumbavu! Ya nini kufa kabla ya wakati wako?"
 
Wanabodi

JF ni ukumbi wa kuhabarishana, kuelimishana, kuburudishana na kusaidiana ikiwemo kuisaidia nchi yetu, taifa letu, viongozi wetu na watu weke.
CCM wameamua kuendesha, (ongoza) nchi kwa mfumo wa unyumbu wa kisiasa

Mfumo wa unyumbu wa kisiasa ni mfumo unao wezesha wanaopewa dhamana kuahirisha kufikiri kwa nafsi kwasababu ya kulitumikia kundi fulani kwa masilahi binafsi kwanjia ya kujipendekeza ama kwa uoga wa kuigiza kwa viongozi wao, (unafiki), a.k.a kujizima data

Kibaya zaidi tunaishi kwenye jamii ya kanyanga twende jamii ambayo unaweza kuisafisha ubongo ikafikiri unavyotaka wewe

Jamii ambayo wengi wao hawawezi kuchakata taarifa chanya na hasi

Human herding in politics is an occurrence of entrusted people suspending their individual reasoning because of working towards group objectives through unbecoming behavior s such as flattering or hypocrisy

Unyumbu, (mawazo ya wanyama yanayo fanana) - similar mind set towards self-absorbed group
 
Back
Top Bottom