Meya wa Kinondoni amkaribisha Benard Membe CHADEMA

TataMadiba

JF-Expert Member
Feb 7, 2014
9,866
5,747
"Meya wa Kinondoni amkaribisha Benard Membe Chadema". Hicho ni kichwa cha habari katika gazeti la Mwananchi ambapo Meya wa Kinondoni, Boniface Jacob amenukuliwa akimshauri aliyekuwa Waziri wa Mambo ya nchi za nje katika awamu ya nne, Benard Membe ahamie UKAWA kwa kile alichokisema hoja alizozitoa Waziri huyo wa Zamani ni za msingi na zilipaswa kutolewa na mpinzani.

Sina haja ya kurudia nini Membea amesema, kama sote tunafuatilia vyombo vya habari ikiwemo mitandao ya kijamii tunajua.

Pamoja na Meya Jacob kuziita hoja za Membe ni za msingi, . Nanukuu "Nadhani hakuwa mtu sahihi kusema hayo, alipaswa kwanza kumtafuta mtu mwingine aseme halafu yeye afuate baadaye, lakini kuanza kusema yeye moja kwa moja wakati alikuwa ananufaika na anachokipinga Rais, anaonekana anamuonea wivu na mgongano wa maslahi. Sasa anapoanza kujibu yeye inashangaza kwa sababu yeye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje, iliyokuwa inafanya matumizi makubwa halafu unakosoa unaonekana kabisa unaonesha kuna mgongano wa maslahi". Mwisho wa kunukuu.

Wanachadema na UKAWA kwa ujumla muulizeni;

1. Mbona anakuwa kigeugeu? Anaziona hoja za Membe za msingi wakati huohuo anasema Membe anamuonea wivu Dr. Magufuli kupiga marufuku safari za nje na kwamba ana mgongano wa kimaslahi kwa sababu yeye alinufaika nazo

2. Kwanini anataka Membe ahamie UKAWA wakati amekiri wazi kuwa alinufaika na safari nje wakati akiwa Waziri wa Nje jambo lililoliingizia taifa hasara kubwa? Au ndo kuwaaminisha Watanzania kuwa ni halali wachafu wote kufuata mkondo wa LOWASSA?
 
"Meya wa Kinondoni amkaribisha Benard Membe Chadema"

Huyu meya ni majanga.Hajui hata kazi ya meya ni nini? Anafikiri ni wenyekiti wa CHADEMA kinondoni!!!!!
Meya ni sawa na kiongozi wa serikali .Ukishachaguliwa ni kazi tu kutumikia wananchi bila kujali chama.Anashusha hadhi ya umeya.

Yeye kama meya ajikite kwenye kuzoa uchafu ulijazana kila kona kinondoni na kuzibua maji machafu na kukarabati mabarabara nk hayo ya chama awaachie viongozi wa CHADEMA wayafanye.

Hakuchaguliwa umeya afanye kazi za chama!!! Asichanganye mambo.Wananchi hawawezi muhoji mafanikio yake kama meya akasema mafanikio yangu kama meya nilimwingiza Membe CHADEMA!!!!!!!!! Meya kama huyu ni jipu la kutumbua na mzigo tu kwa wanakinondoni
 
Ameshindwa kazi kabla ya kuanza. Meya ni wananchi wote sio CDM.
Itakuwa faraja kubwa Membe aondoke ili atumbuliwe kirahisi.
 
Yeye kama meya ajikita kwenye kuzoa uchafu ulijazana kila kona kinondoni na kuzibua maji machafu na kukarabati mabarabara nk hayo ya chama awaachie viongozi wa CHADEMA wayafanye.

Hakuchaguliwa umeya afanye kazi za chama!!! Asichanganye mambo.Wananchi hawawezi muhoji mafanikio yake kama meya akasema mafanikio yangu kama meya nilimwingiza Membe CHADEMA!!!!!!!!! Meya kama huyu ni jipu la kutumbua na mzigo tu kwa wanakinondoni
Unaingilia Uhuru wa MTU, kwani Nape no Mbunge na ni Waziri mbona humshauri asiongee ya CCM na ya Chadema? Yule no Mea was Kinondoni kupitia Chadema sio kutokea chooni kama Slaa alivyo sema, wee uko Chooni ndio maana hujielewi.
 
Personal attack. Inaonekana wewe ulikuwa mmoja ya watu wanaoumendea U meya wa Kinondoni, ila ukaukosa. Sasa umeamua kumletea majungu mwanamume mwenzako! Shameful.
 
Huyu meya ni majanga.Hajui hata kazi ya meya ni nini? Anafikiri ni wenyekiti wa CHADEMA kinondoni!!!!!
Meya ni sawa na kiongozi wa serikali .Ukishachaguliwa ni kazi tu kutumikia wananchi bila kujali chama.Anashusha hadhi ya umeya.
Kuchagua meya ambaye kutwa anaota CHAMA ni hatari.ANYWAY MAJI YAMESHAMWAGIKA .
wewe mwongo uoni waliokuwa nyuma ya Lowasa wanahukumiwa
 
Mimi ni mtiifu sana CDM na nnaipenda milele ila maneno ya Bon ni ya kipuuzi sana, CDM inazidi kushuka hadhi kwakuwa waropokaji.

Binafsi Boni namfaham sana maana nimekuwa nae shule na sio shule tu, tuliishi Boarding school wote. Sijui hata uo umeya walimpaje kati ya madiwani wote tuliokuwa nao
 
Watu hamkusikia Membe alizungumza nini kuhusu wale waliotoka CCM. Ikiwa mlisikia kauli alizotumia kwa watu kama Lowassa, Sumaye, Kingunge, Medeye na wale wote waliotoka CCM na kwenda upinzania.....Hakika msingemkaribisha.

CCM ni chama kinacho toa uhuru kwa wanachama wake kutoa maoni...
ndio maana hata rais Magufuli mwenyewe anasema yale anayo yaamini bila kukwaza chama.....sembuse Membe!?!?!
 
Fis
"Meya wa Kinondoni amkaribisha Benard Membe Chadema". Hicho ni kichwa cha habari katika gazeti la Mwananchi ambapo Meya wa Kinondoni, Boniface Jacob amenukuliwa akimshauri aliyekuwa Waziri wa Mambo ya nchi za nje katika awamu ya nne, Benard Membe ahamie UKAWA kwa kile alichokisema hoja alizozitoa Waziri huyo wa Zamani ni za msingi na zilipaswa kutolewa na mpinzani.

Sina haja ya kurudia nini Membea amesema, kama sote tunafuatilia vyombo vya habari ikiwemo mitandao ya kijamii tunajua.

Pamoja na Meya Jacob kuziita hoja za Membe ni za msingi, . Nanukuu "Nadhani hakuwa mtu sahihi kusema hayo, alipaswa kwanza kumtafuta mtu mwingine aseme halafu yeye afuate baadaye, lakini kuanza kusema yeye moja kwa moja wakati alikuwa ananufaika na anachokipinga Rais, anaonekana anamuonea wivu na mgongano wa maslahi. Sasa anapoanza kujibu yeye inashangaza kwa sababu yeye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje, iliyokuwa inafanya matumizi makubwa halafu unakosoa unaonekana kabisa unaonesha kuna mgongano wa maslahi". Mwisho wa kunukuu.

Wanachadema na UKAWA kwa ujumla muulizeni;

1. Mbona anakuwa kigeugeu? Anaziona hoja za Membe za msingi wakati huohuo anasema Membe anamuonea wivu Dr. Magufuli kupiga marufuku safari za nje na kwamba ana mgongano wa kimaslahi kwa sababu yeye alinufaika nazo

2. Kwanini anataka Membe ahamie UKAWA wakati amekiri wazi kuwa alinufaika na safari nje wakati akiwa Waziri wa Nje jambo lililoliingizia taifa hasara kubwa? Au ndo kuwaaminisha Watanzania kuwa ni halali wachafu wote kufuata mkondo wa LOWASSA?
Fisadi mwingine anaombwa aungane na wenzie. That would be an enormous favour kwa CCM. Mchukuweni tu, tena bila malipo.
 
Tanzania bado sana, maana hata viongozi walioshikilia nafasi nyingi tu ni vilaza. Jamaa alichofanya sio smart kabisa, yeye kaona Membe kaenda against na anachofanya Rais kidogo tu bila hata kupima upepo tayari akarukia yote akidhani cdm itamuangalia, yeyote akiye cdm sasa hivi anayetegemea kupanda top hajisomi, kama walimtosa hadi Dr. Slaa kwa kuwachana ukweli hakuna mtu ambaye cdm haitoweza mgeuka.

Tanzania sasa hivi badala ya kuendeshwa kwa reasoning na kufuata sheria inaongozwa kwa fear na kila mtu anataka headlines kua anafanya kazi, press conference zinaitishwa sana siku hizi. Sehemu Magufuli alikosea ni kuinduce hiki kitabia kilichowapelekea hawa viongozi wote chini yake wajifanye miungu watu wanatoa tu amri bila kufikiria, hata jeshi la polisi inasikitisha kuona wanaamrishwa ovyo tu, ili mradi mtu ana cheo serikalini akisema flani akamatwe they dont question wao wanakamata tu. Nchi imejaa vilaza kila kona na uvunjaji haki, its a shame kwa kweli.
 
Back
Top Bottom