Meya Jerry Silaa kweli hulijui hili....?

Meya Jerry Silaa kweli hulijui hili....?

wananchi wenyewe inabidi tubadilike wewe mimi yule tubadilike jukumu la usafi lianzie home then mtaani kwetu
 
Mkuu wangu chama uko wapi njoo huku utoe ufafanuzi

Mkuu Mungi
Jukumu la kutunza mazingira ni la watu wote anzia nyumbani kwako; toa elimu ya mazingira kwa majirani 10; huu uwe ni mkakati wa kila mtu; Meya peke yake hawezi kulitatua tatizo la uchafu; nyie wenyewe wananchi mnatakiwa mueleimke kwenye hili; vinginevyo mtaishia kutoa lawama ambazo hazina mshiko; yaani wewe mwenyewe unye barabarani halafu unataka jery silaa akazoe mavi yako?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
Mkuu wangu chama uko wapi njoo huku utoe ufafanuzi

Mkuu Mungi
Jukumu la kutunza mazingira ni la watu wote anzia nyumbani kwako; toa elimu ya mazingira kwa majirani 10; huu uwe ni mkakati wa kila mtu; Meya peke yake hawezi kulitatua tatizo la uchafu; nyie wenyewe wananchi mnatakiwa muelemike kwenye hili; vinginevyo mtaishia kutoa lawama ambazo hazina mshiko; yaani wewe mwenyewe unye barabarani halafu unataka Jerry Silaa akazoe mavi yako?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
wewe je.JPG

Mimi bado najiuliza ilitumika Shilingi ngapi kuandaa hili bango, ni kuchezea kodi za wananchi. sababu kama bango linahusu mazingira kwanini wasingeweka picha ya mti, au picha za wale kina mama wasafishaji wa mitaro. kuna uhusiano gani kuweka picha ya Meya kama siyo kujikweza tu .
 
jerry ni wa ilala tu na sio dar nzima msai....kidogo ana vission ukilinganisha na waliobaki

Jerry slaa s doin the best, ilala kuna kampuni ya usafi ina magari ya kisasa kabisa, usafi unafanyika usk...kino na tmk bado wanawatumia mabibi vikongwe kufagia barabara..... Mhulize mzer dr masabuli....
 
Ukweli Dar yote ni chafu sana, nimekaa Moshi na Iringa hii miji ni misafi hata mvua ikinyesha matatizo yake ni kidogo ukilinganisha na Dar. Tatizo viongozi husika hawajui wafanye nini ili kuwashirikisha wananchi, wako bize kukusanya ushuru wa wamachinga, stendi, mabango ya matangazo na kukimbizana na machangudoa.
 
Pamoja na kuwa inaeleweka wazi kuwa Chadema kuna mapimbi wengi ila hizi tuhuma nyingine inabidi mfanye uchunguzi wa kina kabla ya kutapika pumba zenu; JERRY slaa kama meya wa Ilala anajitahidi sana kukabiliana na tatizo la uchafu. Kwenye manispaa yake badala kupoteza muda JF kuandika pumba kama hizi nadhani ingekuwa jambo la busara kutoa changamoto kwa wakazi wa Ilala kuunga mkono juhudi za meya kutatua tatizo la uchafu Ilala.

Chama
Gongo la mboto DSM

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Kuna msemo mmoja ambao tumekuwa tukiutumia kuwa "Mpende adui yako" kumpenda adui yako kunazaa aina mbili za matokeo.
1. Ukimpenda adui utapata kumfahamu sana asili ya nguvu yake hivyo ukaweza kumshinda pindi mkikutana katika mapambano.
2. Ukimpenda adui yako utaweza kuurejesha uhusiano ambao umeharibiwa kipindi chote mlipokuwa katika kumtumikia shetani na mambo yake yote.

Ukimchukia adui matokeo yake ni UADUI ENDELEVU

UCHAFU ni adui yetu na kwa bahati mbaya tumemchukia na kamwe tusidhani kuzoa na kwenda kutupa VINGUNGUTI ni suluhisho la hasha.
Kama ilivyo ada ya dhana ya TUMPENDE ADUI YETU, Uchafu ni adui yetu YATUPASA TUUPENDE ILI TUWEZE KUUONDOA KIRAHISI. Kuziba pua tupitapo majalalani ni suluhisho, tena ni ishara kwamba uchafu umetushinda.
Kuupenda uchafu kutatufanya tusione haya kuuondosha. Tutaweza kukaa nao majumbani mwetu na kuukusanya pamoja tukisubiri magari maalum ya kusomba uchafu kwa ajili ya kumwaga dampo. Tukiuchukia UTABAKI PALE PALE hadi mwisho wa dahari.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom