Mene mene tekeli na pelesi

Shenkalwa

JF-Expert Member
May 3, 2011
580
132
Tawala nyingi zilizoanguka katika dunia hii toka enzi za mababu ziliangushwa baada ya dalili nyingi kujitokeza zikiwa ni pamoja na watawala kutoshaurika, kujiona wao ni miungu zaidi ya Mungu na kuwanyima watu wao yale wanayoyastahili na badala yake watawala kujipenda wenyewe na familia zao, na marafiki zao na jamaa wa koo zao na kuwaacha wengine wakihangaika na maisha.

Zaidi sana kuwanyanyasa kwa kuwabambikia makosa ambayo ni ya kutengenezwa ili mradi tu mkubwa mmoja amemchukia mtu fulani. Haya pamoja na mengine mengi ndiyo yanayotokea katika Tanzania ya leo. utawala uliopo madarakani kwa kupitia ccm hebu someni maneno haya: Mene mene tekeli na pelesi
 
Swadaktaaaaaaaaaa. Mungu ameuhesabu utawala wao umekwisha. Umepimwa kwa mizani nao umepungua kwa sababu wamewatesa watu wa mungu na kuwaongoza ndivyo sivyo. Wameyakumbuka matumbo yao tu. Wamewaibia wajane na wamekula mali za watoto yatima. Elimu na maisha bora ni kwa watu wa nyumbani kwao tu, wananchi wanateseka. Siku zao zinahesabika. Mwisho wao umefika.
 
Tawala nyingi zilizoanguka katika dunia hii toka enzi za mababu ziliangushwa baada ya dalili nyingi kujitokeza zikiwa ni pamoja na watawala kutoshaurika, kujiona wao ni miungu zaidi ya Mungu na kuwanyima watu wao yale wanayoyastahili na badala yake watawala kujipenda wenyewe na familia zao, na marafiki zao na jamaa wa koo zao na kuwaacha wengine wakihangaika na maisha.

Zaidi sana kuwanyanyasa kwa kuwabambikia makosa ambayo ni ya kutengenezwa ili mradi tu mkubwa mmoja amemchukia mtu fulani. Haya pamoja na mengine mengi ndiyo yanayotokea katika Tanzania ya leo. utawala uliopo madarakani kwa kupitia ccm hebu someni maneno haya: Mene mene tekeli na pelesi
Naisoma Tena hii
 
MENE - Mungu ameuhesabu Ufalme wako na kuokomesha.

TEKELI - Umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka.

PERESI - Ufalme wako umegawanyika na wamepewa Wamedi na Waajemi.
 
Hata maneno ya mene mene tekeli na peresi yanawahusu chadema kwenye chaguzi zinazokuja kuwa wajiandae kuondoka
 
Tawala nyingi zilizoanguka katika dunia hii toka enzi za mababu ziliangushwa baada ya dalili nyingi kujitokeza zikiwa ni pamoja na watawala kutoshaurika, kujiona wao ni miungu zaidi ya Mungu na kuwanyima watu wao yale wanayoyastahili na badala yake watawala kujipenda wenyewe na familia zao, na marafiki zao na jamaa wa koo zao na kuwaacha wengine wakihangaika na maisha.

Zaidi sana kuwanyanyasa kwa kuwabambikia makosa ambayo ni ya kutengenezwa ili mradi tu mkubwa mmoja amemchukia mtu fulani. Haya pamoja na mengine mengi ndiyo yanayotokea katika Tanzania ya leo. utawala uliopo madarakani kwa kupitia ccm hebu someni maneno haya: Mene mene tekeli na pelesi....
Sio Pelesi ni Peresi
 
Back
Top Bottom