nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,860
- 5,803
Saturday, 25 May 2013 14:44
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe akifafanua jambo
Dar es Salaam,Tanzania
WAKATI wanasiasa wakipinga hatua ya kuhusika katika vurugu za Mtwara ziliso sababisha vifo vya watu wa wawili na kusababisha uharibifu wa mali, kwa kuijia juu Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kusema kwamba isitafute sababu, bali itafute njia ya kukomesha vurugu na kutatua tatizo la Wana-Mtwara, Wazi wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe naye ameibuka nakudai kuwa ahusiki katika vurugu hizo.
Waziri Membe amevunja ukimya na kudai kwamba tuhuma zinazorushwa kwake na wana CCM wenzake kwamba anahusika katika vurugu hizo si za kweli.
Membe ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku moja tangu tuhuma hizo zilipoanza kusambaa sehemu mbalimbali nchini kwamba anahusika katika vurugu za Mtwara zilizo sababisha Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Anne Makinda asitishe vikao vya Bunge la Bajeti kwa siku mbili.
Akizungumza katika Mahojiano maalum na Habarimpya.com Membe alisema kwamba yeye ahusiki kwa namna yoyote ile na vurugu hizo na kwamba watu walioamua kumhusisha na vurugu hizo wana malengo yao yasiyokuwa na tija.
"Si kweli kabisa kwamba ninahusika kwa namna yoyote ile na vurugu za Mtwara, wanaonihusisha wana malengo yao ya kisiasa ambayo hayana tija kwa maslahi ya nchi yetu pamoja na rasilimali zetu"alisema Waziri Membe. Jana tovuti ya Habarimpya.com katika toleo lake namba 2468 iliyokuwa na kichwa cha habari iliyosomeka kwamba Membe atuhumiwa vurugu za Mtwara ilielezea jinsi ambavyo serikali inawatuhumu wanasiasa kuwa wao ndiyo chanzo cha vurugu hizo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe akifafanua jambo
Dar es Salaam,Tanzania
WAKATI wanasiasa wakipinga hatua ya kuhusika katika vurugu za Mtwara ziliso sababisha vifo vya watu wa wawili na kusababisha uharibifu wa mali, kwa kuijia juu Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kusema kwamba isitafute sababu, bali itafute njia ya kukomesha vurugu na kutatua tatizo la Wana-Mtwara, Wazi wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe naye ameibuka nakudai kuwa ahusiki katika vurugu hizo.
Waziri Membe amevunja ukimya na kudai kwamba tuhuma zinazorushwa kwake na wana CCM wenzake kwamba anahusika katika vurugu hizo si za kweli.
Membe ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku moja tangu tuhuma hizo zilipoanza kusambaa sehemu mbalimbali nchini kwamba anahusika katika vurugu za Mtwara zilizo sababisha Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Anne Makinda asitishe vikao vya Bunge la Bajeti kwa siku mbili.
Akizungumza katika Mahojiano maalum na Habarimpya.com Membe alisema kwamba yeye ahusiki kwa namna yoyote ile na vurugu hizo na kwamba watu walioamua kumhusisha na vurugu hizo wana malengo yao yasiyokuwa na tija.
"Si kweli kabisa kwamba ninahusika kwa namna yoyote ile na vurugu za Mtwara, wanaonihusisha wana malengo yao ya kisiasa ambayo hayana tija kwa maslahi ya nchi yetu pamoja na rasilimali zetu"alisema Waziri Membe. Jana tovuti ya Habarimpya.com katika toleo lake namba 2468 iliyokuwa na kichwa cha habari iliyosomeka kwamba Membe atuhumiwa vurugu za Mtwara ilielezea jinsi ambavyo serikali inawatuhumu wanasiasa kuwa wao ndiyo chanzo cha vurugu hizo.