Membe katika tamasha la Pasaka uwanja wa taifa

Membe katika tamasha la Pasaka uwanja wa taifa

Wamechokwa na wananchi.

ndo kazi waliyobakiwa nayo. Kuhudhuria misiba,harambee na matamasha. Maana shughuli ya kuwaletea wananchi maendeleo imewashinda. Mi naomba tu wananchi waendelee kula hiyo michango yao kwani ni kodi zetu wanazotuibia wanaturudishia
 
aisee nilikuwepo pande zile mh, waziri alikuwa anatoa hotuba ya kisiasa sijui serikali yenu inapunguza uchungu wa maisha, katiba alikuwa anakera sana sijui kwanini nchi yetu wanasiasa wanatukuzwa sana kuliko viongozi wa dini lakini dhambi yao itawatafuna 2015 leo naona atakuwa amejifunza kitu
 
When people they have got no other way to show their dissatisfaction they resort to extreme measures, so long as its non violence I don't see any problem (this so called viongozi they don't listen to reason), therefore may this will grab their attention

Ndugu yangu unawania binti nini? Kizungu chenyewe cha shule ya kata halafu bila aibu unajaribu kujivua nguo hadharani.

Unajua wapagazi wa mafisadi wana hasira kwa sababu walifanya lobbying ili yule aliyeaibishwa Arumeru Mashariki aje kwenye tamasha hili kufanya utakaso akakataliwa. Kwa hasira ndo watu wanakurupuka na kudai kazimewa. Tuliokuwepo uwanjani tunajua kilichotokea na tamasha lilifana sana. Lakini unategemea mtu atapendwa na kila mtu? Assuming alizomewa, kitu ambacho ni uongo, shida iko wapi? Mbona katika utumishi wa umma hilo ni jambo la kawaida sana? Ukweli ni kwamba mafisadi wanaumia sana kuwekwa hadharani.
 
Benard Membe said:
Serikali yenu inasikia kilio chenu na machungu yenu, inachukua hatua za muda wa kati na muda mrefu, baadhi ya matokeo mtayaona karibuni, baadhi yatachukua muda. Hakuna machungu yasiyo na mwisho.
Benard Membe said:
-Tunaelekea kwenye mchakato wa Katiba mpya ambalo ni jaribio lingine. Jaribio ambalo tukifanikiwa kulivuka tutakuwa tumefikia nchi ya ahadi, Tanzania tunayoitarajia.



..jamani huu ni ULAGHAI wa mchana kweupe.

..shame on him kusema uongo wa waziwazi ktk tamasha la kidini.
 
Sio
kweli kwamba Mh. Membe amezomewa leo. Huyo aliyeleta post hii ni MUONGO
MKUBWA. Membe ameshangiliwa saaaana na umati mkubwa uliopo uwanjani.
Namshangaa sana

kwani mkisema ukweli mnakufa? Membe alipoboa watu alizomewa uwanja mzima labda isipokuwa nyi wana usalama mliokuwa mnatukodolea macho watu tuliionekana kama tuna chat na simu! Ujinga wenu kujikomba tu kwa wakubwa!
 
kwani mkisema ukweli mnakufa? Membe alipoboa watu alizomewa uwanja mzima labda isipokuwa nyi wana usalama mliokuwa mnatukodolea macho watu tuliionekana kama tuna chat na simu! Ujinga wenu kujikomba tu kwa wakubwa!

To a hoja na sio kukimbilia kuwa sumu watu wa usalama. Ni wakati gani Membe alizomewa?
 


..jamani huu ni ULAGHAI wa mchana kweupe.

..shame on him kusema uongo wa waziwazi ktk tamasha la kidini.

Inaonekana watoto wa mafisadi mumeumia sana na kitendo cha Membe kuwa mgeni rasmi ktk Tamasha hili. Na bado, mengi yanakuja, subirini, mutaumia zaidi kama hii ndio style yenu.
 
ndo kazi waliyobakiwa nayo. Kuhudhuria misiba,harambee na matamasha. Maana shughuli ya kuwaletea wananchi maendeleo imewashinda. Mi naomba tu wananchi waendelee kula hiyo michango yao kwani ni kodi zetu wanazotuibia wanaturudishia

Hizo nazo ni shughuli za kijamii ambazo zinahitaji kuhudhuliwa na viongozi.
 
To a hoja na sio kukimbilia kuwa sumu watu wa usalama. Ni wakati gani Membe alizomewa?

Mbona ushaambiwa! Unakichwa kizito wewe!
Alipozidisha na kutoa salama za ma askofu alizomewa mara2, alipowaambia watu wasimame kumwombea raisi wa malawi alizomewa na wengine wakasema hatusimami.
Kumbe mnakanushaga ukweliee! Nimejua.
 
Inaonekana
watoto wa mafisadi mumeumia sana na kitendo cha Membe kuwa mgeni rasmi
ktk Tamasha hili. Na bado, mengi yanakuja, subirini, mutaumia zaidi
kama hii ndio style yenu.

Wewe humkui membe nae nifisadi sana!
Nenda boko kwenye national housing zilizojengwa kwa ajili ya wanyo membe nimmoja kati mafisadi waliojiomilikisha nyumba zile, yeye kachukua2 wala hakai kawapangisia watumishi wa vodacom.
 
Wana JF mimi naomba kuuliza, hivi Tamasha hili la Pasaka liliandaliwa na nani? Madhumuni yake yalikuwa ni nini? Mbona sijamsikia mtu yeyote toka ktk Kamati iliyoandaa Tamasha hili akilalamika kwa namna yeyote? Kila mtu aliyehusika ktk Tamasha hili amefurahia sana, hivi haya maneno yanatoka wapi? Huoni kama uharibu shughuli ya wenzio ambayo ilifanikiwa sana? Ni vizuri zaidi mtoa hoja akatueleza ni wakati gani Membe alizomewa? Maana nimepitia video ya tukio zima toka Membe alipoingia uwanjani hadi alipotoka, sijaona hata sehemu moja alipozomewa, zaidi ya kushangiliwa. Kwa mantiki hii, nina wasi wasi na mtoa hoja huenda ana agenda yake ya siri na Mh. Membe. Na wengi wanaomchukia Membe ni MAFISADI au wale wanaomuona kuwa ni tishio ktk medani za kisiasa.
 
Wana JF mimi naomba kuuliza, hivi Tamasha hili la Pasaka liliandaliwa na nani? Madhumuni yake yalikuwa ni nini? Mbona sijamsikia mtu yeyote toka ktk Kamati iliyoandaa Tamasha hili akilalamika kwa namna yeyote? Kila mtu aliyehusika ktk Tamasha hili amefurahia sana, hivi haya maneno yanatoka wapi? Huoni kama uharibu shughuli ya wenzio ambayo ilifanikiwa sana? Ni vizuri zaidi mtoa hoja akatueleza ni wakati gani Membe alizomewa? Maana nimepitia video ya tukio zima toka Membe alipoingia uwanjani hadi alipotoka, sijaona hata sehemu moja alipozomewa, zaidi ya kushangiliwa. Kwa mantiki hii, nina wasi wasi na mtoa hoja huenda ana agenda yake ya siri na Mh. Membe. Na wengi wanaomchukia Membe ni MAFISADI au wale wanaomuona kuwa ni tishio ktk medani za kisiasa.

Kama alishangiliwa basi usishangae hii ya kushangiliwa kwa kuzomewa.........................
 
aisee nilikuwepo pande zile mh, waziri alikuwa anatoa hotuba ya kisiasa sijui serikali yenu inapunguza uchungu wa maisha, katiba alikuwa anakera sana sijui kwanini nchi yetu wanasiasa wanatukuzwa sana kuliko viongozi wa dini lakini dhambi yao itawatafuna 2015 leo naona atakuwa amejifunza kitu

Membe ni Mbunge wa jimbo la Mtama ktk Mkoa wa Lindi, pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Hivi kwa akili zako ulitaka aongee kitu gani zaidi ya siasa? Kazi ya kuhubiri ni ya viongozi wa dini, yeye sio kiongozi wa dini, yeye ni mwanasiasa. Hivi munavyochangia hoja huwa munafikiria kwanza? Naona munajidharaulisha sana. Kwani ukikaa kimya utachekwa? Jitambue, Tafakari...
 
Kama alishangiliwa basi usishangae hii ya kushangiliwa kwa kuzomewa.........................

ok, tuchukulie kwamba alizomewa na hao wasiompenda,, sasa hilo ni jambo la ajabu na la kulileta kujadili hapa? anazomewa Obama na wabaya wake kwanini isiwe Membe kwa wabaya wake. Hata Slaa huzomewa. Wako waliomshangilia Membe, na ni wengi kuliko hao wanaodaiwa kuzomea, ukweli unabaki kuwa huo.
 
Back
Top Bottom