Membe asisitiza kuhusu uraia wa nchi mbili

Membe asisitiza kuhusu uraia wa nchi mbili

Hujaelewa. Kuwapa watu uraia wa nchi mbili kunawafungulia milango huku kwetu ikiwa kule waliko wana uhuru wa kujiedeleza kiuchumi kama raia wa kule, kitu ambacho kwa sasa tunawazuia. Inachotokea ni kwamba kule waliko wanakwamishwa kufanya mambo fulani kama kuwekeza au kumiliki vitu fulani kwa kuwa wao sio raia wa nchi zile, na wao wanaogopa wakichukua uraia wa zile nchi watapoteza uraia wa Tanzania, kulingana na sheria ya uraia ya Tanzania ya sasa.

Tunasema kwamba, kama tukiwaruhusu kuwa raia wa nchi mbili, maendeleo yao ya kiuchumi kule waliko yatakuwa rahisi, kwa kuwa wataruhusiwa kumiliki au kufanya mambo yote ya kukuza uchumi wao waliko wakiwa raia wa nchi hizo. Hiyo ikitokea inakuwa rahisi kwa mapato yao ku-overflow kuja Tanzania ambako wana ndugu, viwanja, na assets nyingine ambazo watakuwa na uwezo wa kuziendeleza.

Mfano, Mtanzania aliyeko Ethiopia haruhusiwi hata kumiliki nyumba kama sio raia wa Ethiopia, hata kama ameoa Mu-Ethiopia. Kwa hiyo ili akue kiuchumi akiwa Ethiopia itabidi aukane uraia wa Tanzania ili achukue wa Ethiopia. Sasa akisha chukua uraia wa Ethiopia na kuwa sio raia wa Tanzania tena, anakosa haki ya mambo mengi tu aliyokuwa nayo Tanzania. Hata kama alikuwa na mashamba au viwanja hapa nyumbani, kisheria mashamba hayo na viwanja sio vyake tena. Akijua hili sio rahisi kwamba ataviendeleza. Sanasana ataishia kuwapa ndugu zake ambao labda kwa sababu za umasikini hawawezi kuviendeleza.

Na pia, ikiwa huyo Mtanzania aliyeko Ethiopia na aliechukua uraia wa Ethiopia anataka kutuma hela Tanzania, serikali ya Ethiopia haitamruhusu kirahisi. Ni sawa na wewe leo jaribu kutuma fedha za kigeni nje ya nchi utaona ilivyo ngumu. Kwanza huruhusiwi kama huna sababu kama kutibiwa, mtoto anasoma sijui nk. Lakini, ikiwa Ethiopia itaruhusu uraia wa nchi mbili, na huyo Mtanzania aliyechukua uraia wa Ethiopia akasema anataka kutuma hela Tanzania ambako kwake ni nyumbani pia, basi kunakuwa na taratibu zinazomruhusu kufanya hivyo. Lakini ikiwa Tanzania ilimnyanganya uraia baada ya yeye kuchukua uraia wa Ethiopia, Ethiopia wanaweza kumkataza kabisa kutuma hela zake Tanzania ambako sio raia tena!

Sasa jaribu kuwaelewesha na wale wengine wote wanaoleta pointi zao za vijiweni hapa kukataa uraia pacha, ooh sijui uzalendo, sijui tukipigana vita watakuwa upande gani!


Mkuu nimekuelewa, maelezo yako yanashawishi lakini uraia pacha unaweza pia kupewa wasio watanzania, ambao watatumia utaratibu huo huo kupata faida za hapana kuzipeleka kwao, kwa mifumo yetu ilvyo na mianya naona itakua hasara zaidi kwetu. Suala hili linahitaji mjadala zaidi. Hatari pia tusizipuuze,kuna uhakika kuwa kwakuwa raia wa Tanzania wataruhusiwa kulieta fedha Tanzania kirahisi zaidi?
 
Marekani inaruhusu dual nationality.

Namuunga mkono Membe kwa hili sababu za kukataa zimekaa kiwivu wivu zaidi.

Mwisho wa siku mtakuja kusema ushoga ruksa, kisa wamarekani wameruhusu jinsia moja kuchimbuana.
 
Mkuu nimekuelewa, maelezo yako yanashawishi lakini uraia pacha unaweza pia kupewa wasio watanzania, ambao watatumia utaratibu huo huo kupata faida za hapana kuzipeleka kwao, kwa mifumo yetu ilvyo na mianya naona itakua hasara zaidi kwetu. Suala hili linahitaji mjadala zaidi. Hatari pia tusizipuuze,kuna uhakika kuwa kwakuwa raia wa Tanzania wataruhusiwa kulieta fedha Tanzania kirahisi zaidi?

Aah, Mkuu, yaani wewe unataka sie tuwe wa kufaidi tu bila kutoa chochote?

Ni kweli unachosema, wapo watakaopata faida na kuzitoa Tanzania, lakini ni wachache sana. Investor wa nje hapa kwetu ni makampuni, na watu binafsi wanaokuja kutafuta fursa za kiuchumi kwamba wataomba uraia pacha ni wachache sana, kwa sababu Tanzania inaonwa nchi masikini. Labda wanaoweza kuomba uraia pacha ni wale waliopewa uraia baada ya kuwa wakimbizi hapa nchini kwa muda mrefu. Na pia kupata uraia lazima uwe umekuwa mkazi wa ile nchi kwa kipindi fulani kirefu tu, sio kwamba mtu anaomba kama vile kuomba kazi.

Na pia jambo la msingi kukumbuka ni kwamba, hata tukikubali kuwa na uraia pacha, sisi wenyewe ndio tutaweka masharti ya nani tutampa uraia wetu. Haina maana tutalegeza masharti ya kuwapa wat uraia wetu kwa sababu tumeruhusu uraia pacha.

Na pia, haitamaanisha tukiruhusu uraia pacha basi tunaondoa masharti yote ya kutoa fedha nje ya Tanzania. Kumbuka kutoa fedha nje ya Tanzania, hata wasio na uraia pacha wanatoa.

 
Kwenye katiba inayopendekezwa yapo baadhi mambo yameshughulikiwa na kumpa fursa raia wa Tanzania aliyechukua uraia wa nchi nyingine kupata upendeleo maalum ikiwa atataka kurudi nyumbani na kutaka kuwekeza au kumiliki nyumba pia ataporudi hatokuwa na ulazima wa kuwa na viza yaani kwa ujumla kero nyingi zilizokuwa zinawasumbua ndugu zetu hawa zimejibiwa japo kuna mengine haikuwezekana mfano fursa ya kupiga kura au kugombea uongozi

Mkuu kwenye katiba kinachopendekezwa ni kwamba utapoteza uraia wa Tanzania, lakini utakuwa prmanent resident wa Tanzania. Sasa haina maana, maana tofauti kati ya permanent resident na raia ni ndogo sana - zaidi ni kwamba huwezi kupiga kura kuchagua viongozi wa nchi, au kugombea nafasi za kisiasa na kuomba baadhi ya kazi. Sioni kwa nini umbane Mtanzania kuwa permanent resident kwenye nchi yake.
 
Aah, Mkuu, yaani wewe unataka sie tuwe wa kufaidi tu bila kutoa chochote?

Ni kweli unachosema, wapo watakaopata faida na kuzitoa Tanzania, lakini ni wachache sana. Investor wa nje hapa kwetu ni makampuni, na watu binafsi wanaokuja kutafuta fursa za kiuchumi kwamba wataomba uraia pacha ni wachache sana, kwa sababu Tanzania inaonwa nchi masikini. Labda wanaoweza kuomba uraia pacha ni wale waliopewa uraia baada ya kuwa wakimbizi hapa nchini kwa muda mrefu. Na pia kupata uraia lazima uwe umekuwa mkazi wa ile nchi kwa kipindi fulani kirefu tu, sio kwamba mtu anaomba kama vile kuomba kazi.

Na pia jambo la msingi kukumbuka ni kwamba, hata tukikubali kuwa na uraia pacha, sisi wenyewe ndio tutaweka masharti ya nani tutampa uraia wetu. Haina maana tutalegeza masharti ya kuwapa wat uraia wetu kwa sababu tumeruhusu uraia pacha.

Na pia, haitamaanisha tukiruhusu uraia pacha basi tunaondoa masharti yote ya kutoa fedha nje ya Tanzania. Kumbuka kutoa fedha nje ya Tanzania, hata wasio na uraia pacha wanatoa.

Mkuu umenena vyema, unajua kuna 'fear of unknown' , kila kitu kipya huwa kinaogopwa elimu inatakiwa, wenye mawazo tofauti wapewe elimu lakini iktengenezwa draft ya sheria hiyo, ingetoa jukwaa zuri la kujadili, nini kiongezwe au kipunguzwe. Hayo masharti ndio haswa yanatakiwa yaangaliwe. kimsingi kwenye uwajibikaji mzuri mambo yatakua shwari ila baadhi ya nafasi ni lazima tuziwekee mashrti isije kutokea kama Peru walikua na raisi ambaye ana uraia wa Japani.
 
stemcell

Namuunga mkono. Sioni hasara walizopata mataifa yaliyokubali uraia wa nchi mbili kwa muda mrefu tu sasa, na wale wote mnaopinga hamtoi mifano halisi ya jinsi nchi hizo zimeingia matatizoni kwa kuruhusu uraia wa nchi mbili, pamoja na nchi jirani kama Kenya na Uganda.

Unajua kila nikisoma sababu za watu wanaopinga uraia pacha nashikwa na hasira unayopata unapomsikiliza mlevi akiongea pumba. Tatizo letu Watanzania tunapenda kubisha bila kuwa na facts, tunaishia ku-speculate tu. Hivi mnafikiri kutorosha mali kwenda nje ya za nchi ni rahisi kiasi hicho, kama watu wanavyofanya madawa ya kulevya?

Mnatoa hadithi za vijiweni huko mnataka ndio uwe msimamo wa serikali. Sijui kukosa uzalendo, sijui tukipigana vita watakuwa upande gani, ooh sijui watatorosha mali na siri za nchi. Hamna lolote la maana mnaongea, pumba tupu kama vile tu ni mjadala unafanyika kwenye shule ya chekechea. au klabu ya ulanzi, kayoga, mbeke, kangara, wanzuki, pyuwa, mataptap, nk. Kama ligi ni kubwa kukuzidi kaa kando acha wenye kelewa mambo waicheze kuliko kuleta hadithi za vijiweni kuhusu uraia pacha.
kwanza Napenda kukutaarifu kukashifu siyo kujenga hoja ,sijasema haina faida bali in hasara yake pia,mfano kuna nchi ambazo hairuhusu kumiliki ardhi mpaka uwe raia na hii Inafungua fursa ya watu wenye asili ya nje kuwekeza pindi watakapo ruhusiwa kuwa na uraia pacha na india ni moja wapo, na sheria ya marekani ya kodi mtu akipata uraia hata kama bado ni mtanzania anatakiwa kulipia income tax hadi kipato chake anachopata Tanzania,hiyo yote ni fursa ya kutoa hela nje ya nchi,raia wengi wasio na asili ya Tanzania itawapa fursa ya kuchukua uraia wa nchi yao ya asili na kubaki Tanzania wakichuma tu,hivi karibuni serikali ya marekani mjini minnesota ilikuwa inalalamikia raia wenye asili ya kisomali wanavyo toa hela kurudisha Somalia bila ya kuwekeza marekani na hii ni baada ya serikali ya Somalia kukubali dual citizenship,lakini Somalia ilifanya hivyo kwa ajili ilikuwa inawahitaji wasomi wao kurudisha lakini hawana mali ya kuporwa kupeleka nje hivyo ni marekani ndiyo inayoumia,sasa sisi wataalamu wetu watarudi na wenye asili ya nje itawapa fursa ya kuwekeza nje.
 
Last edited by a moderator:
stemcell

Namuunga mkono. Sioni hasara walizopata mataifa yaliyokubali uraia wa nchi mbili kwa muda mrefu tu sasa, na wale wote mnaopinga hamtoi mifano halisi ya jinsi nchi hizo zimeingia matatizoni kwa kuruhusu uraia wa nchi mbili, pamoja na nchi jirani kama Kenya na Uganda.

Unajua kila nikisoma sababu za watu wanaopinga uraia pacha nashikwa na hasira unayopata unapomsikiliza mlevi akiongea pumba. Tatizo letu Watanzania tunapenda kubisha bila kuwa na facts, tunaishia ku-speculate tu. Hivi mnafikiri kutorosha mali kwenda nje ya za nchi ni rahisi kiasi hicho, kama watu wanavyofanya madawa ya kulevya?

Mnatoa hadithi za vijiweni huko mnataka ndio uwe msimamo wa serikali. Sijui kukosa uzalendo, sijui tukipigana vita watakuwa upande gani, ooh sijui watatorosha mali na siri za nchi. Hamna lolote la maana mnaongea, pumba tupu kama vile tu ni mjadala unafanyika kwenye shule ya chekechea. au klabu ya ulanzi, kayoga, mbeke, kangara, wanzuki, pyuwa, mataptap, nk. Kama ligi ni kubwa kukuzidi kaa kando acha wenye kelewa mambo waicheze kuliko kuleta hadithi za vijiweni kuhusu uraia pacha.

sababu moja wapo ni ugaidi ya pili ni ushoga watatuambukiza tabia za uko nje
 
Last edited by a moderator:
huyu membe anataka kutuona sisi watanzania mapimbi sana mwambieni hatujasahau machungu ya balali
 
Mkuu nimekuelewa, maelezo yako yanashawishi lakini uraia pacha unaweza pia kupewa wasio watanzania, ambao watatumia utaratibu huo huo kupata faida za hapana kuzipeleka kwao, kwa mifumo yetu ilvyo na mianya naona itakua hasara zaidi kwetu. Suala hili linahitaji mjadala zaidi. Hatari pia tusizipuuze,kuna uhakika kuwa kwakuwa raia wa Tanzania wataruhusiwa kulieta fedha Tanzania kirahisi zaidi?

ndugu yangu unakosea sana sasaivi nchi yetu inatoa uraia kama nyanya mfano angalia wahindi akishakaa miaka kumi anaomba uraia na anapewa wakati huohuo ana uraia wa india hapo mimi ndio napata shida ukitaka kuamini nenda uhamiaji utaona wengi wanao omba uraia ni wahindi.
 
ndugu yangu unakosea sana sasaivi nchi yetu inatoa uraia kama nyanya mfano angalia wahindi akishakaa miaka kumi anaomba uraia na anapewa wakati huohuo ana uraia wa india hapo mimi ndio napata shida ukitaka kuamini nenda uhamiaji utaona wengi wanao omba uraia ni wahindi.
Ni kweli ndugu ndio maana ninaona kuna haja ya kuwa sheria nzuri na kuziba mianya iliyopo hapa kwetu, la kutoa uraia kama nyanya liko wazi wengine wakishapata uraia huo wanasomeshwa na serikali yetu wakihitimu wanarudi kwao kufanya kazi , na wengine huenda kenya, canada na uingereza ndi maeneo yao hayo. NDIO MAANA NASISITIZA KUWA NI LAZIMA SHERIA IKAE VIZURI NA IPATE WASIMAMIZI WAZURI.
 
Hujaelewa. Kuwapa watu uraia wa nchi mbili kunawafungulia milango huku kwetu ikiwa kule waliko wana uhuru wa kujiedeleza kiuchumi kama raia wa kule, kitu ambacho kwa sasa tunawazuia. Inachotokea ni kwamba kule waliko wanakwamishwa kufanya mambo fulani kama kuwekeza au kumiliki vitu fulani kwa kuwa wao sio raia wa nchi zile, na wao wanaogopa wakichukua uraia wa zile nchi watapoteza uraia wa Tanzania, kulingana na sheria ya uraia ya Tanzania ya sasa.

Tunasema kwamba, kama tukiwaruhusu kuwa raia wa nchi mbili, maendeleo yao ya kiuchumi kule waliko yatakuwa rahisi, kwa kuwa wataruhusiwa kumiliki au kufanya mambo yote ya kukuza uchumi wao waliko wakiwa raia wa nchi hizo. Hiyo ikitokea inakuwa rahisi kwa mapato yao ku-overflow kuja Tanzania ambako wana ndugu, viwanja, na assets nyingine ambazo watakuwa na uwezo wa kuziendeleza.

Mfano, Mtanzania aliyeko Ethiopia haruhusiwi hata kumiliki nyumba kama sio raia wa Ethiopia, hata kama ameoa Mu-Ethiopia. Kwa hiyo ili akue kiuchumi akiwa Ethiopia itabidi aukane uraia wa Tanzania ili achukue wa Ethiopia. Sasa akisha chukua uraia wa Ethiopia na kuwa sio raia wa Tanzania tena, anakosa haki ya mambo mengi tu aliyokuwa nayo Tanzania. Hata kama alikuwa na mashamba au viwanja hapa nyumbani, kisheria mashamba hayo na viwanja sio vyake tena. Akijua hili sio rahisi kwamba ataviendeleza. Sanasana ataishia kuwapa ndugu zake ambao labda kwa sababu za umasikini hawawezi kuviendeleza.

Na pia, ikiwa huyo Mtanzania aliyeko Ethiopia na aliechukua uraia wa Ethiopia anataka kutuma hela Tanzania, serikali ya Ethiopia haitamruhusu kirahisi. Ni sawa na wewe leo jaribu kutuma fedha za kigeni nje ya nchi utaona ilivyo ngumu. Kwanza huruhusiwi kama huna sababu kama kutibiwa, mtoto anasoma sijui nk. Lakini, ikiwa Ethiopia itaruhusu uraia wa nchi mbili, na huyo Mtanzania aliyechukua uraia wa Ethiopia akasema anataka kutuma hela Tanzania ambako kwake ni nyumbani pia, basi kunakuwa na taratibu zinazomruhusu kufanya hivyo. Lakini ikiwa Tanzania ilimnyanganya uraia baada ya yeye kuchukua uraia wa Ethiopia, Ethiopia wanaweza kumkataza kabisa kutuma hela zake Tanzania ambako sio raia tena!

Sasa jaribu kuwaelewesha na wale wengine wote wanaoleta pointi zao za vijiweni hapa kukataa uraia pacha, ooh sijui uzalendo, sijui tukipigana vita watakuwa upande gani!




point wewe unayeeleza ya kuwa wateruhusiwa kumiliki ardhi na kuwekeza huko Kisha mali kuna hela zita overflow kuja huku hiyo ni kwa watanzania walioko nje, vipi kwa hawa walioko huku wenye asili ya nje wakichukua uraia wa huko na hela zianze ku overflow opposite side?kama itakuwa rahisi ku overflow kuja huku sidhani itakuwa ngumu kwenda india au Oman nchi ambazo zinawasisitiza wenye asili ya hizo nchi kuchukua uraia.
 
Hujaelewa. Kuwapa watu uraia wa nchi mbili kunawafungulia milango huku kwetu ikiwa kule waliko wana uhuru wa kujiedeleza kiuchumi kama raia wa kule, kitu ambacho kwa sasa tunawazuia. Inachotokea ni kwamba kule waliko wanakwamishwa kufanya mambo fulani kama kuwekeza au kumiliki vitu fulani kwa kuwa wao sio raia wa nchi zile, na wao wanaogopa wakichukua uraia wa zile nchi watapoteza uraia wa Tanzania, kulingana na sheria ya uraia ya Tanzania ya sasa.

Tunasema kwamba, kama tukiwaruhusu kuwa raia wa nchi mbili, maendeleo yao ya kiuchumi kule waliko yatakuwa rahisi, kwa kuwa wataruhusiwa kumiliki au kufanya mambo yote ya kukuza uchumi wao waliko wakiwa raia wa nchi hizo. Hiyo ikitokea inakuwa rahisi kwa mapato yao ku-overflow kuja Tanzania ambako wana ndugu, viwanja, na assets nyingine ambazo watakuwa na uwezo wa kuziendeleza.

Mfano, Mtanzania aliyeko Ethiopia haruhusiwi hata kumiliki nyumba kama sio raia wa Ethiopia, hata kama ameoa Mu-Ethiopia. Kwa hiyo ili akue kiuchumi akiwa Ethiopia itabidi aukane uraia wa Tanzania ili achukue wa Ethiopia. Sasa akisha chukua uraia wa Ethiopia na kuwa sio raia wa Tanzania tena, anakosa haki ya mambo mengi tu aliyokuwa nayo Tanzania. Hata kama alikuwa na mashamba au viwanja hapa nyumbani, kisheria mashamba hayo na viwanja sio vyake tena. Akijua hili sio rahisi kwamba ataviendeleza. Sanasana ataishia kuwapa ndugu zake ambao labda kwa sababu za umasikini hawawezi kuviendeleza.

Na pia, ikiwa huyo Mtanzania aliyeko Ethiopia na aliechukua uraia wa Ethiopia anataka kutuma hela Tanzania, serikali ya Ethiopia haitamruhusu kirahisi. Ni sawa na wewe leo jaribu kutuma fedha za kigeni nje ya nchi utaona ilivyo ngumu. Kwanza huruhusiwi kama huna sababu kama kutibiwa, mtoto anasoma sijui nk. Lakini, ikiwa Ethiopia itaruhusu uraia wa nchi mbili, na huyo Mtanzania aliyechukua uraia wa Ethiopia akasema anataka kutuma hela Tanzania ambako kwake ni nyumbani pia, basi kunakuwa na taratibu zinazomruhusu kufanya hivyo. Lakini ikiwa Tanzania ilimnyanganya uraia baada ya yeye kuchukua uraia wa Ethiopia, Ethiopia wanaweza kumkataza kabisa kutuma hela zake Tanzania ambako sio raia tena!

Sasa jaribu kuwaelewesha na wale wengine wote wanaoleta pointi zao za vijiweni hapa kukataa uraia pacha, ooh sijui uzalendo, sijui tukipigana vita watakuwa upande gani!




point wewe unayeeleza ya kuwa wateruhusiwa kumiliki ardhi na kuwekeza huko Kisha mali kuna hela zita overflow kuja huku hiyo ni kwa watanzania walioko nje, vipi kwa hawa walioko huku wenye asili ya nje wakichukua uraia wa huko na hela zianze ku overflow opposite side?kama itakuwa rahisi ku overflow kuja huku sidhani itakuwa ngumu kwenda india au Oman nchi ambazo zinawasisitiza wenye asili ya hizo nchi kuchukua uraia.usikashifu jibu tu.
 
watakimbia nchi ,tukae humuhumu hadi mchwa wote wafe
 
Mkuu nimekuelewa, maelezo yako yanashawishi lakini uraia pacha unaweza pia kupewa wasio watanzania, ambao watatumia utaratibu huo huo kupata faida za hapana kuzipeleka kwao, kwa mifumo yetu ilvyo na mianya naona itakua hasara zaidi kwetu. Suala hili linahitaji mjadala zaidi. Hatari pia tusizipuuze,kuna uhakika kuwa kwakuwa raia wa Tanzania wataruhusiwa kulieta fedha Tanzania kirahisi zaidi?

Mkuu, hayo ni mambo ya kibisahara huwezi kuyazuia, ila hilo haliwezi kuwa kikwazo cha kuruhusu uraia pacha, kwa sababu unaweza kuweka sheria zinazoweka limit ya capital outflow, au profit repatriation, na kusema kwa mfano, huwezi kutoa nje ya Tanzania faida ya kampuni yako inayozidi 50% ya faida kwa mwaka, cummulatively.

Lakini hata hivyo, kama wasiwasi ni kutoa faida nje, mbona makampuni yanakuja toka nje na kutoa faida yote bila kuwa ni raia pacha? Kwa mfano, miradi ya madini na gesi, wanatoa nje faida karibu yote 100%. Sasa kwa nini suala la faida kutoka nje liwe jambo la kuwabania Watanzania raia wakati tayari tunaruhusu wenye kampuni wasio raia kutoa?
 
point wewe unayeeleza ya kuwa wateruhusiwa kumiliki ardhi na kuwekeza huko Kisha mali kuna hela zita overflow kuja huku hiyo ni kwa watanzania walioko nje, vipi kwa hawa walioko huku wenye asili ya nje wakichukua uraia wa huko na hela zianze ku overflow opposite side?kama itakuwa rahisi ku overflow kuja huku sidhani itakuwa ngumu kwenda india au Oman nchi ambazo zinawasisitiza wenye asili ya hizo nchi kuchukua uraia.usikashifu jibu tu.

Kama nilivyosema kwa Mkuu Stemcell, hilo tayari linafanyika bila hata uraia pacha. Kwani unafikiri haya makampuni ya madini au gas nk hayatoi faida? Yanamilikiwa na nani?

Au hao Wachina mnaosema wanauza hadi mahindi ya kuchoma Kariakoo, unafikiri faida zao hawatoi? Kwani wana uraia pacha? Kwa hiyo tuna watu wasio raia wanatoa faida tayari, na tunakataa watakaokuwa raia wasiingize.

Kwa mantiki hiyo tuko worse off bila uraia pacha kuliko tutakavyokuwa tukiwa na uraia pacha, kwa sababu uraia pacha utafanya angalau kuwepo na faida inayoingia badala ya hali ya sasa ni kwamba faida inatolewa tu na watu wasio raia.

Kwa maneno mengine, tukitumia kutoa fedha kama kigezo cha kuzuia uraia pacha, tunayemkomoa ni atakaekuwa raia wa Tanzania mwenye uraia pacha, maana kwa yule asiye raia tayari tunaruhusu atoe, akija na uwekezaji hata mdogo tu.

Tunazuia uraia pacha bila kujua tunajikomoa wenyewe.
 
kwanza Napenda kukutaarifu kukashifu siyo kujenga hoja ,sijasema haina faida bali in hasara yake pia,mfano kuna nchi ambazo hairuhusu kumiliki ardhi mpaka uwe raia na hii Inafungua fursa ya watu wenye asili ya nje kuwekeza pindi watakapo ruhusiwa kuwa na uraia pacha na india ni moja wapo, na sheria ya marekani ya kodi mtu akipata uraia hata kama bado ni mtanzania anatakiwa kulipia income tax hadi kipato chake anachopata Tanzania,hiyo yote ni fursa ya kutoa hela nje ya nchi,raia wengi wasio na asili ya Tanzania itawapa fursa ya kuchukua uraia wa nchi yao ya asili na kubaki Tanzania wakichuma tu,hivi karibuni serikali ya marekani mjini minnesota ilikuwa inalalamikia raia wenye asili ya kisomali wanavyo toa hela kurudisha Somalia bila ya kuwekeza marekani na hii ni baada ya serikali ya Somalia kukubali dual citizenship,lakini Somalia ilifanya hivyo kwa ajili ilikuwa inawahitaji wasomi wao kurudisha lakini hawana mali ya kuporwa kupeleka nje hivyo ni marekani ndiyo inayoumia,sasa sisi wataalamu wetu watarudi na wenye asili ya nje itawapa fursa ya kuwekeza nje.

Ashkumu si matusi Mkuu, nilitaka tu kusisitiza. Samahani sana. Ukweli ni kwamba hili suala la uraia pacha mie nalielewa kwa undani sana, ndio maana nashangaa sana point zinazotolewa kulipinga kwa sababu si za kweli. Nadhani umeshasoma majibu yangu hapo juu.
 
Mwisho wa siku mtakuja kusema ushoga ruksa, kisa wamarekani wameruhusu jinsia moja kuchimbuana.

Mkuu Mingoi, kwani unaogopa tukiruhusu ushoga? Ina maana huwezi kusema hapana mtu akikuomba?
 
sababu moja wapo ni ugaidi ya pili ni ushoga watatuambukiza tabia za uko nje

Mkuu Kibanga, na wewe swali lile lile kama Mkuu Mingoi; ina maana mashoga wakija wakikuomba lazima useme ndiyo?

Unajua tunapopinga sana ushoga tujiuize pia ni kwa nini tunafanya hivyo. Kwani Tanzania tukisema ni ruksa kula chura ina maana ni lazima kila mtu ale chura? Si ni kwa wale tu wanaopenda kula vyura? Sasa wengine pilipili msiyoila yawawashiani!
 
Back
Top Bottom