Mdee apelekwa Mahakamani chini ya ulinzi mkali

Mdee apelekwa Mahakamani chini ya ulinzi mkali

Abdull Kazi

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2012
Posts
344
Reaction score
306
Mwenyekiti wa Baraza la wanawake Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema,Halima Mdee Muda huu anapelekwa katika mahakama ya hakimu mkazi wa Kinondoni chini ya ulinzi mkali wa Polisi.

Mdee atashitakiwa kwa kufanya maandamano yasiyo na Kibali, shime wapenda mabadiliko mlio karibu mjitokeze kwa ajili ya kumuunga mkono kiongozi huyu katika wakati huu mgumu kwake, kutoka kwa wasiopenda mabadiliko ya Tanzania tuitakayo.

========

Baada ya kukamatwa akifanya maandamano yenye nia kwenda Ikulu kumshinikiza Rais Kikwete kutoipokea Rasimu ya Katiba inayopendekezwa, Mbunge wa Kawe na Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la Chadema (Bawacha), Halima Mdee, anatarajiwa kuripoti leo katika Kituo cha Polisi Oysterbay, jijini Datr es Salaam.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Camillius Wambura, alisema kuwa mbunge huyo ataripoti kituoni hapo ili kufahamu hatua zingine za kisheria zinazoweza kuchukuliwa dhidi yake na wenzake tisa.

"Anatakiwa kuripoti kesho (leo) kutokana na maandamano waliyoyafanya, akisharipoti tarartibu zingine zitajulikana mara tu baaada ya kupokea jalada kutoka kwa Wakili wa Serikali," alisema Wambura.

"Aliaachiwa juzi (Jumamosi) baada ya kutimiza masharti ya dhamana, jalada likishafika itajulikana hatua gani itakayoendelea dhidi ya Mdee," aliongeza.

Wengine waliokamatwa ni Martha Charles, Beauty Mmari, Anna Linjewele, Sofia Phanuel, Remina Peter na Mwanne Kassim. Hata hivyo, siku hiyo jioni kwa dhamana baada ya kutimiza masharti.

NIPASHE ilifanya jitihada za kumatafuta mbunge huyo kupitia simu yake ya mkononi, lakini hakupatikana.

Mdee pamoja na wanachama wengine wa Chadema Oktoba 4 mwaka huu, walikamatwa katika maandamano yaliyokuwa na lengo la kwenda kuonana na Rais Jakaya Kikwete kumshawishi kutoipokea Rasimu ya Katiba inayopendekezwa, ambayo ilipitishwa na Bunge Maalum la Katiba Alhamisi iliyopita.

CHANZO: NIPASHE
 
mwenyekiti wa Baraza la wanawake Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema,Halima Mdee Muda huu anapelekwa katika mahakama ya hakimu mkazi wa Kinondoni chini ya ulinzi mkali wa Polisi

mdee atashitakiwa kwa kufanya maandamano yasiyo na Kibali, shime wapenda mabadiliko mlio karibu mjitokeze kwa ajili ya kumuunga mkono kiongozi huyu katika wakati huu mgumu kwake, kutoka kwa wasiopenda mabadiliko ya Tanzania tuitakayo

What does the law say about demonstration? Definitely CCM/serikali itapigwa chini! Let us wait and see!
 
mwenyekiti wa Baraza la wanawake Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema,Halima Mdee Muda huu anapelekwa katika mahakama ya hakimu mkazi wa Kinondoni chini ya ulinzi mkali wa Polisi

mdee atashitakiwa kwa kufanya maandamano yasiyo na Kibali, shime wapenda mabadiliko mlio karibu mjitokeze kwa ajili ya kumuunga mkono kiongozi huyu katika wakati huu mgumu kwake, kutoka kwa wasiopenda mabadiliko ya Tanzania tuitakayo


Serikai corrupt duniani huangaika sana na watu wadogo wadogo mitaani,hii ni moja wapo.Mafisadi wanaifilisi nchi hawakamatwi/hawashitakiwi/hawafungwi lakini raia wanaotumia haki zao kufikisha ujumbe ndio hubugudhiww/hunyanyaswa/huuwawa(R.I.P Mwangosi) na kufutiliwa mbali na uso wa dunia.
 
Tulishazoea nadhani wabadilishe mbinu tu. Kutubambikia kesi ni kawaida tu, sasa ni zamu ya Mdee kesho tunasubiri mwingine.
 
Polisi wetu wana tabia ya kufanya mambo madogo yaonekane makubwa, na mambo ya maana wanayapuuzia. Ni aibu sana, na dalili mbaya kwa Watawala.

Kosa dogo kama hilo, unashangaa miguvu mingi na ulinzi wa kutisha wakati kesi kubwa kama utoroshaji wa wanyama nje ya nchi Mtuhumiwa anatoroka kilaini, majambazi yanapora mchana kweupe na kuuwa watu na kutoroka kama vile polisi hawapo.

Vv
 
utafiti unaonyesha kwamba hakuna mtu yeyote aliyewahi kufungwa kwa kuandamana , hivyo ni vitisho tu .
 
Polisi wetu wana tabia ya kufanya mambo madogo yaonekane makubwa, na mambo ya maana wanayapuuzia. Ni aibu sana, na dalili mbaya kwa Watawala.

Kosa dogo kama hilo, unashangaa miguvu mingi na ulinzi wa kutisha wakati kesi kubwa kama utoroshaji wa wanyama nje ya nchi Mtuhumiwa anatoroka kilaini, majambazi yanapora mchana kweupe na kuuwa watu na kutoroka kama vile polisi hawapo.

Vv

NAMSHUKURU SANA MUNGU KWA KunIEPUSHA NA KAZI YA POLISI .
 
Hakuna jambo dogo wala kubwa mbona mateja kila siku wanapelewa mahakamani na msiseme kuwa ni uonevu?Haki sawa kwawote imradi tu uwepo wa ukiukwaji wa sheria.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
kazi ya upolisi ni kazi ya kujitoa akili,bora chriss lukosi alijitoa mapema kwenye hii kazi ya kitumwa.
 
Last edited by a moderator:
adhabu ya kuandamana bila kibali ni nini?
_anayeijua hiyo sheria aweke hapa wakuu..
_tangu nimesikia hizi kesi hakuna hata mmoja ameshawahi kwenda jela kwa kosa la kuandama labda hiyo sheria haipo
 
Back
Top Bottom