Mdahalo: Hakuna wakati katika historia ambapo Zanzibar haikuitegemea Bara

Naam!! kumekuwa na ukimya kwa muda kutoka Zanzibar sasa hivi. Ukimya umetokana na kufanikiwa kwa kampeni hii ya Let Zanzibar Go. Tumewapa uhuru na njia zote za kuweza kutoka kwenye Muungano. Hata wanaosema "Muungano haufai" sasa hivi wanaimba "tunataka Muungano wa Mkataba". Ingawa hiili ni absurd sasa hivi hawazungumzi sana kutaka kuvunja Muungano kwa sababu wanajua kwa uhakika mkubwa watapa haki za kujidai na nchi yao lakini watakuwa wamewahukumu watoto wao kwenye maisha ya umaskini. Na kwa vile tayari wana chembe za mgawanyo wanajua kabisa kuwa Zanzibar nje ya Muungano wa aina yoyote haiwezi kufanikiwa. Kupe hawezi kumsusa ng'ombe!
 

Mimi nitaeka suala la nyengeza hapa... Kwanini Tanganyika (Tanesco) haiwakatii umeme Zanzibar?
 

Ndoto za mchana hizo...
 
Ndoto za mchana hizo...
Ndoto ni zipi Mkubwa Takashi!
Hoja zipo hapo jibu hoja, kusema ndoto haitoshi, onyesha wapi ndoto za lunch zilipo.

Narudia, anayetapa tapa ni mznz kwa sasa. Umesikia Mtanganyika akiomba serikali 3 au mkataba wa Vanuata na Yemeni.
Mwanasheria mkuu wa Unguja kagoma, Maalim Kagoma, Seif ndiyo kabisa! yeye amekana hata sera za chama chake anataka EU sasa. Ahmed Rajab hana la kusema bali mkataba, Ally Salehe Kimyaa! Mansour serikali 3. Jusa serikali 3.
Nani amebaki?

Wznz wameulizwa serikali 3 ziweje hawana jibu ila kibwagizo tu, tatu mkataba!
Kwanini hamtaki kuvunja dau!

In short, sasa ZNZ kimyaa! option iliyobaki ni mkataba, nao tunauliza wa nini? Maana huu uliopo ni mkataba.
Mnataka mkataba wa kitu gani msichokisema? Ninyi ni koloni na mnadai uhuru pack and go simple!

LET ZNZ GO!
 
tupe yarehe hasa lini katika historia Zanzibar iliwahi kutegemea tanganyika?

Hesabu ni wazenj wa ngapi wapo bara na wabara wangapi wapo zenji hapo ndio utakapojua kuwa nani anamtegemea mwenzake, ukimaliza kuhesabu rudi tena nikupatie utegemezi mwingine u wapi?

 

Kwanza munge jaribu kuzuwia zile bahasha zenye hela zinazo sambazwa mitaani ... 5,000 tsh ndani ya bahasha kuna maoni yameshaandikwa tayari "mimi napenda Muungano uliopo uendelee kama uliyo, Serikali mbili, ya Jamuhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi"... Sasa kwa taarifa yenu, zile hela watu wanakula , na maaoni yao yatakua kinyume na matakwa yenu.

Tume inasubiriwa ianze kuchukua maoni Mjini Magharib hapo ile "trailer" aliyoonyeshwa SITTA, movie yake ndio itaanza. Simba wa UAMSHO wananoa makali yao.
 

Kimya kina mshindo....LET ZNZ GO!
 
Tunawatakia kheri simba wa UAMSHO na tunawaunga mkono kwa kila hali. Kinachonitatiza ni kuwa Simba wa vita Maalimu Seif Sharif Hamad, Ahmed Rajab, Ali Salehe, Ahmed Rajab, Mansour, Mwanasheria mkuu, Ismaili Jusa wote wamesalim amri, sasa hawa wa UAMSHO wataweza?

Tume ikifika mjini magharibi ambako ni ZNZ zaidi kuliko kwingine watu wasiume maneno, ni kusema Vunja muungano! period.

Nitakushangaa Takashi nikisikia simba wa uamsho wakijiuma uma. Nitashangaa nikisikia tunataka mkataba, au muungano kama ule wa Botswana na Senegal, au Ujerumani na Comoro!
Simba wa Uamsho wakijing'ata tu tutawaomba WZNZ wakae katika majamvi watulie tuli.
 
Shida moja ya Wazanzibar ni watu wabishi . Kama hamtaki Muungano mbona ni kitu rahisi ? Fungasha mizigo yenu wote na muondoke bara mtaona kama kuna mtu atawafuata huko visiwani
 
Mkuu Nonda,
Hatimaye kile anachosema mwanakijiji sasa kipo wazi, ima serikali moja au Let znz go.
Nadhani Nonda ni mpiga debe mkuu wa serikali 3. Huko nyuma wewe na Takashi mlishambulia hoja yangu ya uwepo wa Tanganyika ni maumivu kwa Zanzibar.

Napenda kuwajulisha kuwa wale mnaodhani wanawaonngoza, kumbe wanawadanya na hawajui wasemalo.
Kwa mwaka wa tatu mjadala wetu kuhusu ZNZ ukiwa na washiriki kama Jasusi,JokaKuu na Mkandara kwa uchache tumekuwa tunasema ZNZ na Wznz wanadanganywa, na tumeonekana wachochezi mawakala n.k.

Someni gazeti la Rai mwema toleo la wiki hii na hapa nanukuu kidogo tu kutoka kwa Ahmed Rajabu

''Wakati huohuo sidhani kama hapa tulipofika Wazanzibari wataridhika kuwa na muundo wa Muungano wa Serikali tatu ikiwa muundo huo utapendekezwa kuwa ndio uwe muundo mbadala wa kulifunika kombe na kuunusuru Muungano''

Ahmed Rajab amewakimbia wote kwa hoja yake ile ile aliyokuwa anaipigia debe miaka miwili. Bwana Rajab ambaye ni mkomoro anayeishi Nairobi na Uingereza amekuwa akiwapumbuza wznz kuhusu serikali 3 akishirikiana na Seif Hamad.
Wote kwa pamoja sasa wanakimbilia mkataba na wala hawana wazo la kuvunja muungano tena. Wamesalim amri baada ya kusikia Let znz go na kuwaacha akina Nonda na Takashi wakiwa na hoja za serikali 3.

Ahmed na Seif wamesoma maoni ya Watanganyika waliosema hakuna faida na Znz twaende zao.
Tumesema na binafsi nimeandika katika uzi huu na kule duru za siasa ya kuwa kitendo cha znz kuitaka Tanganyika irudi ni kujichimbia kaburi.

Tanganyika itakuwa na utaratibu wake na wala haitaweka nafasi ya wznz kutumia mianya ya muungano kunufaika. Tanganyika itasema ZNZ ni mzazi mwenzangu, tukae na tuongee tunamlea vipi mtoto muungano.
Kila nchi na hadhi yake. Seif na Ahmed ambao wantusoma wamebaini kuwa huko wanakowapeleka wznz ni kaburini na azma yao ya utegemezi haitakuwepo.

Sasa wamekimbilia mkataba. Tutawafuata huko huko na kuwauliza mkataba wa nini.
Znz ina bendera wimbo wa taifa,Rais bunge na sasa wanataka kiti UN. Swali wanataka mkataba wa kitu gani wasichokisema?

Hapo pia Ahmed Rajab anawaingiza mkenge maana kila mznz anaimba mkataba! mkataba! mkataba.
Muulize wa nini hakuna anayejibu au ajuaye una husu nini.
Tatizo la wznz ni kufuata mkumbo na jazba ndio maana Ahmed na Maalim Seif wanachezea akili zao kama kindergaten!

Sasa nielezeni enyi wana wa nchi ya ahadi;
Seif Sharif Hamad na Ahmed Rajab wamekana serikali 3. Ninyi mna hoja gani tofauti baada ya wakubwa kusalim amri.
Je mada hii isemayeo ZNZ ni tegemezi itake isitake ni uongo?

Ahmed na kundi lake la wana wa usultani linakana mchana kweupe! Hii ni aibu na dhalili kwa vichwa vya kizanzibar, kwamba watu milioni 1.2 wamemkabidhi Ahmed akili zao. Leo anasema serikali 3 wznz wote wanaimba, kesho anasema mkataba wznz wote wanajiunga na kwaya, keshokutwa atasema serikali 5 kama kawaida wznz hawana tafakuri wataimba tu utake usitake

Nasema kawakana vizuri sana na Kasalimu amri! mwenye hoja aje hapa Tusemezane, lakini kwanza ajue kuwa Ahmed amesalim amri na hataki tena serikali 3.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…