Mchungaji Msigwa; the best risk decision maker ever! Tumpongeze

!
!
Kwa Hiyo Mbunge Bosi Wake Ni Rais Na Sio Wananchi Waliomchagua?
Aiseee! Dunia Simama Nishuke.
Mbona Moshi wabunge wao waliijenga na tulisifia, leo kujengeka Iringa imekuwa kero

Huwa nacheka Sana sana hasa waliozaliwa kaskazini kama mimi ingawa sio kwetu na Wale wenye miji yao kaskazini huwa hawapendi kusikia mara Dodoma jiji au Mbeya jiji? Ingetangazwa moshi jiji pasingekalika kwa sifa

Naona unasubiri aseme moshi jiji ili useme Raisi ndie Bosi
 
Iringa imeendelea but all thanks to Kikwete
Mkuu hongera sana umenielewa vizuri niliposema kama Iringa ilipangwa kuendelezwa au ni kwa bahati mbaya imetokea sifa ni kwa msigwa, Ingawa miundombinu ilianza kujengwa enzi za JK sifa zinaenda kwa aliyemalizia
 
Mimi sioni ujinga wa mtoa mada, sioni ujinga wa Mhe. Msigwa kama mwakilishi wa watu wa jiji la Iringa. Tofauti ya upinzani na Rais Dr. John Joseph Pombe Magufuli ni moja tu; kubinya uhuru wa watu na hasa vyama vya upinzani. Kwa kilichokuwa kinajadiliwa Iringa, Mchungaji Mhe. Peter Msingwa angeonekana kituko kama angesema kinyume na alichokisema. Mchungugaji ni mtu wa Mungu na kwa hilo la kumsifu Mhe. Magufuli ulikuwa ni upatanishi, dhamira ya kujenga madaraja na sio kuta. Ni ustaarabu wa hali ya juu. Mlitaka asemeje? Na kwa taarifa yako, wanaoleta matatizo kwa nchi hii ni wale wasiojulikana, ambao kwa kiwango kikubwa hawatumwi na mfumo rasmi wa serikali. Hao ndio tunatakiwa kujihadhari nao. Hilo amelifanya vizuri Mchungaji.

Ninamshauri jambo moja Mchungaji Peter Msigwa, aimarishe chama cha CHADEMA katika eneo lake la kazi na mkoa wa Iringa kwa ujumla. Mchungaji anatuhumiwa kujenga kuta kwa wapinzani wake ndani ya chama cha chadema. Kila mwenye maoni tofauti anasema ametumwa, amenunuliwa na CCM. Ameongeza mpasuko ndani ya chama. Hilo ndilo hatari zaidi kwa ustawi wa CHADEMA kuliko kumsifu Rais kwa mazuri yanayoonekana.

Kumkashifu hadharani au kutoa lugha za kejeli kwa kiongozi mkuu wa nchi, ni laana na ni ushenzi. Mchungaji anayo "forum inayokubalika kisheria" ya kuelezea mapungufu ya serikali na hata mapungufu ya kiongozi mkuu wa serikali; bungeni na kwenye mikutano yake ya hadhara. Lakini hata katika mikutano hiyo hawezi kupinga kila kitu mwanzo mwisho.

Nitoe wito kwa wanamageuzi wa nchi hii hasa vijana na viogozi wa vyama hivi; tukiwa na chuki dhidi ya watawala tutakwama zaidi. Tuwakosoe bila kuwatukana, tuwasifu wanapostahili na tuwaonyeshe njia iliyobora ya kuongoza nchi. Tuwafundishe namna ya kuwa na mijadala yenye tija.
 
Mchungaji Msigwa kaongea kiujanja sana . But he hasn’t conceded anything. BAHATI mbaya wengi hawakumuelewa
Nakubalina na wewe asilimia 100%. Msigwa amepiga madongo ya kufa mtu, lakini wengi akiwemo aliyepigwa madongo hawakuelewa!
 
Mimi sioni ujinga wa mtoa mada, sioni ujinga wa Mhe. Msigwa kama mwakilishi wa watu wa jiji la Iringa. Tofauti ya upinzani na Rais Dr. John Joseph Pombe Magufuli ni moja tu; kubinya uhuru wa watu na hasa vyama vya upinzani. Kwa kilichokuwa kinajadiliwa Iringa, Mchungaji Mhe. Peter Msingwa angeonekana kituko kama angesema kinyume na alichokisema. Mchungugaji ni mtu wa Mungu na kwa hilo la kumsifu Mhe. Magufuli ulikuwa ni upatanishi, dhamira ya kujenga madaraja na sio kuta. Ni ustaarabu wa hali ya juu. Mlitaka asemeje? Na kwa taarifa yako, wanaoleta matatizo kwa nchi hii ni wale wasiojulikana, ambao kwa kiwango kikubwa hawatumwi na mfumo rasmi wa serikali. Hao ndio tunatakiwa kujihadhari nao. Hilo amelifanya vizuri Mchungaji.

Ninamshauri jambo moja Mchungaji Peter Msigwa, aimarishe chama cha CHADEMA katika eneo lake la kazi na mkoa wa Iringa kwa ujumla. Mchungaji anatuhumiwa kujenga kuta kwa wapinzani wake ndani ya chama cha chadema. Kila mwenye maoni tofauti anasema ametumwa, amenunuliwa na CCM. Ameongeza mpasuko ndani ya chama. Hilo ndilo hatari zaidi kwa ustawi wa CHADEMA kuliko kumsifu Rais kwa mazuri yanayoonekana.

Kumkashifu hadharani au kutoa lugha za kejeli kwa kiongozi mkuu wa nchi, ni laana na ni ushenzi. Mchungaji anayo "forum inayokubalika kisheria" ya kuelezea mapungufu ya serikali na hata mapungufu ya kiongozi mkuu wa serikali; bungeni na kwenye mikutano yake ya hadhara. Lakini hata katika mikutano hiyo hawezi kupinga kila kitu mwanzo mwisho.

Nitoe wito kwa wanamageuzi wa nchi hii hasa vijana na viogozi wa vyama hivi; tukiwa na chuki dhidi ya watawala tutakwama zaidi. Tuwakosoe bila kuwatukana, tuwasifu wanapostahili na tuwaonyeshe njia iliyobora ya kuongoza nchi. Tuwafundishe namna ya kuwa na mijadala yenye tija.
Msigwa ametumia akili kubwa sana kumkosoa mkuu!
 
Nakubaliana na wewe sana. Wanatupigania/wanapigania haki sana. Hili kateleza na kuna mahali nimesema kuwa mimi namuamini sana tena sana Msigwa, kwa hili kateleza kidog. Hatuwezi kumhukumu kwa hili dogo, ila kusema ni lazima lisirudiwe tena!
Hajateleza hata kidogo ametenda lililosawa. Ulitaka aseme nini? Wewe ungepewa nafasi ungethubutu kuyasema unayotaka Mchunga Mhe. Peter Msingwa ayaseme? Haya unayoyasema sasa ni kwa sababu uko peke yako na simu au komputa yako chumbani kwako na kutumia kivuli cha " retired" badala ya jina lako halisi. Achana na Mchungaji kwa hili.
 
Rubbish! Msingi usiokuwa na kujali maisha ya watu ni wendawaqzimu.....wakati Ben saanane amepotea, Azory, Mawazo, etc.....
Ebbo, hivi wewe hukumsikia Mbowe akisema kuwa lazima watanzania 100 wafe ili Chadema iingie madarakani? Pengine ndio hao japokuwa idadi yake haijafikia hao watanzania 100 aliopendekeza Mbowe.
 
..Magufuli alisema Msigwa hafai, wapiga kura wa Iringa Mjini wamefanya makosa kumchagua.

..lakini kwasababu Msigwa ni muungwana, alipopewa nafasi ya kuzungumza hakumkejeli wala kumbeza Magufuli, badala yake alisifia utendaji wa Magufuli.

..sasa kwa busara za kawaida kabisa ungetegemea hotuba ya Msigwa ingefungua ukurasa mpya wa siasa za tija zisizo na vijembe au kashfa.

..lakini cha kusikitisha ni kwamba Magufuli amerudia michezo yake mibaya dhidi ya wapinzani, ambapo leo umepita jimboni kwa mbunge wa chadema na kurudia hujuma zilezile alizomfanyia Msigwa, kwa kudai kuwa wapiga kura wamekosea kumchagua mbunge wa chadema.

..sasa hebu tujiulize, Je ikiwa mbunge wa chadema atasimama ktk mkutano uliohudhuriwa na Raisi na kuwaambia wapiga kura kwamba wamekosea kumchagua Magufuli walipaswa kumchagua Lowassa nini kitamtokea mbunge huyo?

..Kwanini Raisi anatumia mikutano ya hadhara na ziara za KISEREKELI kuwakebehi, na kuwapiga vijembe wapinzani? Kwanini asisubiri kufanya hayo wakati wa ziara za kichama?

..Au kwanini vyama vya upinzani vinanyimwa fursa ya kuzungumza na wananchi na kuelezea upande wao wa shilingi?

..Kwa maoni mpasuko wa kisiasa umesababishwa na UBINAFSI na DOUBLE STANDARD ya mtu mmoja. Watanzania walikosea kumpa kura.
 
Mkuu hongera sana umenielewa vizuri niliposema kama Iringa ilipangwa kuendelezwa au ni kwa bahati mbaya imetokea sifa ni kwa msigwa, Ingawa miundombinu ilianza kujengwa enzi za JK sifa zinaenda kwa aliyemalizia
JK ndio aliipenda Iringa...
 
Mchungaji Msigwa kaongea kiujanja sana . But he hasn’t conceded anything. BAHATI mbaya wengi hawakumuelewa
Mnachonifurahisha bavicha ni kupenda kujifanya watafsiri yaliyomoyoni mwa wale mnaowapenda pale wanapokosea.
 
Ningekuwa kiongozi wa chadema ningefanya kama alivyofanya Mh.Msigwa.
Kuna watu wengi sana wangependa Rais asemwe vibaya na wapinzani,ijapo wao ni ccm damu!Na wengi ni wanafiki sana.Hakuna sababu ya kuumia kwa ajili ya watu wanafiki!Siku ukiumia,watakuwa wa kwanza kukuzodoa.Natamani Lema,Mbowe na hata Tundu Lissu,wamuunge mkono Rais hadharani,wanaoumia kwa hilo wengi ni ccm!Baadhi nawafahamu sana!Kwa siri wanashabikia sana wanaomkosoa Rais,lakini wakisimama kwenye majukwaa,wanawaponda sana wapinzani.
 
Tatizo lako hujafika Iringa ya sasa, Iringa hasa manispaa ya Msigwa huduma muhimu serikali imezifanya kwa 100 percent, kuanzia maji, umeme, Afya na barabara

Huwezi linganisha Iringa na mikoa mingi sana, Tuliofika mikoa mingi ina shida Sana ya umeme na maji lakini sio Iringa

Rubbish ni kuendekeza Uchadema na Uccm kwenye mambo ya msingi
Kiukweli mkuu nakuunga mkono...bahati nzuri nimebahatika kufika mikoa mingi ila kwenye suala la infrastructures Iringa ipo vizuri huwezi fananisha na sehemu kama Lindi au singida kwa Nchemba....sehemu kama Miyomboni pamepangika vizuri sana
 
Nilijua atakuwa mpole maana JPM anajua pesa ya jimbo mil 50 zimeshatolewa kwa wabunge na angeweza kumchallenge kama alivyofanya kwa yule wa kilolo.wapo Karibu na chanzo cha maji halafu JPM akakadiria sh 5 mil zingetosha kufunga water pump na kuyaleta kijijini.
Kwa kifupi ,Nae msigwa ameogopa ku challengiwa na JPM kuhusu pesa ya jimbo.Pesa ambazo kwa wabunge wao ni siri sana ila JPM huwaumbua kama wamepewa na wananchi wajue kuwa pesa ya maendeleo ya jimbo anayo mbunge wao.
acha ujinga dogo pesa ya mfuko wa jimbo inapitia kwa mkurugenzi, mbunge anaiclaim kupitia kwenye vikao vya madiwani.
 
Kwa alivyoongea msigwa hakuna haja kabisa kwa wana iringa kuchagua upinzani. Nawaza kwanini hajahamia chama tawala huyu mchungaji mkataa pema...
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom