Mchungaji Maboya: Mungu haweki agano na maskini

Mchungaji Maboya: Mungu haweki agano na maskini

Ingekuwa kweli basi Yesu Kristo nayeye angezaliwa kwa wazazi matajiri, labda hata kwenye ukoo wa kifalme... imekuwaje sasa akazaliwa na Bikira Maria ambaye alikuwa kachumbiwa na Joseph Seremala??
Kwasbb adamu aliuza kila kitu kwa shetani!
Ndo maana ht Yesu alipojaribiwa hakubisha alikuwa mpole!
Mpk alipoenda msalabani,ili turudishiwe lilichokua kimepotea
 
Wakristo tuwe makini, Shetani baada ya kuona Mwanadamu amevunja amri zote 10 za Mungu hivyo sasa hivi ameanza kushughulika na Biblia Takatifu na kudai maneno yote ni uongo na shetani ameinua watu wanafanyakazi hiyo kwa gharama kubwa .Biblia imempa heshima maskini kwa kiwango cha juu hata Yesu Kristo amezaliwa katika hali ya umaskini wakati yeye ni Bwana wa vyote.Huyo Maboya amepotosha andiko na nia yake nikutaka kutapeli matajiri.Ingawa KiBiblia kuwa tajiri sio dhambi bali utumie utajiri kwa utukufu wa Mungu.
 
Ni rahisi zaidi ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.
@ Kawagawie maskini mali zote kisha unifuate.
@ mwanamke huyu maskini na mjane ametoa zaidi kuliko wote maana ametoa vyote alivyonavyo lakini wengine walitoa ziada ya mali zao.
Heri waliomaskini wa roho maana.....
Hiyo ni mistari michache inayoonesha jinsi Mungu anavyothamini maskini
Je,kuna mistari yoyote Inayosimamia hayo mafundisho ya huyo nabii??
Kumb 8:18
 
Ingekuwa kweli basi Yesu Kristo nayeye angezaliwa kwa wazazi matajiri, labda hata kwenye ukoo wa kifalme... imekuwaje sasa akazaliwa na Bikira Maria ambaye alikuwa kachumbiwa na Joseph Seremala??
Usichanganye mambo, huo mfano ni kigezo tosha cha kuonesha kwamba Mungu anaweza kukuinua ukawa juu bila kujali historia yako na ukawa mfano na akafanya agano na wewe
 
Ingekuwa kweli basi Yesu Kristo nayeye angezaliwa kwa wazazi matajiri, labda hata kwenye ukoo wa kifalme... imekuwaje sasa akazaliwa na Bikira Maria ambaye alikuwa kachumbiwa na Joseph Seremala??
Kwa habari ya ukoo wa Yesu, ametoka kwenye ukoo wa kifalme(mfalme Daudi)
 
Kwa habari ya ukoo wa Yesu, ametoka kwenye ukoo wa kifalme(mfalme Daudi)
Kwel lakin, mfano aliotoa hapana, maana huo mfano unadhihirisha uwezo wa Mungu...anaweza kumnyanyua yeyote
 
KUHUSU huyo maboya, anawapeleka maboya Kama lilivyo jina lake, Mungu aliweka agano na Musa akiwa hana chochote anachunga mifugo ya mkwe wake Yethro, Mungu aliweka agano na Yakobo akiwa porini hajui hata ale nini, maana alikuwa katika mfulio mkali
 
Ni rahisi zaidi ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.
@ Kawagawie maskini mali zote kisha unifuate.
@ mwanamke huyu maskini na mjane ametoa zaidi kuliko wote maana ametoa vyote alivyonavyo lakini wengine walitoa ziada ya mali zao.
Heri waliomaskini wa roho maana.....
Hiyo ni mistari michache inayoonesha jinsi Mungu anavyothamini maskini
Je,kuna mistari yoyote Inayosimamia hayo mafundisho ya huyo nabii??
Mtumishi ukiendelea na hicho unachofikiri utapotea biblia inatwambia ni lazima tuache urithi kwa watoto wetu maana ya mali sio jina la ukoo nenda kasome (mithali 13:22)

Pia mkristo kuwa tajiri ni wajibu kasome (2 wakorintho 8:9)
Pia ukisoma (mwanzo 1 : 22) Mwanzo 1:22
[22]Mungu akavibarikia, akisema, Zaeni, mkaongezeke, mkayajaze maji ya baharini, ndege na wazidi katika nchi.
And God blessed them, saying, Be fruitful, and multiply, and fill the waters in the seas, and let fowl multiply in the earth.
Mungu hakumaanisha kuzaa watoto pekeake (Be fruitful and multiply) maana yake anakazia production ya mali

Ni kweli Mungu haweki agano na masikini kasome (kumb 8:18)
 
Back
Top Bottom