Andrew john
Senior Member
- Mar 10, 2009
- 110
- 122
kwa vile amekuwa muwazi, na umesema ni mcha Mungu we muoe tu, ila jipe muda kwanza ili umfahamu zaidi usifanye haraka, wanawake tuna siri nyingi mno tungekuwa tunaziweka wazi hakuna ambae angeolewa hata mmoja, wapo waliotoa mimba zaidi ya kumi lakini kwa sasa ni wife materials, wapo waliokuwa machangudoa lakin kwa sasa wametulia na familia zao!, wapo yaani wengine hawaelezeki lakin kwa sasa ni mama bora kwa familia zao!! nadhani hata wewe una mabaya yako ya nyuma huko lakin kwa vile mnaanza moja hamtakiwi kuangalia ya nyuma,
thank u kakaThat is good advive. Ushauri mzuri sana
Kifupi kulingana na umriwake..nadhani huyo nimwazi.wengi hawawezi kuweka wazi hayo.wakatimwingine mambo hayo wanafanyiwa bila hiali kutokana na mazingira tata.hasa pale anapotokea kuwa hamjui mzazi mwingine..maanayake kwao ni shida kidogo.ilapia nimuhimu kumuuliza zaidi imeshiriki kinyume namaumbile marangapi...hii nikwasababu asijekuwa addicted...na aliacha mdagani.ili u measure vizr how to control her.but nivizuri usimuache.pia toa msimamo unao onyesha kukemea sana hilo.pia mchunguze vzr kama haja athirika kimaumbile,kwanini nasema hivyo!!labda kaona kuna jambo hutendeka bila kificho kutokana na kuingiliwa kinyume.nakama utagundua lipo..tibakwanza ilibaadae lisije kuwa kigezo cha kumnyanyasa.hongera kwahiloHeri ya mwaka mpya wana Jf wote..!
Nalileta kwenu hili nikiamini humu kuna watu wazima wenye kuweza kunishauri katika hili.
Ila kwa wale wadogo zangu ambao bado mko masomoni naomba muwaachie wakubwa wetu wanishauri na sio kuleta utani,matusi na kejeli.
Ni muda sasa nlikuwa natafuta mchumba ambaye badae aje kuwa mke, nilileta uzi humu lakini pia niliwashirikisha watu wa karibu ikiwemo viongozi wa kiroho na nilifikia uamzi huo baada ya kuona muda wangu wa kuoa umefika pia nlishachoka na maisha ya kihuni
Wengi niliokutana nao sikuvutiwa na tabia zao.
Lakini kuna binti nimempata ambaye kweli ana sifa zote nilizotaka.
Ni mcha Mungu,ana heshima kwangu na kwa jamii inayomzunguka pia anaonekana muwazi kwangu.
Nilimfahamu kupitia mama mmoja wanasali kanisa moja
Baada ya mazungumzo marefu nlimueleza nia yangu ya kumwoa akanielewa ila akaomba tusifanye sex mpaka ndoa nilipomuuliza kwa nini akasema alikuwa na mchumba ambaye alimfanya ayachukie mapenzi baada ya kumtenda.
Nilimwomba anieleze kwa kirefu akasema yeye ni mtoto wa kwanza kwa kati ya watoto watano ambapo mama yao amezaa kila mtoto na babake!
Hamjui babake na alipomaliza elimu ya msingi mama hakuwa na uwezo wa kumsomesha hivyo alipelekwa Dar kufanya kazi za ndani kwa mama mmoja ambapo amedumu mwaka 1.
kisha manyanyaso yalipozidi akapata kazi sehemu nyingine ambapo alikuwa analipwa pesa nzuri na kumtumia mamake kijijini lakn badae mtoto wa kiume wa bosi wake akamrubuni mpaka kumtoa bikra na kuanza mahusiano ambayo yalidumu kwa kificho na kijana alikuwa akimsaidia binti kwa mambo mengi lakn tatizo alianza kumlazimisha kufanya mapenzi kinyume na maumbile ambapo alishindwa kumkatalia kwani hakujua kama kuna madhara pia aliogopa kupoteza ajira.
Anadai alikuwa anasikia maumivu ila alivumilia na kijana alimwahidi kumwoa lakini baada ya mwaka mmoja kijana alileta msichana mwingine na kumtambulisha kwa wazazi mbele ya huyu binti.
Kitendo kilimuuma sana ndipo aliamua kuacha kazi na kurudi kijijini kwa mamake.
Ukweli anaonekana ana nia ya kuolewa ila kinachonipa hofu ni hili la mapenzi kinyume na maumbile.
Je nikimwoa na mimi sifanyi uchafu huo ataweza kuacha kabisa?
Japo yeye anaahidi hatoweza kurudia na hapendi.
Je ni kweli inawezekana mtu aliyepitia mchezo huo akaacha?
Nawaza pia nisimwoe lakini yeye amekuwa mkweli kunipa historia yake kwa kuamini ntamwoa.
Wangapi wanawaficha wachumba wao historia zao za kimapenzi mpaka wanaolewa?
Kifupi binti huyu ni tofauti kabisa na wengine niliowahi kuwapata ambao wengi wao waliweka pesa mbele na uongo mwingi!
Huyu binti ni mdogo miaka 19 na jana nliamua kumpeleka hospital afanyiwe vipimo vyote vya zinaa na H.I.V.
Majibu yalionesha hana tatizo lolote ila sasa tatizo linaloniumiza kichwa ni hilo tu.!
Ikiwa ntamwoa nfanyeje asije kuniletea matatizo mbeleni?
Au nimwache?
Pia nikimwacha ntamwaminije mwingine kuwa hajafanyiwa mchezo huo maana wengi sio wakweli.
Mbarikiwe sana.!!!
Neno muhimu sana hiliUsimuoe MTU kwa kumuonea huruma..
Inataka moyo sana na upendo wa kipekee, ni vema binti huyo aibu angeificha maana ni maumivu kwa mwanaume.Usimuache kaka ushauri wangu mpelek hospital akafanyiwe uchunguz kam hajaaribiwa huko nyum ila muoe uwezi kujua atakufaa nini katik safar yako ya maish Mungu akubarik
Ninashangaa sana, hata kuleta uzi huu jamaa hajishtukii.Kweli dunia inaelekea ukingoni. Yaani binti mwenye sifa hizo halafu waja kutuuliza? Bora asingekwambia.
ashasema aliumia na hapendi..sidhan kama kuna ukweli mwingine unauitaji hapo, puunguza wasiwasi take risks, no one is perfect at list huyo umepata wazo la kumuoa na umeona ni mkweli. watu hubadilika na kukua, so enjoy the present while it last. yakitokeza ya sintofaham huko mbele utapata busara za kukabiliana nazo.Sawa mkuu lakini hawa huwa wanaacha jumla kweli huo mchezo?