Nchaby
JF-Expert Member
- Aug 12, 2013
- 797
- 259
Habari zenu wana jamvi.
Nakumbuka ilikuwa Juni 2012, nilipokutana na dada huyu aitwaye Apaikunda.
Kama ilivyo kawaida ya wanaume, siku hiyo nikamwomba namba yake ya simu, hakusita, akanipatia. Tulikuwa tukiongea kwenye simu mara kwa mara na kutumiana sms mara nyingi.
Siku moja wikendi nikamtafuta, hakusita kama ilivyokuwa mwanzo. Tukakutana sehemu moja ya wazi kwa minajiri ya kutaka kufahamiana zaidi.
Maongezi yetu ya kwanza yalichukua kama masaa matatu hivi na ndio yaliyopelekea kumfahamu dada huyo kuwa anaitwa Apaikunda na ni mwajiriwa wa kampuni moja hapa Jijini.
Ndani ya masaa hayo matatu nilimtolea yangu yote ya moyoni. Jibu lake lilikuwa "kaka nina mchumba wangu nimpendaye sana na tayari tumeshatambulishana kwa wazazi".
Kila nilipojaribu kumwonyesha nia yangu ya dhati, kwamba lengo na madhumuni yangu siyo kumpotezea muda, bali kwa uhakika ni kumtaka awe wangu wa kufa na kuzikana.
Jibu lake lilikuwa moja tu "pole kaka, ulishachelewa na sina namna yoyote ile ya kufanya kwani niliyenaye ananitosha na nampenda mno na siwezi kumwacha wala kumsariti".
Kiukweli huyo Apaikunda ana sifa zote za kuitwa dada mrembo. Ana kila kitu ambacho mwanaume yeyote yule anakihitaji kwa mwanamke.
Kiufupi yuko kwenye orodha ya wale akinadada wachache mno wenye umbo adimu, uso wenye sura ya upole na macho makubwa ya mviringo yanayotaka kama kudondoka hivi na yakusinziasinzia huku nyuma akiwa amefungashia mzigo mkubwa sana usiowiana na mwili wake!!!
Kikao chetu hicho kilimalizika siku hiyo pasipo kutozaa matunda yaliyotarajiwa, tuliagana siku hiyo, na kila mtu akachukua njia yake.
Baada yakama mwezi mmoja hivi kupita alinitumia sms kunijulia hali, kwani tangu siku ile mie nilikata tamaa kabisa na niliheshimu na kukubaliana na msimamo wake. Hivyo sikuwa namewasiliana naye tena.
Siku moja baada ya kama miezi miwili kupita, alinipigia simu na kusema anataka kuja kunitembelea nyumbani ninapoishi. Mie nikaona kama vile kuna kila dalili za mwanga wa matumaini kuchanua.
Haraka haraka nikamwambia karibu sana. Siku ya jumapili dada akatia timu nyumbani kwangu ninapoishi. Lakini cha kushangaza msimamo wake ukabakia vilevile. "Kaka ulishachelewa soon nitaolewa".
Nilichukia vibaya mno. Kila nilichojaribu, nilionekana kama mtoto mdogo ambaye yuko chekechea katika darasa la kushawishi, kubembeleza na kutongoza. Kila nilichojaribu nilijibiwa kabla ya kumaliza sentensi.
Hasira, machungu, huzuni na fadhaa nilivyokuwa navyo siku hiyo nilihisi kama vile moyo wangu unataka kupasuka na huku kijasho kikinitoka. Wakati fulani nilisahau kama pale palikuwa kwangu na kutaka kuuliza mahali toile ilipo!!!
Wiki kama tatu hivi baadae, Apaikunda alinipigia simu akasema anahitaji kuja tena kunitembelea nyumbani. Mie nikagoma, akasema hapana, anajambo anataka kuja kunieleza. Siku ikafika, akatia timu tena.
Akasema anakubali kuwa rafiki yangu, lakini hatutooana. Nilikubaliana naye kwa shingo upande. Mie nilimtaka jumla jumla, yeye ananitaka rejareja. Kweli hii ni sawa??
Lakini siku hiyo tofauti na siku yakwanza, tulikubaliana kugegedana.
Duuuuu!!! Kweli nimeona maumbo mengi ya hawa viumbe, lakini hili umbo lilikuwa balaaaaaa!!!!!
Tangu siku hiyo ikawa kama kawaida yetu mara kwa mara.
Sasa wanajamvi, nimempata mchumba harisi mwenye kutaka mme na aliye tayari kuishi na mimi kwa muda wa maisha yake yote.
Na habari hii nimeifikisha kwa Apaikunda kama ilivyo. Sikutegemea, dada kacharuka, kawa mkali mithili ya mbogo aliyejeruhiwa. Eti alishaachana na bwanake siku nyingi, nisithubutu kufanya hivyo.
Na amenitamukia wazi kwa macho makavu kabisa kwamba nisipomuoa yeye mwaka huu sitaumaliza!!
Wanajamvi, kuna usalama kweli hapa??
Angalizo: kama huna cha kuchangia, pita kimyakimya.
Nakumbuka ilikuwa Juni 2012, nilipokutana na dada huyu aitwaye Apaikunda.
Kama ilivyo kawaida ya wanaume, siku hiyo nikamwomba namba yake ya simu, hakusita, akanipatia. Tulikuwa tukiongea kwenye simu mara kwa mara na kutumiana sms mara nyingi.
Siku moja wikendi nikamtafuta, hakusita kama ilivyokuwa mwanzo. Tukakutana sehemu moja ya wazi kwa minajiri ya kutaka kufahamiana zaidi.
Maongezi yetu ya kwanza yalichukua kama masaa matatu hivi na ndio yaliyopelekea kumfahamu dada huyo kuwa anaitwa Apaikunda na ni mwajiriwa wa kampuni moja hapa Jijini.
Ndani ya masaa hayo matatu nilimtolea yangu yote ya moyoni. Jibu lake lilikuwa "kaka nina mchumba wangu nimpendaye sana na tayari tumeshatambulishana kwa wazazi".
Kila nilipojaribu kumwonyesha nia yangu ya dhati, kwamba lengo na madhumuni yangu siyo kumpotezea muda, bali kwa uhakika ni kumtaka awe wangu wa kufa na kuzikana.
Jibu lake lilikuwa moja tu "pole kaka, ulishachelewa na sina namna yoyote ile ya kufanya kwani niliyenaye ananitosha na nampenda mno na siwezi kumwacha wala kumsariti".
Kiukweli huyo Apaikunda ana sifa zote za kuitwa dada mrembo. Ana kila kitu ambacho mwanaume yeyote yule anakihitaji kwa mwanamke.
Kiufupi yuko kwenye orodha ya wale akinadada wachache mno wenye umbo adimu, uso wenye sura ya upole na macho makubwa ya mviringo yanayotaka kama kudondoka hivi na yakusinziasinzia huku nyuma akiwa amefungashia mzigo mkubwa sana usiowiana na mwili wake!!!
Kikao chetu hicho kilimalizika siku hiyo pasipo kutozaa matunda yaliyotarajiwa, tuliagana siku hiyo, na kila mtu akachukua njia yake.
Baada yakama mwezi mmoja hivi kupita alinitumia sms kunijulia hali, kwani tangu siku ile mie nilikata tamaa kabisa na niliheshimu na kukubaliana na msimamo wake. Hivyo sikuwa namewasiliana naye tena.
Siku moja baada ya kama miezi miwili kupita, alinipigia simu na kusema anataka kuja kunitembelea nyumbani ninapoishi. Mie nikaona kama vile kuna kila dalili za mwanga wa matumaini kuchanua.
Haraka haraka nikamwambia karibu sana. Siku ya jumapili dada akatia timu nyumbani kwangu ninapoishi. Lakini cha kushangaza msimamo wake ukabakia vilevile. "Kaka ulishachelewa soon nitaolewa".
Nilichukia vibaya mno. Kila nilichojaribu, nilionekana kama mtoto mdogo ambaye yuko chekechea katika darasa la kushawishi, kubembeleza na kutongoza. Kila nilichojaribu nilijibiwa kabla ya kumaliza sentensi.
Hasira, machungu, huzuni na fadhaa nilivyokuwa navyo siku hiyo nilihisi kama vile moyo wangu unataka kupasuka na huku kijasho kikinitoka. Wakati fulani nilisahau kama pale palikuwa kwangu na kutaka kuuliza mahali toile ilipo!!!
Wiki kama tatu hivi baadae, Apaikunda alinipigia simu akasema anahitaji kuja tena kunitembelea nyumbani. Mie nikagoma, akasema hapana, anajambo anataka kuja kunieleza. Siku ikafika, akatia timu tena.
Akasema anakubali kuwa rafiki yangu, lakini hatutooana. Nilikubaliana naye kwa shingo upande. Mie nilimtaka jumla jumla, yeye ananitaka rejareja. Kweli hii ni sawa??
Lakini siku hiyo tofauti na siku yakwanza, tulikubaliana kugegedana.
Duuuuu!!! Kweli nimeona maumbo mengi ya hawa viumbe, lakini hili umbo lilikuwa balaaaaaa!!!!!
Tangu siku hiyo ikawa kama kawaida yetu mara kwa mara.
Sasa wanajamvi, nimempata mchumba harisi mwenye kutaka mme na aliye tayari kuishi na mimi kwa muda wa maisha yake yote.
Na habari hii nimeifikisha kwa Apaikunda kama ilivyo. Sikutegemea, dada kacharuka, kawa mkali mithili ya mbogo aliyejeruhiwa. Eti alishaachana na bwanake siku nyingi, nisithubutu kufanya hivyo.
Na amenitamukia wazi kwa macho makavu kabisa kwamba nisipomuoa yeye mwaka huu sitaumaliza!!
Wanajamvi, kuna usalama kweli hapa??
Angalizo: kama huna cha kuchangia, pita kimyakimya.