Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
- Thread starter
- #41
Rutashubanyuma i know ni ngumu but ndio hivyo......
maamuzi magumu hayo......... Elizabeth Dominic..lol
Last edited by a moderator:
Rutashubanyuma i know ni ngumu but ndio hivyo......
Huo ni ushahidi dada yangu!. Ndoa yenyewe inakuwa bado kutimizwa.
Kyaiyembe umesema hakuna ndoa nahuku ndoa mshaifunga? Inategemea mmefunga ndoa ya aina gani, kama ninayoijua mimi ndoa ipo kabisa...
Hakuna ndoa kama JOGOO HAWIKI!. Elizabeth Dominic na Rutashubanyuma hilo mlitambue
yeye alioa bila kujua anatatizo gani? huku ndio kujaribu jehanam hakutakiwa kufanya hivyo ila alitakiwa kuoa ndoa za msimu ili awe anatest kuona kama jogoo anawika nje ya hapo ni aibu
Ruta unasemea ndoa nje ya misisngi ya UKRISTO na UUMBAJI.ndoa siyo lazima itimizwe kitandani bali ni makubaliano ya kuishi nyote..........for better or for worse..................in most cases we vow in vain because when the real tests come along we falter miserably.......... Kyaiyembe
Hata hizo za Uingereza, Marekani Afrika Kusini na kwingineko lazima kuna neno " I pronounce you HUSBAND and WIFE"Kyaiyembe mwenzetu haya ya majogoo kuwika wayatoa wapi....nijuavyo ndoa ni kukubalina kuishi pamoja kw mazuri hata mabaya kama ya hayo majogoo yasiyowika........
Na likiwika wanao shuhudia watasema kuwa wahusika wamafanya tendo la ndoa!.jogoo laweza kuwika na kufanya machahari yake yote na bado isiwe ni ndoa kama hajakubalina kuishi pamoja............ Kyaiyembe
Rutashubanyuma kuna dada mmoja ameolewa na 0.5 yeye alikuwa mweusi kama lami looo ametumia mkorogo amefanana na mumewe usoni tatizo akivaa malapa ukimwangalia vidole vya miguu unapata mshangaoLemonade ni kweli bi harusi alikuwa akikimbia mechi kwa kuhofia asije julikana yeye ni tetracycline..........sura ni nyingine na kiwiliwili ni sura nyingine.....................lakini alikuja kutiwa kitanzini
Mchungaji kapera hakuacha kuangaza-angaza macho
Kwenye kwaya ya kanisa lake akajionea kitoweo murua
Binti sura nyororo na rangi yake ni hudhurungi bila karaha
Mchungaji kuona hivyo akaambuliwa suluba ya mahaba tele
Mchubuo wa Bi harusi wamzalishia talaka yenye simango kibao!
Binti sura yawaka lakini mwili wake kaufunika gubigubi la ushungi
Wengi waliamini hayo ni maadili ya malezi bora aliyolelewa nayo
Kumbe yeye ana lake jambo na siri kubwa alikuwa anaisetiri
Hata umakini wa mchungaji haukufua dafu na mkenge kuingizwa
Mchubuo wa Bi harusi wamzalishia talaka yenye simango kibao!
Hayawi hayawi huwa, mchungaji akabeba chake bila ya mikwara
Siku zikawa siku na Bi harusi kukwepa majukumu yake ya kitandani
Visingizio kibao hasa majukumu kuwa ndiyo ghala la utetezi wake
Asubuhi kudamka mapema na usiku kuchelea kulala akificha utupu wake
Mchubuo wa Bi harusi wamzalishia talaka yenye simango kibao!
Za mwizi ni arobaini na zilipofikia aliona cha moto kikimwakia
Siri ikaanikwa hadharani kumbe mambo yote ni mchubuo!
Mchungaji akajawa na hamaki asiamini alivyonyimwa unyumba
Ama kwa hakika tatizo ni matarajio ya mchungaji kuyumbishwa
Mchubuo wa Bi harusi wamzalishia talaka yenye simango kibao!
Jisomee Mchubuo wa Bi harusi wamzalishia talaka yenye simango kibao
Ruta unasemea ndoa nje ya misisngi ya UKRISTO na UUMBAJI.
Sijawahi kusikia watu waliofanya tendo la ndoa kanisani au msikitini.
Hata kimila wazee wetu walikuwa nautaratibu mzuri kuhusu ndoa.
Nijuavyo mimi ndoa ni makubaliano ya wawili waishi kama mke na mme!
Sasa sijui kama unaelewa maana ya kuwa mke wa, na kuwa mme wa.
Ruta katika kauli hizo hapo juu lazima kuwepo na kitendo maalmu.
Na ikitokea mmojawapo akalalamika kuwa tendo hilo halifanyiki NDOA ubatilishwa!.
Rutashubanyuma kuna dada mmoja ameolewa na 0.5 yeye alikuwa mweusi kama lami looo ametumia mkorogo amefanana na mumewe usoni tatizo akivaa malapa ukimwangalia vidole vya miguu unapata mshangao
Samahani nisaidie kidogo, nipe tofauti ya ndoa hizi!Kyaiyembe ukweli ni kuwa mnapooana hamsemi kuwa mnakwenda kudu..........hay ni matunda yake na tena siyo yote.............mkishindwa kwa sababu ya kimaumbile siyo sababu ya kuachana.
Hizo ndizo kafara zenyewe............until death us apart..............the Scriptures say
Blaki Womani " na 0.5" ndiyo nini ? Sijaelewa maana yake.................khalafu huyu mdada wa ajabu mume tayari anaye na kwani alikuwa hajui rangi yake.......................sasa hii khofu ya kujichubua yatoka wapi. Uzoefu wangu ni kuwa unapohangaika kutafuta rangi au maumbile tofauti ya yale uliyonayo unakhoji busara za Muumba kukupa alichoona ndicho stahili yako........na matokeo yake unachafua kazi murua ya maumbile yako. Khadi leo ninatafuta mchubuo mwenye mvuto kulikoni alivyokuwa awali bado sijakutana naye................am still searching, though............na sitarajii kukutana naye.