Mchezo wa Voliball unavyowavutia wanawake wa Kashmir

Abdull Kazi

JF-Expert Member
Dec 29, 2012
322
255
Imetafsiriwa kutoka katika gazeti la RS.

WAKATI mpira wa wavu ukishika kasi miongoni mwa wachezaji wa kike wa Kashmir, baadhi yao wamejitokeza na kujifunza kwa juhudi kubwa mchezo huo

Katika viwanja mbali mbali wanaonekana wasichana wakishiriki kwa kutupa mipira kwa nguvu, kuelekea kwa wapinzani wao, huku nao wakijibu mashambulizi hayo

Wachezaji hawa wa kike hutoa damu na jasho kila siku kujifunza mbinu za mpira wa wavu, kuhakikisha wanajenga majina yao kwenye mchezo huo, ikiwa ni maandalizi ya kuwaandaa wasichana wa Kashmir kushiriki mashindano mbali mbali

Amir Bhat na Munner Aalam, walifungua Klabu yao ya mpira wa wavu kwa Wasomi wanawake mwaka wa 2014.

"Kila mara kulikuwa na ushiriki zaidi wa wachezaji wa kike kutoka Jammu na wachache kutoka Kashmir. Ili kuhamisha utawala huu, klabu ilikaribisha na kuanza kuwafunza wasichana,” Muneer alisema.

Klabu hiyo ilianzishwa mwaka wa 2011, ikitambulika kama Klabu ya Mpira wa Wavu ya Wasomi ikiwa inafahaamika zaidi kwa kutengeneza seti ya wachezaji wa mpira wa wavu huko Kashmir wanaoshiriki katika michuano ya kitaifa.

Kwa sasa klabu hiyo ina wasichana 32 wa vikundi tofauti wakiwa na umri mbali mbali ambao ni kutoka wilaya tofauti kama vile Baramulla, Ganderbal, Shopian

Muneer anasema hapo awali wasichana hao baada ya kumaliza kucheza mashindano ya vyuo vikuu hawakuwa na chaguo lolote la kucheza na hivyo klabu hiyo inawapa jukwaa la kwenda mbali zaidi katika mchezo huo.

"Tumetoa jukwaa kwao la kuendeleza vipaji vyao walivyokuwa navyo vyuoni, na kwa sasa Wachezaji wetu hawa wameweka viwango bora na wanaweza kushindana na wachezaji wa jimbo lolote,” aliongeza.

Akifanya kazi ya kutafuta vipaji katika ngazi ya chini kabisa kwa kile anachoeleza kwamba mchezo unahitaji kuinuliwa zaidi.

"Wachezaji wanapaswa kupata ufikiaji mzuri wa viwanja vya ndani na malazi kwa wale ambao wanatoka wilaya zingine. Hosteli zinapaswa kutengenezwa ili kuchukua watoto. Kwa sera ya michezo, kila mtoto anapaswa kupenda, "alisema.

Anasema kila siku inayopita, wanawake zaidi na zaidi wanaibuka huku wengine wakijitahidi kuwa bora zaidi.

Insha Bashir, mchezaji pekee wa kike kutoka Kashmir ambaye amechezea timu ya taifa mara 4 mfululizo akiwakilisha Jammu na Kashmir kama nahodha kwa sasa ni kocha wa timu ya voliboli ya wavulana na wasichana huko Kashmir Kaskazini.

Akiwa ni mwenyeji wa Baramulla, Insha anaeleza kuwa alilazimika kuhamia Srinagar kila siku ili kujifunza mchezo huo.

Anasema kwamba alikuwa anaondoka nyumbani kwake mapema saa 6:30 asubuhi na kurudi nyumbani saa 11:00 jioni.

"Nilikuwa na wakati mgumu wakati huo wakati hakukuwa na kituo cha mpira wa wavu katika wilaya yangu. Nauli ilikuwa kubwa sana na nyakati fulani ilikuwa vigumu kwangu kulipa.”

Alisema,

“Hapo awali hakukuwa na mbinu nyingi zilizofunzwa kwenye mchezo lakini Muneer Aalam alinoa ujuzi wangu. Alinifundisha kwa miaka 4 ambayo ilinifanya kuwa nahodha wa timu ya J&K.”anasema

Akiwa amecheza michuano 3 ya kitaifa ya vyuo vikuu na michuano 7 ya serikali, kila mara alitaka kuweka mazingira mazuri ya mpira wa wavu katika wilaya hiyo ili wasichana wadogo wasikabiliane na matatizo ambayo alikumbana nayo.

"Hapo awali timu ya wavulana ingeenda tu kwa mechi. Niliamini kwamba timu ya wasichana inapaswa kwenda pia. Nilizungumza na mamlaka yangu ya juu na hatimaye ikawezekana.”

Kwa zaidi ya miaka miwili sasa timu ya wasichana kutoka Baramulla inakwenda kwenye mechi huku zikiwa zieapata mafunzo chini ya Insha.

“Wasichana wanajitokeza kwa wingi. Ninapaswa kuwafunza wasichana 15 pekee lakini ninapata wasichana 30-35.”anasema Insha

Mchezaji mwingine wa kitaifa, Arifa Gulzar alielezea uzoefu wake wa mechi za kitaifa na kusema.

“Licha ya ushindani mkubwa tunaokabiliana nao, timu yetu inafanya vizuri sana. Tunathaminiwa na kiwango cha uchezaji kimepanda kutokana na ufundishaji bora tunaopokea.”

Arifa ameolewa na pia ana mtoto na anatazamia kufanya mazoezi zaidi.

"Wazazi wanapaswa kuwaruhusu wasichana wao kwenda kwenye mchezo huo kwani ni baadhi tu wamepewa talanta hivyo hawapaswi kupoteza talanta ya binti zao," alisema.

Asiya Awan(21) anayetokea Bandipora, akiwa tayari amecheza michuano miwili ya ngazi ya taifa ya vyuo vikuu na tatu za serikali,akidhamiria kufanya kazi katika mchezo huo, alisema kuwa mchezo wa voliboll ni mchezo wa ndoto yake



"Michezo ya vyuo vikuu tuliyoshiriki na kushika nafasi ya pili baada ya kushinda mechi tatu ilikuwa ni mchezo wa kipekee sana kwetu
Mwaka jana, tulicheza katika michuano ya serikali na baada ya muda mrefu, timu yetu ilishika nafasi ya pili.”

Akicheza kama setter katika mchezo huo, alisema kuwa klabu yake ya Elite volleyball imewaumbua wachezaji kwani ni mchezo wa timu na kila mmoja anatakiwa kuweka juhudi sawa.

"Tuna uwezo na tunachohitaji ni nafasi tu. Tunaweza kuwa sehemu ya jukwaa la kimataifa pia,” alisema.

Suriya Feroz kutoka Chadoora ambaye hapo awali alikuwa mchezaji mahiri wa Kabaddi alihamasishwa kuona kocha Muneer akifundisha mpira wa wavu kwa wasichana.

Bila kufikiria tena, alibadilisha mchezo wake na kuchagua voliboli.

"Kocha aliniambia kuwa urefu wangu ni mzuri, ambayo ni hatua ya ziada katika mchezo huu, kwa hivyo nilianza kucheza mchezo kwa umakini sana," alisema.

Akiwa amecheza michuano mingi ya serikali, michuano ya kitaifa na 2 ya vyuo vikuu, alisema kuwa idadi ya wasichana wanaocheza kutoka wilaya yake ni ndogo ikilinganishwa na Srinagar na wachezaji wanapaswa kuja Polo Ground kwa mafunzo.
Anasema umbali wa anakotoka kwake si kitu cha kujali zaidi ya mapenzi yake kwenye mchezo huo yanayomfanya aendelee kuucheza

Baadhi ya wachezaji bora na wazoefu wanapitisha ujuzi kwa kizazi kipya na kutoa mafunzo kwa wachezaji chipukizi.

Klabu ya Mpira wa Wavu ya Kashmir, iliyoanzishwa hivi karibuni, inaendeshwa na wachezaji wawili wa mpira wa wavu- Sadiya Hussain na Anas Younis.

Syed Aqsa mwenye umri wa miaka 21 amekuwa akipenda mpira wa wavu tangu utotoni.

Akiwa ameshacheza michuano mbalimbali ya vyuo vikuu, alichohitaji ni mwongozo zaidi hali iliyomlazimu akajiunga na klabu hiyo ili aweze kucheza kwa ustadi.

Anasema alipata msukumo kwa kutazama wasichana wakitengeneza majina yao katika michezo tofauti, na kujiuliza kwanini yeye hawezi kushinda kama wao?

“Siogopi kamwe. Mimi hujaribu kila wakati kuwa bora kwenye mchezo. Mtu anapaswa kuweka lengo kabla ya kwenda kortini," alisema.

Akizungumzia kuongezeka kwa idadi ya wasichana katika mpira wa wavu, alisema kuwa hapo awali watu hawakuupa umuhimu mkubwa suala la michezo.

"Voliboli imekuwa ndoto yangu. Kwa bahati nzuri nina binamu yangu ambaye ni mwalimu wa michezo na alipendekeza niende kwenye michezo kwani ina wigo mkubwa,” aliongeza.

Binti mwingine kutoka Srinagar, Peerzada Shaista Farooq Masoodi, ambaye kwa sasa anasoma katika Women College MA Road hakuweza kukaa kwa muda mrefu kwa sababu ya masuala ya afya yake. “Mara tu nilipopata nafuu, niliruka kurudi kortini. Sikuweza kukaa mbali na mahakama kwa muda mrefu,” alisema.

Akiwa na makocha wa klabu hiyo, Shaista pamoja na wengine wanafanya mazoezi magumu na kujiandaa kwa mechi zijazo za ngazi ya serikali. "Kila msichana anapaswa kushiriki katika mchezo na kufikia pale anapotakiwa kuwa. Mtu anapaswa kufanya kazi kwa bidii ili kudhibitisha uwezo wake. Hata leo wasichana wengi ambao wanaweza kuwa wachezaji wazuri, hawaruhusiwi kucheza na wazazi wao,” alisema.

Hata hivyo anaelezea wasiwasi wake kuhusu vifaa vinavyotolewa katika wilaya nyingine za bonde hilo.

“Miundombinu bado haitoshi kwa wasichana ambao ni wa wilaya nyingine. Kunapaswa kuwa na vifaa katika wilaya zote," alisema.

Kando ya kuwa mjuzi wa michezo mingine, Syed Rabiya kutoka Baramulla alichagua voliboli aliposema, "Moyo wangu unadunda kwa voliboli pekee."

Hivi sasa anajitayarisha kwa michuano ijayo ya jimbo na anatamani kuchaguliwa.

“Ninajituma sana katika michezo na ninashiriki katika michezo mbalimbali. Tunapata mafunzo ya kushinda na kutengeneza nafasi yetu kwenye mchezo,” alisema.

Alisema kuwa wachezaji mbalimbali wa kimataifa na kitaifa wameibuka kutoka katika wilaya zake na wengi wanajitokeza.

"Ninahisi kushikamana na mchezo huu na nina uhakika na hili. Ninajifunza mchezo kwa hamu na kusimamia masomo yangu pia”anasema





s_637826773362171493_volley.jpg
 
Back
Top Bottom