Mchengerwa: Rufiji Mbioni Kuwa Mkoa

Mchengerwa: Rufiji Mbioni Kuwa Mkoa

Baada ya harakati za kugawa majimbo ya Uchaguzi kushika Kasi suala la kuunda Mikoa mipya nalo limeanza kujitokeza ambapo Waziri wa Tamisemi bwana Mchengerwa amesema huenda Rufiji ikawa Mkoa Mpya.Pia soma Ushauri. Ni muda sahihi Bagamoyo ipewe hadhi ya mkoa

Waziri huyo na Mbunge wa Rufiji amesema jambo Hilo litategemea ikiwa Wilaya za Mkoa jirani wa Lindi ya Kilwa kama itakubali Ili kufanikisha Vigezo.

Ikumbukwe Mikoa mingine iliyoomba kugawanywa na kuwa Mkoa Mpya ni

-Chato (itachukua Wilaya za Kagera,Mwanza,Kigoma),

-Mkoa wa Manonga( kutoka Tabora),

-Mkoa wa Handeni( kutoka Tanga),

-Mkoa wa Kilombero (kutoka Morogoro) na

-Mkoa wa Rufiji (kutoka Pwani & Lindi).

View: https://www.instagram.com/reel/DHyZU5Kom_c/?igsh=a3NlOHk4bmMxYnly

My Take
Kuongeza Mikoa mipya bila kubadili mfumo wa Usimamizi wake haiwezi kusaidia lolote kwenye maendeleo sana sana itaongeza mzigo Kwa walipakodi.

Ni jambo jema Mkoa wa MOROGORO ni makubwa sana kuanzia MOROGORO mjini hadi Ketaketa Wilaya ya Ulanga au Kilosa kwa Mpepo Wilaya ya Malinyi ni mbali sana.
 
Wangefanya mpango wa mfumo wa majimbo tu..Tz iwe na majimbo kama 4 au 5 tu yenye magavana wao kwisha. Mikoa mikoa inazidisha kuwa na viongozi wengi wa kunyonya bajeti ya Nchi
 
Wangefanya mpango wa mfumo wa majimbo tu..Tz iwe na majimbo kama 4 au 5 tu yenye magavana wao kwisha. Mikoa mikoa inazidisha kuwa na viongozi wengi wa kunyonya bajeti ya Nchi
1. Moro ni kubwa ikatwe
2. Pwani ni kubwa ikatwe
Tupate mikoa mipya ya kilombero na Rufiji na
1. Kilombero makao makuu yawe ifakara
2. Rufiji makao makuu yawe Ikwiriri
 
Wangefanya mpango wa mfumo wa majimbo tu..Tz iwe na majimbo kama 4 au 5 tu yenye magavana wao kwisha. Mikoa mikoa inazidisha kuwa na viongozi wengi wa kunyonya bajeti ya Nchi
Majimbo ndio nini? Kenya Kuna Majimbo? Mbona mumekariri ujinga? Kwani ikiitwa Mikoa Kuna shida gani?
 
1. Moro ni kubwa ikatwe
2. Pwani ni kubwa ikatwe
Tupate mikoa mipya ya kilombero na Rufiji na
1. Kilombero makao makuu yawe ifakara
2. Rufiji makao makuu yawe Ikwiriri
Mkoa mkubwa namba 1 🇹🇿 ni Tabora
 
Unaweza kuwa na hospital ya hadhi ya mkoa wilayani?..utapata huduma zinazopatikana ofisi za mkoa wilayani?..
Ndio ,kwani Nansio ukerewe wanajenga ya hadhi gani? Tuna hospital ngapi za hadhi ya kitaifa za private huko Wilayani? Eg Ikonda Market,Hydom Manyara,Nzega Vijijini nk?

Ujinga wa kukwepa majukumu ndio unawafanya mnawaza hivyo na Kwa taarifa Yako tuu sio sifa kusafiri umbali.mkubwa kufuata Huduma Kwa huo utoto wa sijui Wilayani sijui Mkoani au taifani.
 
Uliendelea, lakini siyo kwa kiwango cha kutisha km cha kabla ya centralization!
Africa upigaji umekuwa kama asili yetu, ni kama tulivyo relation oriented kwenye jamii zetu.
Hakuna mahala upigaji umepungua na kutowapa mamlaka ya usimamizi Serikali za Mitaa ndio imefanya wizi uwe chain kubwa ya kuanzia wizarani.
 
Morogoro na Tabora pekee ndio mikoa yenye sifa ya kugawanywa.

Huko kwingine ni siasa tupu.

Pwani kama ni kubwa wahamishie baadhi ya wilaya mkoa wa Dar
 
Ongezeko la utumizi wa mifuko hauhitaji ongezeko la majengo
 
Uliendelea, lakini siyo kwa kiwango cha kutisha km cha kabla ya centralization!
Africa upigaji umekuwa kama asili yetu, ni kama tulivyo relation oriented kwenye jamii zetu.
I bed to differ on suala la upiga, haujaisha ila umebadilika, instead ya kuanzia chini unaanzia juu kushuka.
If you tell me ni kupunguza upigaj is not right
 
Morogoro na Tabora pekee ndio mikoa yenye sifa ya kugawanywa.

Huko kwingine ni siasa tupu.

Pwani kama ni kubwa wahamishie baadhi ya wilaya mkoa wa Dar
Fikiria raia anatoka ikwiriri anapita dsm anafata huduma ya kimkoa kibaha kisha anarudi ikwiriri, huoni ni usumbufu mkubwa?
 
Back
Top Bottom