Mchengerwa: Rufiji Mbioni Kuwa Mkoa

Mchengerwa: Rufiji Mbioni Kuwa Mkoa

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
79,088
Reaction score
84,978
Baada ya harakati za kugawa majimbo ya Uchaguzi kushika Kasi suala la kuunda Mikoa mipya nalo limeanza kujitokeza ambapo Waziri wa Tamisemi bwana Mchengerwa amesema huenda Rufiji ikawa Mkoa Mpya.Pia soma Ushauri. Ni muda sahihi Bagamoyo ipewe hadhi ya mkoa

Waziri huyo na Mbunge wa Rufiji amesema jambo Hilo litategemea ikiwa Wilaya za Mkoa jirani wa Lindi ya Kilwa kama itakubali Ili kufanikisha Vigezo.

Ikumbukwe Mikoa mingine iliyoomba kugawanywa na kuwa Mkoa Mpya ni

-Chato (itachukua Wilaya za Kagera,Mwanza,Kigoma),

-Mkoa wa Manonga( kutoka Tabora),

-Mkoa wa Handeni( kutoka Tanga),

-Mkoa wa Kilombero (kutoka Morogoro) na

-Mkoa wa Rufiji (kutoka Pwani & Lindi).


My Take
Kuongeza Mikoa mipya bila kubadili mfumo wa Usimamizi wake haiwezi kusaidia lolote kwenye maendeleo sana sana itaongeza mzigo Kwa walipakodi.

 
Baada ya harakati za kugawa majimbo ya Uchaguzi kushika Kasi suala la kuunda Mikoa mipya nalo limeanza kujitokeza ambapo Waziri wa Tamisemi bwana Mchengerwa amesema huenda Rufiji ikawa Mkoa Mpya.

Waziri huyo na Mbunge wa Rufiji amesema jambo Hilo litategemea ikiwa Wilaya za Mkoa jirani wa Lindi ya Kilwa kama itakubali Ili kufanikisha Vigezo.

Ikumbukwe Mikoa mingine iliyoomba kugawanywa na kuwa Mkoa Mpya ni Chato (itachukua Wilaya za Kagera,Mwanza,Kigoma),Mkoa wa Manonga( kutoka Tabora),Mkoa wa Handeni( kutoka Tanga),Mkoa wa Kilombero (kutoka Morogoro) na Mkoa wa Rufiji (kutoka Pwani & Lindi).

View: https://www.instagram.com/reel/DHyZU5Kom_c/?igsh=a3NlOHk4bmMxYnly

My Take
Kuongeza Mikoa mipya bila kubadili mfumo wa Usimamizi wake haiwezi kusaidia lolote kwenye maendeleo sana sana itaongeza mzigo Kwa walipakodi.

Hili suala bora wangeenda slow kuliko kuharakisha kama wanavyo fanya
 
Huo mfumo mpya wa usimamizi unaoutaka wewe ndio ukoje?
1.Kuondoa ma DC na kuwapa Nguvu Serikali za Mitaa kuamua mambo Yao badala ya Sasa kuwa mawakala wa Serikali kuu.

2.Kuwa na Kanuni maalumu za mgawanyo wa Rasilimali za Serikali Kuu kama ilivyo Nchi nyingi hasa USA badala ya Sasa kutegemea uchawa(viongozi wanaotoka kwenu).

3.Kukusanya na kupanga matumizi ya Fedha wenyewe badala ya Kila chanzo kuingia Serikali Kuu harafu ndio mnasubiria huruma za walioko Dom/Dar.
 
Ongeza mikoa, ongeza wilaya, ongeza majimbo ya uchaguzi, ongeza kila kitu. Vitu vyote hivyo vinaongeza mzigo kwa mlipakodi kugharamia serikali kubwa.

Sehemu kubwa ya mapato itaenda kwenye uendeshaji wa serikali, maendeleo tutachelewa sana.

Mapato yasipotosha tutalazimika kukimbilia kwenye mikopo ili kuwezesha serikali kuendelea kuwepo huku maendeleo kwa wananchi yakiwa ni kiduchu sana.
 
3.Kukusanya na kupanga matumizi ya Fedha wenyewe badala ya Kila chanzo kuingia Serikali Kuu harafu ndio mnasubiria huruma za walioko Dom/Dar.
Hili si lilishafanyika huko nyuma, na matokeo yake watu wakawa wanajipigia tu pesa kwenye halmashauri za miji na wilaya bila huruma na hakuna wa kuwauliza?
 
Baada ya harakati za kugawa majimbo ya Uchaguzi kushika Kasi suala la kuunda Mikoa mipya nalo limeanza kujitokeza ambapo Waziri wa Tamisemi bwana Mchengerwa amesema huenda Rufiji ikawa Mkoa Mpya.Pia soma Ushauri. Ni muda sahihi Bagamoyo ipewe hadhi ya mkoa

Waziri huyo na Mbunge wa Rufiji amesema jambo Hilo litategemea ikiwa Wilaya za Mkoa jirani wa Lindi ya Kilwa kama itakubali Ili kufanikisha Vigezo.

Ikumbukwe Mikoa mingine iliyoomba kugawanywa na kuwa Mkoa Mpya ni

-Chato (itachukua Wilaya za Kagera,Mwanza,Kigoma),

-Mkoa wa Manonga( kutoka Tabora),

-Mkoa wa Handeni( kutoka Tanga),

-Mkoa wa Kilombero (kutoka Morogoro) na

-Mkoa wa Rufiji (kutoka Pwani & Lindi).

View: https://www.instagram.com/reel/DHyZU5Kom_c/?igsh=a3NlOHk4bmMxYnly

My Take
Kuongeza Mikoa mipya bila kubaki mfumo wa Usimamizi wake haiwezi kusaidia lolote kwenye maendeleo sana sana itaongeza mzigo Kwa walipakodi.

Kuongeza mikoa na majimbo ni famba sana, haina tija.
 
Back
Top Bottom