DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb) ametangaza rasmi kuanza kutumika kwa Kitita cha Huduma Muhimu cha Bima ya Afya kwa Wote kwa awamu ya kwanza.
Amesema kuwa kitita hicho kitaanza kutumika Januari 26, 2026 kwa kundi litakalogharamiwa na Serikali. Haya ameyasema leo wakati akizungumza na Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi Watendaji, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya kuhusu utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.
Amesema kuwa suala la afya ni suala muhumi ambalo limebeba utu wa Mtanzania na mhimili wa maendeleo hivyo kila kiongozi ni lazima alibebe na kulifanya ajenda ya kudumu katika vikao vyote ili liweze kutekelezeka na kuleta matokeo chanya kwa afya za watanzania.
Mhe. Mchengerwa amesema kuwa kulingana na maamuzi ya Serikali ya kuanza utekelezaji wa mpango huu kwa awamu, ni wajibu wa kila mmoja kutekeleza majukumu yake kwa weledi ili kufanikisha maono haya ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.
”Bila afya njema kwa wananchi ni ngumu kufanya mabadiliko yoyote ya kitaifa kwa wananchi wanaotumia muda mwingi hospitalini kuliko kazini. Hata teknolojia iwe ya kisasa kiasi gani, hata sera ziwe nzuri kiasi gani, bila watu wenye afya-hakuna mabadiliko yatakayodumu hivyo ni lazima hili tulitekeleze kwa nguvu zetu zote ili wananchi waweze kuwa na uhakika wa matibabu,” alisema Mhe. Mchengerwa.
Kutokana na hayo, amesema kuwa kutakuwa na uzinduzi wa kihistoria wa Bima ya Afya kwa Wote kabla ya kukamilika kwa siku 100 za Mheshimiwa Rais, uzinduzi ambao utabadilisha dhana ya haki ya huduma za afya nchini Tanzania na kuweka msingi mpya wa ulinzi wa afya ya Mtanzania.
Aliwasisitiza viongozi hao kuwa kwa sasa ajenda ya Bima ya Afya kwa Wote lazima iondoke kwenye ngazi ya waraka na iingie kwenye maamuzi ya kila siku ya uongozi wa Mkoa.
Pia Soma: Gharama ya Bima ya Afya kwa wote ni Tsh. 150, 000 kwa kaya, wasio na uwezo kugharamiwa na serikali
Amesema kuwa kitita hicho kitaanza kutumika Januari 26, 2026 kwa kundi litakalogharamiwa na Serikali. Haya ameyasema leo wakati akizungumza na Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi Watendaji, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya kuhusu utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.
Amesema kuwa suala la afya ni suala muhumi ambalo limebeba utu wa Mtanzania na mhimili wa maendeleo hivyo kila kiongozi ni lazima alibebe na kulifanya ajenda ya kudumu katika vikao vyote ili liweze kutekelezeka na kuleta matokeo chanya kwa afya za watanzania.
Mhe. Mchengerwa amesema kuwa kulingana na maamuzi ya Serikali ya kuanza utekelezaji wa mpango huu kwa awamu, ni wajibu wa kila mmoja kutekeleza majukumu yake kwa weledi ili kufanikisha maono haya ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.
”Bila afya njema kwa wananchi ni ngumu kufanya mabadiliko yoyote ya kitaifa kwa wananchi wanaotumia muda mwingi hospitalini kuliko kazini. Hata teknolojia iwe ya kisasa kiasi gani, hata sera ziwe nzuri kiasi gani, bila watu wenye afya-hakuna mabadiliko yatakayodumu hivyo ni lazima hili tulitekeleze kwa nguvu zetu zote ili wananchi waweze kuwa na uhakika wa matibabu,” alisema Mhe. Mchengerwa.
Kutokana na hayo, amesema kuwa kutakuwa na uzinduzi wa kihistoria wa Bima ya Afya kwa Wote kabla ya kukamilika kwa siku 100 za Mheshimiwa Rais, uzinduzi ambao utabadilisha dhana ya haki ya huduma za afya nchini Tanzania na kuweka msingi mpya wa ulinzi wa afya ya Mtanzania.
Aliwasisitiza viongozi hao kuwa kwa sasa ajenda ya Bima ya Afya kwa Wote lazima iondoke kwenye ngazi ya waraka na iingie kwenye maamuzi ya kila siku ya uongozi wa Mkoa.
Pia Soma: Gharama ya Bima ya Afya kwa wote ni Tsh. 150, 000 kwa kaya, wasio na uwezo kugharamiwa na serikali