Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
"Mwaka 2024/25 Ofisi ya Rais TAMISEMI iliidhinishiwa shilingi bilioni 254.82 kwa ajili ya kuratibu na kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 247.03 ni fedha kutoka serikali kuu na shilingi bilioni 7.78 ni fedha za mapato ya ndani ya halmashauri kwa ajili ya uchaguzi. Uchaguzi huu ulihusisha uchaguzi wa viongozi katika ngazi ya msingi ambao ni wenyeviti wa vijiji, mitaa, vitongoji, wajumbe wa halmashauri za vijiji na wajumbe wa kamati za mitaa"- Mchengerwa.
Waziri wa TAMISEMI Mohammed Mchengerwa ameyasema hayo Jumatano Aprili 16,2025 bungeni Jijini Dodomacwakati akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Waziri wa TAMISEMI Mohammed Mchengerwa ameyasema hayo Jumatano Aprili 16,2025 bungeni Jijini Dodomacwakati akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026.
