Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa, amesema kuwa serikali imetenga kiasi cha Shilingi bilioni 23.5 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vipya vya afya katika majimbo mbalimbali nchini, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa awamu ya pili ya mpango huo.
Mchengerwa ametoa taarifa hiyo, Jumamosi Julai 12, 2025, jijini Dodoma, wakati wa Mkutano wa Mwaka wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri kwa mwaka 2025, wenye kaulimbiu isemayo: “Wajibu wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri katika Kuimarisha Ubora wa Huduma za Afya kuelekea Bima ya Afya kwa Wote.”
Aidha, Waziri Mchengerwa amesema kuwa Serikali pia imetoa Shilingi bilioni 17.36 kwa ajili ya kukamilisha maboma ya zahanati 346 ambayo yalikuwa yameanzishwa na wananchi katika maeneo mbalimbali lakini hayajakamilika.
Mchengerwa ametoa taarifa hiyo, Jumamosi Julai 12, 2025, jijini Dodoma, wakati wa Mkutano wa Mwaka wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri kwa mwaka 2025, wenye kaulimbiu isemayo: “Wajibu wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri katika Kuimarisha Ubora wa Huduma za Afya kuelekea Bima ya Afya kwa Wote.”
Aidha, Waziri Mchengerwa amesema kuwa Serikali pia imetoa Shilingi bilioni 17.36 kwa ajili ya kukamilisha maboma ya zahanati 346 ambayo yalikuwa yameanzishwa na wananchi katika maeneo mbalimbali lakini hayajakamilika.