Mchango wa World Cup Kwenye Uchumi Wa AFRICA

ZionTZ

JF-Expert Member
Oct 6, 2009
1,283
538
wakulu natanguliza heshima kwanza kama utamaduni wetu wa ki-AFRICA ulivyo, siku nyingi nilitamani kuona mtu au watu waliopata manufaa kiuchumi direct kutoka na kombe la dunia, so nikaamua kufanya research hapa tanzania ni watu gani au makampuni gani yamepata faida kutokana na kombe hili,

Kutokana na research yangu nimefanikiwa kumpata mtu mmoja tu kutoka TZ, nae si mwingine bali ni Mzee Mengi, yeye kapata tenda ya kusuply maji ya KILIMANJARO world CUP 2010 south africa. Baada ya kuwini hiyo tenda ilibidi afwate masharti yao, walimtaka abadili muonekano wa chupa...na ndo mana siku hizi umeona hizi chupa mpya zina shepu tofauti na ile ya zamani. Mi napenda kumpa pongezi kubwa kwa kweli, kwa sababu kitendo cha kuuza maji yenye jina na nembo ya mlima wetu KILIMANJARO italeta impact fulani kwenye kampeni zetu za kukuza utalii tanzania. Pamoja ya kwamba coca-cola ndo wazamini wakuu kwenye kombe hili bado kitendo cha kupeleka maji yenye lebo inayoonyesha yametengenezwa tanzania na Ml. kilimanjaro ni jambo la kujivunia.

Big Up BONITE Bottlers LTD...Hakikisheni mnazidi kuongeza ubora kwenye product zenu ili kupitia hizo tuweze kukuza uchumi wetu pamoja na kuitangaza inchi yetu Duniani.

Wawakulu mnaweza kutuhabarisha watu wengine walionufaika na kombe la dunia especially wa tanzania.....??
 
Back
Top Bottom