mkiluvya
JF-Expert Member
- May 23, 2019
- 802
- 725
MSEMAJI Mkuu wa Serikali, Dk. Hassan Abbas, amesema Serikali imeagiza treni tano za kisasa ambazo kila moja itakuwa na mabehewa nane ambayo yatasafirisha abiria kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma.
Pia alisema Serikali haitarudi nyuma wala kusalimu amri, licha ya uwepo wa hujuma zinazofanyika kutaka kurudisha nyuma kasi ya maendeleo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa jana kuhusu utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimaendeleo nchini, Dk. Abbas alisema Serikali imeanza zabuni ya kuagiza vichwa 22, vitano vya mafuta yaani dizeli na 17 vya umeme na mabehewa ya abiria 60 na ya mizigo.
“Serikali imeanza zabuni ya treni tano zilizokamilika za abiria zenye mabehewa nane kila moja na vichwa viwili kwa ajili ya uendeshaji wa treni za abiria kwa kipande cha Dar– Moro na kisha Dodoma,” alieleza Dk. Abbasi.