GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,383
- 108,441
- Thread starter
- #21
Agreed !
Tena asali sana pia maana huu umri anaosema anao ukipiga hesabu alipokuwa Lyoni na Simba data zinagongana !!
Mkuu nakubaliana na wewe tena kwa 100% kuwa Waafrika wengi hasa WACHEZAJI mpira hupenda KUDANGANYA kuhusu UMRI wao ila kwa umri wa Mbwana Samatta HAJAONGOPA mkuu amini usiamini ila tatizo kubwa la sisi Waafrika na labda niseme kwetu hapa Tanzania huwa hatufanyi Scouting nzuri kwa Wachezaji wetu na kibaya zaidi hatuzingatii hata DOCUMENTATION. Kwa mfano nenda pale TFF sasa hivi uliza jambo tu la mwaka 1985 au 1990 ukilikuta ni MSALIA MTUME. Mbwana nisiwe mwongo bado ni mdogo na hata huo UMRI wake ni sahihi nenda kokote kaulize isipokuwa kuna Wachezaji leo naambiwa bado wadogo mfano Nahodha wa Mtibwa Shaaban Nditi nasikia hata katika Passport yake imeandikwa NJEMBA ndiyo kwanza Inagonga 26 sasa tizama NYAGO lake ongeza na UNYUMBULIFU wake uwanjani kisha JIONGEZE.