Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,760
- 40,971
MBUZI ISOKUNA NAZI?
Macho puu yanitoka, nimepigwa na butwaa,
Na taya limedondoka, nimebaki kushangaa,
Moyo umenishituka, pumzi imenipaa,
Mbuzi isokuna nazi, ni bora kuiachiya!
Jikoni mumeiweka, hiyo mbuzi inangaa,
Kwenye ghala mwatundika, eti hiyo yawafaa,
Kukuna kunapofika, mbuzi mnaiandaa,
Mbuzi isokuna nazi, bora mbali kutupiya!
Eti mbuzi ya hakika, sifa mnazitangaa,
Mwajivuna mwadundika, mbona mwaleta balaa,
Mbuzi hiyo imechoka, acheni wenu unaa,
Mbuzi isokuna nazi, haifahi kukuniya!
Mbuzi zenu zavunjika, ya kwangu miye ayeyaa,
Tena inaazimika, ikakuna kwa staa,
Na nazi ikakunika, mapishi yakakufaa,
Mbuzi isokuna nazi, ni mbuzi yao vichaa!
Nimechoka kuandika, kalamu yanidondokaa,
Ukweli huu hakika, hadharani wazagaa,
Mbuzi iloharibika, kukuna haitafaa,
Mbuzi isokuna nazi, kwanini mwaikalia?
Macho puu yanitoka, nimepigwa na butwaa,
Na taya limedondoka, nimebaki kushangaa,
Moyo umenishituka, pumzi imenipaa,
Mbuzi isokuna nazi, ni bora kuiachiya!
Jikoni mumeiweka, hiyo mbuzi inangaa,
Kwenye ghala mwatundika, eti hiyo yawafaa,
Kukuna kunapofika, mbuzi mnaiandaa,
Mbuzi isokuna nazi, bora mbali kutupiya!
Eti mbuzi ya hakika, sifa mnazitangaa,
Mwajivuna mwadundika, mbona mwaleta balaa,
Mbuzi hiyo imechoka, acheni wenu unaa,
Mbuzi isokuna nazi, haifahi kukuniya!
Mbuzi zenu zavunjika, ya kwangu miye ayeyaa,
Tena inaazimika, ikakuna kwa staa,
Na nazi ikakunika, mapishi yakakufaa,
Mbuzi isokuna nazi, ni mbuzi yao vichaa!
Nimechoka kuandika, kalamu yanidondokaa,
Ukweli huu hakika, hadharani wazagaa,
Mbuzi iloharibika, kukuna haitafaa,
Mbuzi isokuna nazi, kwanini mwaikalia?