Mbunge Zungu, hapa unachemsha vibaya!!!

Mbunge Zungu, hapa unachemsha vibaya!!!

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,647
Reaction score
14,646
Mbunge wa Ilala Musa Zungu ananishangaza.
Utafikiri katumwa bungeni na wamachinga, na kwa maslahi ya wamachinga.

Mimi nikitegemea kama mkazi wa Jiji la Dar es salaam, angekewa na mawazo endelevu kwa kuliboresha Jiji, ili liwe sawa na miji mingi aliyotembelea duniani.

Kwa siku kadhaa sasa kajipachika kuwa msemaji wa wamachinga, suala amnayo kimsingi ni kutetea tu maslahi ambayo naona no binafsi.
Maslahi binafsi yanakuja pale tunapoona 2015 inazidi kusogea.

Machinga kama msingi wa ajira kwa vijana si endelevu na mbaya zaidi ktetea machinga ni kutetea ukwepaji wa kodi ya mauzo.

Sasa mtu mzima kutetea mfumo ambao kimsingi ni ukiukwaji wa taratibu endelevu za kuendesha jiji, mimi inanitia wasiwasi.Kuna Machinga Co,pex pale Ilala, Zungu kimya!!!

Inabidi Zungu aambiwe kuwa kama hana cha kuonyesha kwa miaka yake mitano bungeni ajihukumu mwenyewe, ama sivyo kelele za kutetea umachinga kwa hakika zinakera.
 
Nilistuka nilipo soma Gazeti moja la kila siku nikakuta akiwashutumu RC na Mkurugenzi wa Jiji kwa kuwaondoa Wamachinga ktkt ya Jiji. Badala ya kuwaunga mkono kwa jitihada zao za kulisafisha na kulipendezesha Jiji anaomba Rais awatimue kibarua! Kiongozi aina ya Zungu haifai Dar es Salaam! Bila shaka chama chake kitamtafuta mtu bora zaidi kugombea Ubunge wa Ilala.
 
Nilistuka nilipo soma Gazeti moja la kila siku nikakuta akiwashutumu RC na Mkurugenzi wa Jiji kwa kuwaondoa Wamachinga ktkt ya Jiji. Badala ya kuwaunga mkono kwa jitihada zao za kulisafisha na kulipendezesha Jiji anaomba Rais awatimue kibarua! Kiongozi aina ya Zungu haifai Dar es Salaam! Bila shaka chama chake kitamtafuta mtu bora zaidi kugombea Ubunge wa Ilala.
Mkuu wa Mkoa wa DSM ni mtu makini sana na kila mtu anajua hilo.

Ila huyu Zungu nafikiri ana matatizo fulani, ila kutetea dhana ya umachinga ni kushikilia unyasi!!
Anazama huyo.
 
Zungu anafanya old fashioned politics
Hazita mwongezea kura, come 2015.
 
Mbunge wa Ilala Musa Zungu ananishangaza.
Utafikiri katumwa bungeni na wamachinga, na kwa maslahi ya wamachinga.

Mimi nikitegemea kama mkazi wa Jiji la Dar es salaam, angekewa na mawazo endelevu kwa kuliboresha Jiji, ili liwe sawa na miji mingi aliyotembelea duniani.

Kwa siku kadhaa sasa kajipachika kuwa msemaji wa wamachinga, suala amnayo kimsingi ni kutetea tu maslahi ambayo naona no binafsi.
Maslahi binafsi yanakuja pale tunapoona 2015 inazidi kusogea.

Machinga kama msingi wa ajira kwa vijana si endelevu na mbaya zaidi ktetea machinga ni kutetea ukwepaji wa kodi ya mauzo.

Sasa mtu mzima kutetea mfumo ambao kimsingi ni ukiukwaji wa taratibu endelevu za kuendesha jiji, mimi inanitia wasiwasi.Kuna Machinga Co,pex pale Ilala, Zungu kimya!!!

Inabidi Zungu aambiwe kuwa kama hana cha kuonyesha kwa miaka yake mitano bungeni ajihukumu mwenyewe, ama sivyo kelele za kutetea umachinga kwa hakika zinakera.

Kaka kama wewe unaajira ya serikali au iliyo rasmi poa,lakini kwa ndugu zetu wanaoitwa machinga tunampongeza sana mh,Zungu kwani ameonyesha kutujali sana kuliko hayo magamba wengine na atachaguliwa tena 2015.
 
Kaka kama wewe unaajira ya serikali au iliyo rasmi poa,lakini kwa ndugu zetu wanaoitwa machinga tunampongeza sana mh,Zungu kwani ameonyesha kutujali sana kuliko hayo magamba wengine na atachaguliwa tena 2015.

Huyu unayemtetea hawasaidii wana ilala kwa ujumla wake, waliomchagua ni wananchi wa Ilala, kuruhusu watu kuudha bidhaa sehemu zisizo rasmi si kuwasaidia wana Ilala kwa upana wake.

Nafahamu na nina uhakika wa asilimia 100 huyu bwana ana-loby kw anguvu kubwa sana kubadilisha matumizi ya ardhi ya moja ya maeneo makubwa zaidi ya ardhi ya wazi hapo ilala,ili iwe kwa ajili ya matumizi binafsi, kupeleka kelele bungeni wakurugenzi wafukuzwe ni njia rahisi kwa akili yake ndogo ya ku-create havoc kufanikisha mipango yake.
Ni jambo la kusikitisha,kuwa wananchi wa ilala waliamu akuchagua mtu mwenye simple mind kama huyu, sasa watapata wanachokitaka,pindi watakapogundua jamaa kabinafsisha park zao.
 
2015 haiko mbali kwa hiyo anatafuta atoke vipi!
do not trust a politician even a single minute.
 
Kaka kama wewe unaajira ya serikali au iliyo rasmi poa,lakini kwa ndugu zetu wanaoitwa machinga tunampongeza sana mh,Zungu kwani ameonyesha kutujali sana kuliko hayo magamba wengine na atachaguliwa tena 2015.

Wafanyabiashara ndogo hawawezi achiwa kuzunguka hovyo bila mpangilio. Tunapo sifia miji ya Ulaya,America na Asia ni kwamba kuna utaratibu siyo kila mtu kuibuka huko atokako kuja mjini kupanga bidhaa barabarani.
 
Wafanyabiashara ndogo hawawezi achiwa kuzunguka hovyo bila mpangilio. Tunapo sifia miji ya Ulaya,America na Asia ni kwamba kuna utaratibu siyo kila mtu kuibuka huko atokako kuja mjini kupanga bidhaa barabarani.

OK,kama serikali imefanya juhudi gani kuwasaidia hao wamachinga?
 
Zungu bure kabisa siku hizi kariakoo panapendeza na maduka yanafikika.Siasa za tanzania ni adui wa maendeleo
 
hongera sana zungu, tanzania ni yetu sote, asante kwa kujali machinga!
 
Kaka kama wewe unaajira ya serikali au iliyo rasmi poa,lakini kwa ndugu zetu wanaoitwa machinga tunampongeza sana mh,Zungu kwani ameonyesha kutujali sana kuliko hayo magamba wengine na atachaguliwa tena 2015.
Mkuu kuna kitu kinaitwa anarchy, its not an option to poverty!
Na kwa taarifa yako najiajiri vile vile.
 
OK,kama serikali imefanya juhudi gani kuwasaidia hao wamachinga?
Mtu kama Zungu wamechaguliwa kuongoza ili majawabu ya tatizo hilo yapatikane.
Sasa kiongozi anapokuwa hana akili sawasawa na hana mawazo zaidi ya umachinga hicho ni kiama.

Machinga complex ipo Ilala, tunauliza kwa nini haitumiki?
Tatizo lililopo ni kuwa na mawazo finyu kama hao kina Zungu.
 
yote aliyoyazungumza zungu ni sahihi kabisa,watanzania waliowengi wanauchumi mdogo na wanaishi kwa kazi hizo wana family wana somesha wana wake wana wategemezi wajaliwe! pia hoja yake ya vocha kuwa pre~taxed na ikibidi mapato yake yakasoma direct tra nimemuunga mkono by 100%,tena nashauri isiishie hapo hata bus ticket daladala na za mikoani zitengenezewe mfumo kwani ktk kila ticket ya 500/-za daladala serikali ikichukuwa 30/-kwa abiria wote wa jiji hili almost 2ml,hata tukiachana na propert tax ya vijumba vya wastaafu nchi itasonga HONGERA MB. ZUNGU ILALA YAMEREMETA!
 
Mtu kama Zungu wamechaguliwa kuongoza ili majawabu ya tatizo hilo yapatikane.
Sasa kiongozi anapokuwa hana akili sawasawa na hana mawazo zaidi ya umachinga hicho ni kiama.

Machinga complex ipo Ilala, tunauliza kwa nini haitumiki?
Tatizo lililopo ni kuwa na mawazo finyu kama hao kina Zungu.

Hao wamachinga si ndiyo anawashikisha sembe, sasa wanafukuzwa na yeye anafikiria li biashara lake la sembe itakuwaje na mtaji wa 2015. Heheheee ...!!!
 
Hao wamachinga si ndiyo anawashikisha sembe, sasa wanafukuzwa na yeye anafikiria li biashara lake la sembe itakuwaje na mtaji wa 2015. Heheheee ...!!!

Mkuu umechanganya huyu ni wa ilala na siyo kinondoni
 
yote aliyoyazungumza zungu ni sahihi kabisa,watanzania waliowengi wanauchumi mdogo na wanaishi kwa kazi hizo wana family wana somesha wana wake wana wategemezi wajaliwe! pia hoja yake ya vocha kuwa pre~taxed na ikibidi mapato yake yakasoma direct tra nimemuunga mkono by 100%,tena nashauri isiishie hapo hata bus ticket daladala na za mikoani zitengenezewe mfumo kwani ktk kila ticket ya 500/-za daladala serikali ikichukuwa 30/-kwa abiria wote wa jiji hili almost 2ml,hata tukiachana na propert tax ya vijumba vya wastaafu nchi itasonga HONGERA MB. ZUNGU ILALA YAMEREMETA!
You are off the rails!
Kama kupanga bi dhaa barabarani ni dili (kama Zungu anavyotaka) basi hata uwanja wa ndege wanapotua wazito wakazipange bidhaa hizo.
Basically hii ni thinking ya morons.
 
Mwacheni ZUNGU jamani!!!!

Machinga wote wakiondolewa atamuuzia nani DAWA???
 
Back
Top Bottom