Mbunge: Watendaji wanamdharau rais

sulphadoxine

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
2,257
645
WABUNGE wameendelea kuirarua serikali katika mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kuhusu mambo mbalimbali hasa utendaji wake na baadhi wakienda mbali
wakisema kuwa wapo watendaji wanaomdharua Rais Jakaya Kikwete.

Miongoni mwa wabunge hao ni Bw. Salum Baruany (Lindi Mjini-CUF), aliyesema kuwa kutotekelezeka kwa ahadi za Rais Kikwete katika maeneo mbalimbali nchini ni dalili kwamba watendaji kumdharau rais wao.

“Ahadi za rais si ahadi za kufanyia mchezo kwa kuwa kauli yake ni nzito na huwa ni ya mwisho, lakini pia kauli yake inaizidi hata sheria. Lindi alikuja na kuahidi mambo mengi ikiwemo bandari, soko na nyingine nyingi, na sasa amebakiza
miaka mitatu kumaliza mkataba wake wa urais na hakijafanyika chochote na hii inaonesha au ina maana kuwa serikali mnamdharau rais wenu,” alisema.

Alisema kuwa kuna mambo mengi ya kimaendeleo ambayo yamekwama na kusababisha nchi kushindwa kupiga hatua kutokana na watendaji kutowajibika.

Mbunge huyo alisema kuwa wananchi kila kona wanalalamikia mambo mbalimbali yakiwemo ya ajira ambazo alieleza kuwa zimeghubikwa na kujuana na ukabila.

“Mfano mzuri ni kwenye kada ya majeshi yetu, ajira za polisi na majeshi mengine kwa sasa zinapatikana kwa kujuana, mtu akiwa RPC sehemu fulani anaita ukoo wake wote na hii tusipoangalia italeta hatari hapo baadaye,” alisema.

Suala jingine alilozungumzia ni tatizo la mauaji ya albino, ambapo aliitaka serikali kutoa tamko ni hatua gani zilizofikiwa na serikali katika kukomesha tatizo hili na kudhibiti tatizo jingine ambalo lipo sasa la walemavu hao kupotea katika mazingira ya kutatanisha.

Mbunge huyo ambaye pia ni albino, alisema kuwa dalili zinaonesha kuwa biashara hiyo haramu ya viungo vya albino, ilikuwa inafanywa na watu wenye uwezo mkubwa kwa kuwa viungo hivyo viliuzwa kwa gharama kubwa kama sh. milioni 200 hadi 400.

Alisema kuwa kiwango hicho cha fedha kisingekuwa rahisi kwa watu wenye uwezo wa chini, hivyo akashauri ni vyema ukafanyika utafiti kubaini watu hao, huku akiomba kundi la walemavu kuingizwa katika wizara mtambuka na si kubaki katika Wizara ya
Afya na Ustawi wa Jamii.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kasulu Mjini, Bw. Moses Machali, alisema kuwa pamoja na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kujisifu kuwa imefanya mambo makubwa ndani ya kipindi cha miaka 50 ya uhuru, lakini alisema yaliyofanywa hayalingani na
kipindi hicho.
 
Back
Top Bottom